Mithali 12:28
12:28 Kum 30:15; Rum 5:21; Mit 10:2Katika njia ya haki kuna uzima;
katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
Mithali 13:1-9
Mema Ya Muda Mfupi Na Yale Ya Kudumu
13:1 1Sam 2:25; Mit 10:1; 12:1; 15:5Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya babaye,
bali mwenye dharau hasikilizi maonyo.
13:2 Mit 12:14Kutoka tunda la midomo yake mtu hufurahia mambo mema,
bali wasio waaminifu wanatamani sana jeuri.
13:3 Za 12:2; Yak 3:2; Mit 10:6; Ay 1:22Yeye alindaye midomo yake hulinda nafsi yake,
bali yeye asemaye kwa haraka ataangamia.
13:4 Mit 21:25-26Mvivu hutamani sana na hapati kitu,
bali nafsi ya mwenye bidii
hutoshelezwa kikamilifu.
13:5 Kol 3:9; Rum 12:9Mwenye haki huchukia uongo,
bali waovu huleta aibu na fedheha.
13:6 Mit 11:3-5; Yer 44:5Haki humlinda mtu mwadilifu,
bali uovu humwangusha mwenye dhambi.
13:7 2Kor 6:10Mtu mmoja hujifanya tajiri, kumbe hana chochote;
mwingine hujifanya maskini, kumbe ana utajiri mwingi.
13:8 Mit 15:16Utajiri wa mtu waweza kukomboa maisha yake,
bali mtu maskini hasikii kitisho.
13:9 Ay 18:5; Mit 4:18-19Nuru ya mwenye haki hungʼaa sana,
bali taa ya mwovu itazimwa.