Mithali 1:8-19
Onyo Dhidi Ya Ushawishi Wa Marafiki Waovu
1:8 Mit 6:20; 22:17; Kum 21:18Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako,
wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
1:9 Mit 3:21-22; 4:1-9Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako,
na mkufu wa kuipamba shingo yako.
1:10 Mwa 39:7; Ay 24:15; Kum 13:8; Rum 16:18Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi,
usikubaliane nao.
1:11 Mit 12:6; Yer 5:26; Mik 7:2Kama wakisema, “Twende tufuatane;
tukamvizie mtu na kumwaga damu,
njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;
1:12 Ay 33:18; Mwa 38:25; Za 40:3tuwameze wakiwa hai kama kaburi,1:12 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.
wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni.
Tutapata aina zote za vitu vya thamani
na kujaza nyumba zetu kwa nyara.
1:14 Mit 1:19Njoo ushirikiane nasi,
vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”
1:15 Za 119:101; Mwa 49:6; Mit 4:14Mwanangu, usiandamane nao.
Usiweke mguu wako katika njia zao,
1:16 Mit 6:18; Isa 59:7kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi,
ni wepesi kumwaga damu.
Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu
wakati ndege wote wanakuona!
1:18 Za 71:10Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe;
hujivizia tu wenyewe!
1:19 Mit 11:19; 15:27; 2Fal 5:20-27Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila;
huuondoa uhai wa wale wenye mali.