Zaburi 30:8-12
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita,
kwa Bwana niliomba rehema:
30:9 Ay 33:18; Isa 38:18; Za 6:5; 88:11; 115:17“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu?
Katika kushuka kwangu shimoni?
Je, mavumbi yatakusifu?
Je, yatatangaza uaminifu wako?
30:10 Za 17:1; 4:1; 20:2Ee Bwana, unisikie na kunihurumia,
Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
30:11 2Sam 3:31; 6:14; Es 4:1; Kut 15:20; Za 35:13; 16:9; Kum 16:15Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza,
ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
30:12 Za 35:18; 75:1; 118:21; 44:8; 52:9; Ufu 11:17ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya.
Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.