Mithali 8:12-21
8:12 Mit 1:4“Mimi hekima, nakaa pamoja na busara;
ninamiliki maarifa na busara.
8:13 Kut 20:20; Yer 44:4; Zek 8:17; Mit 16:6Kumcha Bwana ni kuchukia uovu;
ninachukia kiburi na majivuno,
tabia mbaya na mazungumzo potovu.
8:14 Mhu 7:19; Ay 9:4Ushauri na hukumu sahihi ni vyangu;
nina ufahamu na nina nguvu.
8:15 Dan 2:21; Mt 28:18; Rum 13:1Kwa msaada wangu wafalme hutawala
na watawala hutunga sheria zilizo za haki,
8:16 2Nya 1:10; Mit 29:4kwa msaada wangu wakuu hutawala,
na wenye vyeo wote watawalao dunia.
8:17 Za 91:14; Yn 14:21-24; 1Sam 2:30; Yak 1:5Nawapenda wale wanipendao,
na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
8:18 Mt 6:33; 1Fal 3:13; Kum 8:18; Mit 3:16Utajiri na heshima viko kwangu,
utajiri udumuo na mafanikio.
8:19 Mit 3:13-14; 10:20Tunda langu ni bora kuliko dhahabu safi;
kile nitoacho hupita fedha iliyo bora.
Natembea katika njia ya unyofu
katika mapito ya haki,
8:21 Mit 15:6; 24:4nawapa utajiri wale wanipendao
na kuzijaza hazina zao.