Zaburi 148:1-6
Zaburi 148
Mwito Kwa Ulimwengu Kumsifu Mungu
148:1 Za 33:2; 103; 1; 19:1; 69:34; 150:1Msifuni Bwana.
Msifuni Bwana kutoka mbinguni,
msifuni juu vileleni.
148:2 Za 103:20; 1Fal 22:19; Dan 7:10; Ebr 1:7Msifuni, enyi malaika wake wote,
msifuni yeye, enyi jeshi lake lote la mbinguni.
148:3 Za 19:1Msifuni yeye, enyi jua na mwezi,
msifuni yeye, enyi nyota zote zingʼaazo.
148:4 Kum 10:14; Mwa 1:7; 1Fal 8:27Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu sana,
na ninyi maji juu ya anga.
148:5 Za 145:21; 147:15; Ebr 11:3Vilisifu jina la Bwana
kwa maana aliamuru navyo vikaumbwa.
148:6 Yer 31:35-36; 33:25; 33:25Aliviweka mahali pake milele na milele,
alitoa amri ambayo haibadiliki milele.