Zaburi 119:9-16 NEN

Zaburi 119:9-16

Kutii Sheria Ya Bwana

119:9 Za 119:65, 169; 39:1; Mit 1:4, 10Kijana aifanye njia yake kuwa safi jinsi gani?

Ni kwa kutii, akilifuata neno lako.

119:10 Za 119:21, 118; 9:1; 2Nya 15:15Ninakutafuta kwa moyo wangu wote,

usiniache niende mbali na amri zako.

119:11 Isa 63:13; Mit 3:23; Za 119:133, 165; 18:22-23; Kum 6:6; Lk 2:19; Ay 22:22Nimelificha neno lako moyoni mwangu

ili nisikutende dhambi.

119:12 Isa 63:13; Lk 2:19Sifa ni zako, Ee Bwana,

nifundishe maagizo yako.

119:13 Za 119:72Kwa midomo yangu nitasimulia sheria zote

zinazotoka katika kinywa chako.

119:14 Za 119:111Ninafurahia kufuata sheria zako

kama mtu afurahiaye mali nyingi.

119:15 Za 119:97, 148; 1:2Ninatafakari maagizo yako

na kuziangalia njia zako.

119:16 Za 112:1Ninafurahia maagizo yako,

wala sitalipuuza neno lako.

Read More of Zaburi 119