Zaburi 31:1-8
Zaburi 31
Maombi Na Sifa Kwa Kuokolewa Kutoka Kwa Adui
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
31:1 Za 7:1; 5:8Ee Bwana, nimekukimbilia wewe,
usiache nikaaibika kamwe,
kwa haki yako uniokoe.
31:2 Za 6:4Nitegee sikio lako,
uje uniokoe haraka;
uwe kwangu mwamba wa kimbilio,
ngome imara ya kuniokoa.
31:3 Za 18:2; 23:3; Yer 14:7Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu,
uniongoze na kunilinda kwa ajili ya jina lako.
31:4 1Sam 28:9; Ay 18:10; Za 9:9Uniepushe na mtego niliotegewa,
maana wewe ndiwe kimbilio langu.
31:5 Lk 23:46; Ebr 6:18; Mdo 7:59; Isa 45:19; 65:16; 2Tim 1:12Ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako,
unikomboe Ee Bwana, uliye Mungu wa kweli.
31:6 Kum 32:21; Za 4:5Ninawachukia wale wanaongʼangʼania sanamu batili;
mimi ninamtumaini Bwana.
31:7 Yn 10:27; Lk 22:44; Za 25:17Nitafurahia na kushangilia upendo wako,
kwa kuwa uliona mateso yangu
na ulijua maumivu ya nafsi yangu.
31:8 Za 18:19; Kum 32:30; 2Sam 22:20Hukunikabidhi kwa adui yangu
bali umeiweka miguu yangu mahali penye nafasi.