Mithali 4:10-19
4:10 Kum 11:21; Mit 3:2Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia,
nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
4:11 1Sam 12:23; 2Sam 22:37; Za 5:8Ninakuongoza katika njia ya hekima
na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.
4:12 Ay 18:7; Yer 13:16; Za 18:36Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa;
ukimbiapo, hutajikwaa.
4:13 Mit 3:22Mkamate sana elimu, usimwache aende zake;
mshike, maana yeye ni uzima wako.
4:14 Za 1:1; Mit 1:15Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu
wala usitembee katika njia ya watu wabaya.
Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo;
achana nayo, na uelekee njia yako.
4:16 Za 36:4; Mik 7:3Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu;
wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.
4:17 Mwa 49:5; Za 73:6; Mit 1:10-19; Isa 59:6; Yer 22:3; Hab 1:2; Mal 2:16Wanakula mkate wa uovu,
na kunywa mvinyo wa jeuri.
4:18 Mt 5:14; Ay 17:9; Isa 26:7; Dan 12:3; Yn 8:12Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko,
ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.
4:19 Ay 18:5; Yn 12:35Lakini njia ya waovu ni kama giza nene;
hawajui kinachowafanya wajikwae.