Mithali 31:1-9
Misemo Ya Mfalme Lemueli
31:1 Mit 22:17Misemo ya Mfalme Lemueli, usia wa mama yake aliyomfundisha:
31:2 Amu 11:30; Isa 49:15“Ee mwanangu, ee mwana wa tumbo langu,
ee mwana wa nadhiri zangu,31:2 Au: Ewe uliye jibu la maombi yangu.
31:3 Neh 13:26; Kum 17:17; Hos 4:11; 1Fal 11:3Usitumie nguvu zako kwa wanawake,
uhodari wako kwa wale wanaowaharibu wafalme.
31:4 Mhu 10:17; Isa 5:22“Ee Lemueli, haifai wafalme,
haifai wafalme kunywa mvinyo,
haifai watawala kutamani sana kileo,
31:5 1Fal 16:9; Mit 16:12; Hos 4:11wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru
na kuwanyima haki zao wote walioonewa.
31:6 Mwa 14:18Wape kileo wale wanaoangamia,
mvinyo wale walio na uchungu,
31:7 Es 1:10Wanywe na kusahau umaskini wao
na wasikumbuke taabu yao tena.
31:8 1Sam 19:4; Es 4:16; Ay 29:12-17“Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea,
kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa.
31:9 Law 19:15; Yer 22:16; Kum 1:16; Isa 1:17Sema na uamue kwa haki,
tetea haki za maskini na wahitaji.”