Mithali 25:11-20 NEN

Mithali 25:11-20

25:11 Mit 15:23; Isa 50:4Neno lisemwalo kwa wakati ufaao

ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu

yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.

25:12 Za 141:5; Mit 15:31Kama vile kipuli cha dhahabu

au pambo la dhahabu safi,

ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima

kwa sikio lisikilizalo.

25:13 Mit 13:17; 10:26Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno

ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao,

huburudisha roho za bwana zake.

25:14 Mit 20:6; Yud 12Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua

ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.

25:15 Mhu 10:4; Mit 15:1; Mwa 32:4; 1Sam 25:24Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa,

nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.

25:16 Mit 25:27Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha,

ukila zaidi, utatapika.

Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache,

ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.

25:18 Za 57:4; Mit 12:18Kama vile rungu au upanga au mshale mkali

ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.

25:19 Ay 6:14-20; 2Tim 4:16Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa,

ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.

25:20 Dan 6:18; Rum 12:15Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi,

au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi,

ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.

Read More of Mithali 25