Mithali 13:20-25, Mithali 14:1-4 NEN

Mithali 13:20-25

13:20 2Nya 10:8Yeye atembeaye na mwenye hekima atapata hekima,

bali rafiki wa mpumbavu hupata madhara.

13:21 Za 32:10; Mit 19:17; 11:12Balaa humwandama mtenda dhambi,

bali mafanikio ni thawabu kwa mwenye haki.

13:22 Es 8:2; Mhu 2:26Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi,

bali mali ya wenye dhambi imehifadhiwa

kwa ajili ya wenye haki.

13:23 Mit 12:11Shamba la mtu maskini laweza kuzalisha chakula kingi,

bali dhuluma hukifutilia mbali.

13:24 Mit 29:15-17; Efe 6:4Yeye aizuiaye fimbo yake hampendi mwanawe,

bali yeye ampendaye

huwa mwangalifu kumwadibisha.

13:25 Za 34:10; Mit 10:3Mwenye haki hula mpaka akaridhisha moyo wake,

bali tumbo la mwovu hutaabika kwa njaa.

Read More of Mithali 13

Mithali 14:1-4

14:1 Rut 3:11; Mit 24:3Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake,

bali mpumbavu huibomoa nyumba yake

kwa mikono yake mwenyewe.

14:2 Ay 12:4Yeye ambaye njia zake ni nyofu humcha Bwana,

bali yeye ambaye njia zake zimepotoka humdharau Mungu.

14:3 Mit 12:6; 10:13Mazungumzo ya mpumbavu huleta fimbo mgongoni mwake,

bali mwenye hekima hulindwa na maneno ya midomo yake.

14:4 Za 12:2; Mit 12:17Pale ambapo hakuna mafahali, hori ni tupu,

bali kutokana na nguvu za fahali huja mavuno mengi.

Read More of Mithali 14