Ayubu 4:1-21
Elifazi Anazungumza: Ayubu Ametenda Dhambi
4:1 Mwa 36:11; Ay 15:1; 22:1Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:
4:2 Yer 4:19; 20:9; Ay 32:20“Kama mtu akithubutu kuzungumza nawe,
kutakukasirisha?
Lakini ni nani awezaye
kujizuia asiseme?
4:3 Sef 3:16; Hos 6:3; Ebr 12:12; Kum 32:2; Ay 29:23; 26:2; Za 71:9; Isa 13:7; 35:3Fikiri jinsi ambavyo umewafundisha watu wengi,
jinsi ambavyo umeitia nguvu
mikono iliyokuwa dhaifu.
4:4 Yer 31:8; Ay 16:5; 29:16, 25; Isa 1:17; 35:3; Ebr 12:12Maneno yako yamewategemeza wale waliojikwaa;
umeyatia nguvu magoti yaliyokuwa dhaifu.
4:5 Rut 1:13; Za 38:2; Ay 6:14; Mit 24:10; Lk 4:23Lakini sasa hii taabu imekujia wewe,
nawe unashuka moyo;
imekupiga wewe,
nawe unafadhaika.
4:6 Mwa 6:9; Za 71:5; Mit 3:26; Ay 1:1; 1Fal 18:19Je, kumcha Mungu kwako hakupaswi kuwa
ndiyo matumaini yako
na njia zako kutokuwa na lawama
ndilo taraja lako?
4:7 Za 41:12; 91:9-10; 37:25; 2Pet 2:9; Mit 12:21; Ay 5:11; 36:7; Mt 19:23“Fikiri sasa: Ni mtu yupi asiye na hatia ambaye aliwahi kuangamia?
Ni wapi wanyofu waliwahi kuangamizwa?
4:8 Amu 14:18; Gal 6:7-8; Hos 8:7; Za 7:14; Yos 1:9; Ay 5:3; 15:17; 5:6; 15:35; Mt 11:18Kwa jinsi ambavyo mimi nimechunguza,
wale walimao ubaya
na wale hupanda uovu,
huvuna hayo hayo hayo.
4:9 Kut 15:10; 2The 2:8; Law 26:38; Isa 25:7; Ay 41:21; 40:13Kwa pumzi ya Mungu huangamizwa;
kwa mshindo wa hasira zake huangamia.
4:10 Ay 38:15; 29:17; Za 22:13; 17:12; 22:21; Mt 28:15Simba anaweza kunguruma na kukoroma,
lakini bado meno ya simba mkubwa huvunjika.
4:11 Kum 28:41; Mit 30:14; Ay 5:4; Za 34:10; 58:6; Ay 27:14; 29:17Simba anaweza kuangamia kwa kukosa mawindo,
nao wana wa simba jike hutawanyika.
4:12 Ay 26:14; 33:14; 32:13; 12:23; Yer 9:23; Za 78:59“Neno lililetwa kwangu kwa siri,
masikio yangu yakasikia mnongʼono wake.
4:13 Ay 33:15Katikati ya ndoto za kutia wasiwasi wakati wa usiku,
hapo usingizi mzito uwapatapo wanadamu,
4:14 Dan 10:8; Hab 3:16; Ay 21:6; Za 48:6; 55:5; 119:120, 161; Yer 5:22; 2Kor 7:15hofu na kutetemeka kulinishika
na kufanya mifupa yangu yote itetemeke.
4:15 Za 104:4; Mt 14:26; Ebr 1:14; Dan 5:6; 7:15, 28; 10:8Kuna roho aliyepita mbele ya uso wangu,
nazo nywele za mwili wangu zikasimama.
4:16 1Fal 19:12Yule roho akasimama,
lakini sikuweza kutambua kilikuwa kitu gani.
Umbo fulani lilisimama mbele ya macho yangu,
kukawa na ukimya kisha nikasikia sauti:
4:17 Za 143:2; Mdo 17:24; Mal 2:10; Mit 20:9; Ay 9:2; 8:3; 10:3; 14:4; 15:14; 13:18; Mhu 7:20; Isa 51:13‘Je, binadamu aweza kuwa mwadilifu kuliko Mungu?
Je, mtu aweza kuwa safi kuliko Muumba wake?
4:18 Ay 25:5; 21:22; 5:4; 1Pet 2:4; Ebr 1:14Kama Mungu hawaamini watumishi wake,
kama yeye huwalaumu malaika zake kwa kukosea,
4:19 Isa 64:8; 2Kor 4:7; 2Pet 2:4; Mwa 2:7ni mara ngapi zaidi wale waishio katika nyumba
za udongo wa mfinyanzi,
ambazo misingi yake ipo mavumbini,
ambao wamepondwa kama nondo!
4:20 Za 89:47; 90:5-6; Yak 4:14; Ay 14:2, 20; 15:33; 20:7Kati ya mawio na machweo
huvunjwa vipande vipande;
bila yeyote kutambua,
huangamia milele.
4:21 Ay 8:22; Isa 38:12; Mit 5:23; Yn 8:24; Yer 9:3Je, kamba za hema yao hazikungʼolewa,
hivyo hufa bila hekima?’
Ayubu 5:1-27
Elifazi Anaendelea
5:1 Ay 15:15; Za 89:5-7; Hab 1:2“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu?
Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
5:2 Mit 12:16; Gal 5:26; Ay 21:15; 36:13Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu,
nao wivu humchinja mjinga.
5:3 Isa 40:24; Eze 17:6; Za 109:9-10; 37:35; 37:22; Mit 3:33; Ay 4:8; 24:18; Yer 12:2; Mit 6:15Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi,
lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
5:4 Ay 20:10; 4:11, 19; Amo 5:12; Za 109:12; Isa 9:17; 1Yn 2:1Watoto wake wako mbali na usalama,
hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5:5 Law 26:16; Mik 6:15; Amu 2:15; Ay 20:18; 31:8Wenye njaa huyala mavuno yake,
wakiyatoa hata katikati ya miiba,
nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
5:6 Ay 4:8Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo,
wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
5:7 Mwa 3:17; Mit 22:8; Ay 10:17; 15:35; Za 51:5; 58:3; 90:10Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika,
kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
5:8 Za 50:15; 27:14; 35:23; Ay 8:5; 11:13; 13:3, 15; 13:4; 40:1; Yer 12:1; 1Kor 4:1“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu,
ningeliweka shauri langu mbele zake.
5:9 Za 78:4; 11:2; Kum 29:9; Ay 9:4, 10; 11:7; 25:2; 26:14; Isa 40:28; Rum 11:23Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa,
miujiza isiyoweza kuhesabika.
5:10 Za 135:7; Yer 14:22; Mt 5:45; Law 26:4; Ay 36:28; 37:6, 13Yeye huipa nchi mvua,
huyapeleka maji kunyesha mashamba.
5:11 1Sam 2:7-8; Ay 4:7; Za 75:7; 113:7-8; Isa 61:2; Rum 12:5; Yak 4:10; Mt 23:12; 5:4Huwainua juu wanyonge,
nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
5:12 Isa 8:10; Yer 19:7; Neh 4:15; Isa 19:3; Za 33:10; 78:59; Ay 12:23Huipinga mipango ya wenye hila,
ili mikono yao isifikie ufanisi.
5:13 Za 36:3; Lk 20:23; Ay 37:24; Isa 29:14; 44:25; Yer 8:8; 18:18; 51:57; 1Kor 3:19; 2Kor 11:3Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao,
nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
5:14 Isa 8:22; Yn 12:35; Amo 8:9; Ay 15:22, 30; 18:6; Kum 28:29Giza huwapata wakati wa mchana;
wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
5:15 Kut 22:23; Ay 4:10; 8:6; 22:27; 33:26; 36:15; 35:10Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao;
huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
5:16 Za 63:11; Rum 3:19; Ay 20:19; 31:16; Mit 17:5; 22:22; Isa 11:4; 41:17; 61:1Kwa hiyo maskini analo tarajio,
nao udhalimu hufumba kinywa chake.
5:17 Sef 3:7; Yak 1:12; Mit 3:11; Yer 31:18; Ebr 12:5-11; Za 94:12; Yak 1:12; Kum 8:5; Ay 33:19; 36:10; Ebr 12:5-11“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi;
kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.5:17 Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania Shaddai (hapa na kila mahali katika kitabu hiki cha Ayubu).
5:18 Isa 30:26; Kum 32:39; 1Sam 2:6; Isa 57:15; 61:1; Hos 6:1Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga;
huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
5:19 Mit 3:25-26; Kut 12:46; Za 34:19; 91:10; Mit 1:33; 2The 3:3; 2Pet 2:9Kutoka majanga sita atakuokoa;
naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
5:20 Ay 5:22; Za 33:19; 22:20; 91:7; 140:7; 144:10; Yer 39:18Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo,
naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
5:21 Za 31:15; 12:2-4; 31:20; 23:4; 27:1; 91:5; Ay 5:15Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi,
wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
5:22 Hos 2:18; Mk 1:14; Ay 8:21; 39:7, 18, 22; 41:29; 5:20; Law 25:18; Za 91:13Utayacheka maangamizo na njaa,
wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa
wanyama wakali wa mwituni.
5:23 2Fal 3:19-25; Mt 13:8; Isa 65:25; Eze 34:25; Za 91:12; Isa 28:15; Hos 2:18; Za 91:12Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba,
nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
5:24 Ay 12:6; 21:9; 8:6; 22:23Utajua ya kwamba hema lako li salama;
utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
5:25 Kum 28:4; Za 72:16; Isa 48:19; 44:3-4Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi,
nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
5:26 Kum 11:21; Mhu 8:13; Mwa 15:15; Mit 3:21-26Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu,
kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
5:27 Ay 32:10; 8:5; 11:13; 22:27“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli.
Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Ayubu 6:1-30
Hotuba Ya Pili Ya Ayubu
Ayubu Anajibu: Malalamiko Yangu Ni Ya Haki
Kisha Ayubu akajibu:
6:2 Ay 31:6; Mit 11:1; Dan 5:27“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa,
nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
6:3 Mit 27:3; Ay 21:4; 16:6; 2Fal 4:29; Ay 6:11, 26; 7:11; 16:6Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote,
kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
6:4 Kum 32:23; Za 38:2; 88:15-18; Mao 3:12; Ay 16:12-14; Za 7:13; 18:14; 21:12; Mwa 17:1; Ay 7:20; 6:12, 13; Kum 32:32Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu,
roho yangu inakunywa sumu yake;
vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
6:5 Mwa 16:12; Ay 30:7; 30:24Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani,
au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6:6 Ay 33:20; Za 107:18Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi,
au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
6:7 Za 31:22Ninakataa kuvigusa;
vyakula vya aina hii hunichukiza.
“Laiti ningepata haja yangu,
kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
6:9 1Fal 19:4; Za 31:22kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda,
kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
6:10 Mk 8:38; Za 119:102; Law 19:2; 2Fal 19:22; Ay 2:11; 15:11; Za 94:19; 38:17; Yer 4:19; 45:3; Ay 22:22; 23:12Ndipo bado ningekuwa na hii faraja,
furaha yangu katika maumivu makali:
kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
6:11 Ay 6:3“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini?
Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
6:12 Ay 26:2Je, mimi nina nguvu za jiwe?
Je, mwili wangu ni shaba?
6:13 Ay 26:2Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe,
wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
6:14 Ay 4:5; 15:4; 1Sam 20:42; Za 38:11; 69:20; 1Yn 3:17; Mwa 17:1“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake,
hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
6:15 Ay 13:4; 16:2; 21:34; Za 22:1; 38:11; Yer 15:18Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa,
ni kama vijito vya msimu,
ni kama vijito ambavyo hufurika
6:16 Za 147:18wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo,
ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
6:17 Ay 24:19lakini hukauka majira ya ukame,
na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
Misafara hugeuka kutoka njia zake;
hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
6:19 Mwa 25:15; Isa 21:14; Mwa 10:7, 28Misafara ya Tema inatafuta maji,
wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri
hutazama kwa matarajio.
6:20 Yer 14:3; Yoe 1:11Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini;
wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
6:21 Za 38:11Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote;
mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
6:22 Mdo 20:33; Hes 35:31; Ay 33:24; Za 49:7; Yer 15:10Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu,
au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
6:23 2Fal 19:19au niokoeni mikononi mwa adui,
au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
6:24 Mit 17:27; Mhu 5:2; Ay 2:10; 33:33; Za 39:1; 141:3; 39:1; Mit 10:19“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya;
nionyesheni nilikokosea.
6:25 Mhu 12:11; Isa 22:23Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli!
Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
6:26 Mwa 41:6; Yer 5:13; Ay 6:3; 8:2; 15:3; 16:3Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema,
na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
6:27 Nah 3:10; 2Pet 2:3; Eze 24:6; Yoe 3:3; Oba 1:11; Kut 22:22, 24; Isa 10:2; Ay 31:17Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima,
na kubadilishana rafiki yenu na mali.
6:28 Ay 9:15; 24:25; 27:4; 34:10; 33:1, 3; 34:6; 36:3, 4“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi.
Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
6:29 Za 66:10; Zek 13:9; Ay 19:6; 27:2; 40:8; Isa 40:27; Ay 2:3; 9:21; 10:7Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu;
angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.6:29 Au: haki yangu bado inasimama.
6:30 Ay 27:4; 33:8-12; Yak 3:13; Ay 12:11Je, pana uovu wowote midomoni mwangu?
Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?
Ayubu 7:1-21
Ayubu: Mateso Yangu Hayana Mwisho
7:1 Ay 14:6, 13-14; Isa 40:2; Law 25:50; Za 39:4; Mhu 3:1, 2; Ay 5:7“Je, mwanadamu hana kazi ngumu duniani?
Siku zake si kama zile za mtu aliyeajiriwa?
7:2 Law 19:13; Ay 14:1; Mhu 2:23; Ay 14:6Kama mtumwa anavyovionea shauku vivuli vya jioni,
au mtu aliyeajiriwa anavyoungojea mshahara wake,
7:3 Mhu 4:1; Mao 1:2, 16; Za 39:5; Mhu 1:14; Isa 16:9; Yer 9:1ndivyo nilivyogawiwa miezi ya ubatili,
nami nimeandikiwa huzuni usiku hata usiku.
7:4 Kum 28:67; Ay 7:13-14Wakati nilalapo ninawaza, ‘Itachukua muda gani kabla sijaamka?’
Usiku huwa mrefu, nami najigeuzageuza hadi mapambazuko.
7:5 Ay 17:14; Za 38:5-7; Isa 1:6Mwili wangu umevikwa mabuu na uchafu,
ngozi yangu imetumbuka na kutunga usaha.
Ayubu Anamlilia Mungu
7:6 Za 39:5; 52:9; Isa 38:15; Ay 9:25; 13:15“Siku zangu zinapita upesi kuliko mtande wa kufuma,
nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini.
7:7 Mhu 7:15; Yak 4:14; Ay 9:25; Za 78:39Kumbuka, Ee Mungu, maisha yangu ni kama pumzi;
macho yangu kamwe hayataona tena raha.
7:8 Isa 41:12; Mdo 20:25; Ay 20:9Lile jicho linaloniona sasa halitaniona tena;
utanitafuta, wala sitakuwepo.
7:9 Ay 30:15; 38:17; 2Sam 12:23; Za 39:13Kama vile wingu liondokavyo na kutoweka,
vivyo hivyo yeye ashukaye kaburini7:9 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. harudi tena.
7:10 Ay 18:21; 21:18; 27:21; Za 58:9; Yer 18:17; 19:8; Za 37:10; 104:35Kamwe harudi tena nyumbani mwake;
wala mahali pake hapatamjua tena.
7:11 Za 39:1, 9“Kwa hiyo sitanyamaza;
nitanena kutokana na maumivu makuu ya roho yangu,
nitalalama kwa uchungu wa nafsi yangu.
7:12 Mwa 1:21; Eze 32:2-3; Ay 38:8-11; Isa 1:14Je, mimi ni bahari, au mnyama mkubwa mno akaaye vilindini,
hata uniweke chini ya ulinzi?
7:13 Ay 7:11Ninapofikiri kwamba kitanda changu kitanifariji,
nacho kiti changu cha fahari kitapunguza malalamiko yangu,
7:14 Ay 9:34; 3:26; Mwa 41:8ndipo wanitisha kwa ndoto
na kunitia hofu kwa maono,
7:15 1Fal 19:4; Yn 4:3; Ay 6:9; Ufu 9:6hivyo ninachagua kujinyonga na kufa,
kuliko huu mwili wangu.
7:16 Mwa 27:46; Za 62:9; 1Fal 19:4; Ay 10:1; Mhu 6:11Ninayachukia maisha yangu; nisingetamani kuendelea kuishi.
Niache; siku zangu ni ubatili.
7:17 Za 144:3; 8:4; Ebr 2:6; Ay 4:19“Mwanadamu ni kitu gani hata umjali kiasi hiki,
kwamba unamtia sana maanani,
7:18 Ay 23:10; 14:3; Za 139:23; 17:3; 26:2; 66:10; 73:14kwamba unamwangalia kila asubuhi
na kumjaribu kila wakati?
7:19 Ay 7:16; 9:18; 13:26; 14:6; 27:2; Za 139:7Je, hutaacha kamwe kunitazama,
au kuniacha japo kwa kitambo kidogo tu?
7:20 Yer 7:19; Ay 6:4; 16:12; 35:6; Za 36:6Ikiwa nimetenda dhambi, nimekufanyia nini,
Ewe mlinzi wa wanadamu?
Kwa nini umeniweka niwe shabaha yako?
Je, nimekuwa mzigo kwako?
7:21 Yer 31:34; Mwa 3:19; Ay 9:28; Ebr 1:3; Za 119:120; 7:5; 22:15; 90:3; 104:29; Isa 43:25Kwa nini husamehi makosa yangu
na kuachilia dhambi zangu?
Kwa kuwa hivi karibuni nitalala mavumbini;
nawe utanitafuta, wala sitakuwepo.”