Mithali 17:15-24 NEN

Mithali 17:15-24

17:15 Za 94:21; Kut 23:6-7; Mit 18:5; Mao 3:34-36; Isa 5:23Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki,

naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki:

Bwana huwachukia sana wote wawili.

17:16 Mit 23:23Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu,

wakati yeye hana haja ya kupata hekima?

17:17 2Sam 15:21; Mit 27:10Rafiki hupenda wakati wote

naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.

17:18 Mit 6:1-5; 11:5Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani,

naye huweka dhamana kwa jirani yake.

Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi;

naye ainuaye sana lango lake17:19 Kuinua lango maana yake ni kusema kwa majivuno. hutafuta uharibifu.

Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa;

naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.

17:21 Mit 10:1Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni;

hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.

17:22 Kut 12:46; Za 22:15Moyo wenye furaha ni dawa nzuri,

bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.

17:23 Kut 18:21; 1Sam 8:3Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri

ili kupotosha njia ya haki.

17:24 Ay 31:1; Mhu 2:14Mtu wa ufahamu huitazama hekima,

lakini macho ya mpumbavu huhangaika

hadi kwenye miisho ya dunia.

Read More of Mithali 17