Zaburi 119:137-144
Haki Ya Sheria Ya Bwana
119:137 Kut 9:27; Ezr 9:15; Neh 9:13, 33; Yer 12:1; Dan 9:7Ee Bwana, wewe ni mwenye haki,
sheria zako ni sahihi.
119:138 Za 119:75, 86; 19:7Sheria ulizoziweka ni za haki,
ni za kuaminika kikamilifu.
119:139 Za 69:9; Yn 2:17Jitihada yangu imenidhoofisha, kwa kuwa adui zangu
wanayapuuza maneno yako.
119:140 Yos 23:14; Za 12:6; 119:47Ahadi zako zimejaribiwa kikamilifu,
mtumishi wako anazipenda.
119:141 Za 22:6; 119:61, 134; Mit 15:16; Amo 7:2; Lk 6:20; 2Kor 8:9; Yak 2:5Ingawa ni mdogo na ninadharauliwa,
sisahau mausia yako.
119:142 Za 119:151, 160; 19:7, 9; Yn 17:17; Efe 1:3Haki yako ni ya milele,
na sheria yako ni kweli.
119:143 Za 119:24, 47Shida na dhiki zimenipata,
lakini amri zako ni furaha yangu.
119:144 Za 119:34Sheria zako ni sahihi milele,
hunipa ufahamu ili nipate kuishi.