Zaburi 144:1-8
Zaburi 144
Mfalme Amshukuru Mungu Kwa Ushindi
Zaburi ya Daudi.
144:1 Mwa 49:24; 2Sam 22:35Sifa ni kwa Bwana Mwamba wangu,
aifundishaye mikono yangu vita,
na vidole vyangu kupigana.
144:2 Za 59:9; 91:2; 18:39; 27:1; 37:39; 43:2; 18:2; Amu 4:23; Mwa 15:1Yeye ni Mungu wangu wa upendo na boma langu,
ngome yangu na mwokozi wangu,
ngao yangu ninayemkimbilia,
ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
144:3 Ebr 2:6Ee Bwana, mwanadamu ni nini hata umjali,
Binadamu ni nini hata umfikirie?
144:4 Ay 7:7; 27:3; 14:2; Isa 2:22; 1Nya 29:15; Yak 4:14Mwanadamu ni kama pumzi,
siku zake ni kama kivuli kinachopita.
144:5 Za 18:9; 57:3; 104:32; Isa 64:1; Mwa 11:5Ee Bwana, pasua mbingu zako, ushuke,
gusa milima ili itoe moshi.
144:6 Hab 3:11; Zek 9:14; Za 59:11; 68:1; 7:12, 13; 18:14Peleka umeme uwatawanye adui,
lenga mishale yako uwashinde.
144:7 2Sam 22:17; Za 3:7; 57:3; 69:2; 18:44Nyoosha mkono wako kutoka juu,
nikomboe na kuniokoa
kutoka maji makuu,
kutoka mikononi mwa wageni
144:8 Za 12:2; 41:6; 26:3; Mwa 14:22; Kum 32:40ambao vinywa vyao vimejaa uongo,
na mikono yao ya kuume ni midanganyifu.