Mithali 1:1-7
Utangulizi: Kusudi Na Kiini
1:1 1Fal 4:29-34Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:
Kwa kupata hekima na nidhamu;
kwa kufahamu maneno ya busara;
1:3 Mit 2:1; 2:1, 9kwa kujipatia nidhamu na busara,
kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;
1:4 Mit 8:5, 12; 2:10-11huwapa busara wajinga,
maarifa na akili kwa vijana;
1:5 Mit 9:9wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao,
wenye kupambanua na wapate mwongozo;
1:6 Za 78:2; Mt 13:10-17; Hes 12:8; Amu 14:12kwa kufahamu mithali na mifano,
misemo na vitendawili vya wenye hekima.
1:7 Kut 20:20; Ay 28:28Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa,
lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.