Mithali 9:1-12 NEN

Mithali 9:1-12

Makaribisho Ya Hekima Na Ya Upumbavu

9:1 Efe 2:20-22; 1Tim 3:15; 1Pet 3:5Hekima amejenga nyumba yake;

amechonga nguzo zake saba.

9:2 Lk 14:16-23; Isa 25:6; 62:8Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake;

pia ameandaa meza yake.

9:3 Mit 1:20; 8:1-3; Mt 22:3, 4, 9; Lk 14:17; Rum 10:15Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita

kutoka mahali pa juu sana pa mji.

9:4 Mit 1:22; 6:32; Mt 11:25Anawaambia wale wasio na akili,

“Wote ambao ni wajinga na waje hapa!

9:5 Za 42:2; Isa 44:3; Mt 26:26-28Njooni, mle chakula changu

na mnywe divai niliyoichanganya.

9:6 Mit 8:35; 3:1-2Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi;

tembeeni katika njia ya ufahamu.

9:7 Mit 23:9; Mt 7:6“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha

hukaribisha matukano;

yeyote anayekemea mtu mwovu

hupatwa na matusi.

Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia;

mkemee mwenye hekima naye atakupenda.

9:9 Mit 15:31; 19:25; Mt 13:12Mfundishe mtu mwenye hekima

naye atakuwa na hekima zaidi;

mfundishe mtu mwadilifu

naye atazidi kufundishika.

9:10 Ay 28:28“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima,

na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.

9:11 Mwa 15:15; Kum 11:21; Mit 10:27Kwa maana kwa msaada wangu

siku zako zitakuwa nyingi,

na miaka itaongezwa katika maisha yako.

9:12 Ay 35:6, 7Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo;

kama wewe ni mtu wa mzaha,

wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”

Read More of Mithali 9