Zaburi 144:1-8 NEN

Zaburi 144:1-8

Zaburi 144

Mfalme Amshukuru Mungu Kwa Ushindi

Zaburi ya Daudi.

144:1 Mwa 49:24; 2Sam 22:35Sifa ni kwa Bwana Mwamba wangu,

aifundishaye mikono yangu vita,

na vidole vyangu kupigana.

144:2 Za 59:9; 91:2; 18:39; 27:1; 37:39; 43:2; 18:2; Amu 4:23; Mwa 15:1Yeye ni Mungu wangu wa upendo na boma langu,

ngome yangu na mwokozi wangu,

ngao yangu ninayemkimbilia,

ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.

144:3 Ebr 2:6Ee Bwana, mwanadamu ni nini hata umjali,

Binadamu ni nini hata umfikirie?

144:4 Ay 7:7; 27:3; 14:2; Isa 2:22; 1Nya 29:15; Yak 4:14Mwanadamu ni kama pumzi,

siku zake ni kama kivuli kinachopita.

144:5 Za 18:9; 57:3; 104:32; Isa 64:1; Mwa 11:5Ee Bwana, pasua mbingu zako, ushuke,

gusa milima ili itoe moshi.

144:6 Hab 3:11; Zek 9:14; Za 59:11; 68:1; 7:12, 13; 18:14Peleka umeme uwatawanye adui,

lenga mishale yako uwashinde.

144:7 2Sam 22:17; Za 3:7; 57:3; 69:2; 18:44Nyoosha mkono wako kutoka juu,

nikomboe na kuniokoa

kutoka maji makuu,

kutoka mikononi mwa wageni

144:8 Za 12:2; 41:6; 26:3; Mwa 14:22; Kum 32:40ambao vinywa vyao vimejaa uongo,

na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.

Read More of Zaburi 144