Mithali 9:1-12
Makaribisho Ya Hekima Na Ya Upumbavu
9:1 Efe 2:20-22; 1Tim 3:15; 1Pet 3:5Hekima amejenga nyumba yake;
amechonga nguzo zake saba.
9:2 Lk 14:16-23; Isa 25:6; 62:8Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake;
pia ameandaa meza yake.
9:3 Mit 1:20; 8:1-3; Mt 22:3, 4, 9; Lk 14:17; Rum 10:15Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita
kutoka mahali pa juu sana pa mji.
9:4 Mit 1:22; 6:32; Mt 11:25Anawaambia wale wasio na akili,
“Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
9:5 Za 42:2; Isa 44:3; Mt 26:26-28Njooni, mle chakula changu
na mnywe divai niliyoichanganya.
9:6 Mit 8:35; 3:1-2Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi;
tembeeni katika njia ya ufahamu.
9:7 Mit 23:9; Mt 7:6“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha
hukaribisha matukano;
yeyote anayekemea mtu mwovu
hupatwa na matusi.
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia;
mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9:9 Mit 15:31; 19:25; Mt 13:12Mfundishe mtu mwenye hekima
naye atakuwa na hekima zaidi;
mfundishe mtu mwadilifu
naye atazidi kufundishika.
9:10 Ay 28:28“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima,
na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
9:11 Mwa 15:15; Kum 11:21; Mit 10:27Kwa maana kwa msaada wangu
siku zako zitakuwa nyingi,
na miaka itaongezwa katika maisha yako.
9:12 Ay 35:6, 7Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo;
kama wewe ni mtu wa mzaha,
wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”