Ayubu 22:1-30, Ayubu 23:1-17, Ayubu 24:1-25 NEN

Ayubu 22:1-30

Elifazi Anasema: Uovu Wa Ayubu Ni Mkubwa

22:1 Ay 4:1Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:

22:2 Lk 17:10; Za 16:2“Je, mwanadamu aweza kuwa wa faida kwa Mungu?

Je, hata mtu mwenye hekima aweza kumfaidi?

22:3 Isa 1:11; Hag 1:8; Za 143:2; Ay 35:7; Za 9:12Je, Mwenyezi angefurahia nini

kama ungekuwa mwadilifu?

Au je, yeye angepata faida gani

kama njia zako zingekuwa kamilifu?

22:4 Isa 3:14; Eze 20:35“Je, ni kwa ajili ya utaua wako ndiyo maana anakukemea

na kuleta mashtaka dhidi yako?

22:5 Ezr 9:13; Ay 11:6; Ezr 9:13; Ay 15:5; 15:13; 20:29; 29:17Je, uovu wako si mkuu?

Dhambi zako si hazina mwisho?

22:6 Kum 24:6, 17; Eze 18:12-16Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu;

umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi.

22:7 Ay 31:16-17; Eze 18:7; Mt 25:42Hukumpa maji aliyechoka,

nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,

22:8 Ay 15:19; Isa 3:3; 5:13; 9:15; Ay 12:19ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi:

mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake.

22:9 Isa 10:2; Lk 1:53Umewafukuza wajane mikono mitupu

na kuzivunja nguvu za yatima.

22:10 Ay 18:9; 10:3; 15:21Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote,

hatari ya ghafula inakutia hofu,

22:11 Ay 5:14; Isa 58:10-11; Mao 3:54ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona,

tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika.

22:12 Ay 11:8; 16:19“Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu?

Juu kuliko nyota zilizo juu sana!

22:13 Eze 9:9; Efe 6:2; Sef 1:12; Za 139:11Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’

Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo?

22:14 Ay 26:9; Za 97:2; 105:39; 105:13; 2Fal 21:16; Ay 37:18; Za 18:11; Mit 8:27; Yer 23:23-24Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi

atembeapo juu ya anga la dunia.

22:15 Mwa 6:11-13Je, utaifuata njia ya zamani,

ambayo watu waovu waliikanyaga?

22:16 Ay 15:32; Mwa 7:23; Mt 7:26-27Waliondolewa kabla ya wakati wao,

misingi yao ikachukuliwa na mafuriko.

22:17 Ay 21:15Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi!

Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’

22:18 Ay 12:6; 21:16Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri,

hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu.

22:19 Za 64:10; 97:12; Ay 21:3“Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi,

nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema,

22:20 Ay 15:30‘Hakika adui zetu wameangamizwa,

nao moto umeteketeza mali zao.’

22:21 Mit 3:10; 1Pet 5:6; Isa 27:5“Mjue sana Mungu ili uwe na amani,

ndipo mema yatakapokujia.

22:22 Kum 8:3; Ay 6:10; Eze 3:10; Mit 2:6; Za 37:31Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake,

na maneno yake uyaweke moyoni mwako.

22:23 Isa 19:22; 44:22; Eze 18:32; Mdo 20:32; Ay 11:14Kama ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya:

Kama ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako,

22:24 Isa 2:20; 30:22kama dhahabu yako ukiihesabu kama mavumbi,

dhahabu yako ya Ofiri kama miamba ya mabondeni,

22:25 2Fal 18:7; Mt 6:20-21ndipo Mwenyezi atakuwa dhahabu yako,

naye atakuwa fedha yako iliyo bora.

22:26 Za 2:8; Isa 61:10Hakika ndipo utakapojifurahisha kwa Mwenyezi,

nawe utamwinulia Mungu uso wako.

22:27 Ay 5:27; Isa 58:9Utamwomba yeye, naye atakusikia,

nawe utazitimiza nadhiri zako.

22:28 Za 103:11; 145:19; Ay 33:28; Mit 4:18; Za 97:11Utakusudia jambo nalo litatendeka,

nao mwanga utaangazia njia zako.

22:29 Za 18:27; 1Pet 5:5Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’

ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.

22:30 2Sam 22:21; Ay 42:7-8Atamwokoa hata yule ambaye ana hatia,

ataokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.”

Read More of Ayubu 22

Ayubu 23:1-17

Hotuba Ya Nane Ya Ayubu

Ayubu Anajibu: Kulalamika Kwangu Ni Uchungu

Ndipo Ayubu akajibu:

23:2 Ay 6:3; 7:11; 1Sam 1:10“Hata leo malalamiko yangu ni chungu;

mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.

23:3 Kum 4:29Laiti ningefahamu mahali pa kumwona;

laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!

23:4 Ay 13:18; 9:15Ningeliweka shauri langu mbele zake,

na kukijaza kinywa changu na hoja.

Ningejua kwamba angenijibu nini,

na kuelewa lile ambalo angelisema.

23:6 Ay 9:4, 19; Isa 27:4Je, angenipinga kwa nguvu nyingi?

La, asingenigandamiza.

23:7 Mwa 3:8; Ay 9:3Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake,

nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.

“Lakini nikienda mashariki, hayupo;

nikienda magharibi, simpati.

23:9 Ay 9:11Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni;

akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.

23:10 Za 66:10; 139:1-3; 12:6; 1Pet 1:7; Yak 1:12Lakini anaijua njia niiendeayo;

akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.

23:11 Za 17:5; Ay 31:7; Yer 11:20; Za 44:18; 125:5Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu;

nimeishika njia yake bila kukengeuka.

23:12 Ay 6:10; 15:11; Yn 4:32, 34; Mt 4:4Sijaziacha amri zilizotoka midomoni mwake;

nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku.

23:13 Za 115:3; Isa 55:11; Mhu 3:14; Rum 9:19“Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga?

Yeye hufanya lolote atakalo.

23:14 1The 3:3; 1Pet 4:12Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu,

na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.

23:15 Mwa 45:3; Yos 24:14; Mhu 3:14; 12:13; 2Kor 5:11Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake;

nifikiriapo haya yote ninamwogopa.

23:16 Za 22:14; Yer 51:46; Ay 27:223:16 Kum 20:3; Ay 27:2; Kut 3:6; Ufu 6:16Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia;

yeye Mwenyezi amenitia hofu.

23:17 Ay 3:6; 6:9; 19:8Hata hivyo sijanyamazishwa na giza,

wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.

Read More of Ayubu 23

Ayubu 24:1-25

Ayubu Analalamikia Jeuri Duniani

24:1 Yer 46:10; 2Pet 3:7; Ay 15:20; Mdo 1:7“Kwa nini Mwenyezi asiweke nyakati kwa ajili ya hukumu?

Kwa nini wale wamjuao wazitafute siku kama hizo bila mafanikio?

24:2 Kum 19:14; 27:17; Mit 23:10Watu husogeza mawe ya mpaka;

huchunga makundi ya wanyama waliyonyangʼanya kwa nguvu.

24:3 Kum 24:6-10; 12:17; Ay 6:27Huwanyangʼanya yatima punda wao,

na kumchukua rehani fahali wa mjane.

24:4 Mit 28:28; Ay 20:19; Isa 11:4; Za 12:5Humsukuma mhitaji kutoka njia,

na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.

24:5 Mwa 16:12; Za 104:23; Ay 30:3Kama punda-mwitu jangwani,

maskini huzunguka katika kazi zao za kutafuta chakula;

mahali palipo jangwa

huwapa chakula cha watoto wao.

24:6 Ay 6:5; Rut 2:22; 1Fal 21:19Hukusanya chakula mashambani na kuokota masazo

katika mashamba ya mizabibu ya waovu.

24:7 Kut 22:26-27; Kum 24:12; Ay 22:6Kwa kukosa nguo, usiku kucha hukaa uchi;

hawana chochote cha kujifunika baridi.

24:8 Dan 4:25, 33; Mao 4:5Hutota kwa mvua za mlimani,

nao huikumbatia miamba kwa ajili ya kukosa pa kujisitiri.

24:9 Kum 24:17Mtoto yatima hupokonywa matitini;

mtoto wachanga wa maskini hunyakuliwa kwa ajili ya deni.

24:10 Kum 24:12-13; Law 19:9Kwa kukosa nguo, hutembea uchi;

hubeba miganda ya ngano, lakini huwa na njaa.

24:11 Isa 5:2; 16:10; Hag 2:16; Mik 6:15Hukamua zeituni katika mawe ya kusagia;

hukanyaga mashinikizo, lakini wanaona kiu.

24:12 Isa 30:19; Ay 9:23; Ufu 6:10; Mhu 8:11Kilio cha huzuni cha wanaokufa kinapaa kutoka mjini,

nazo nafsi za waliojeruhiwa zinalilia msaada.

Lakini Mungu hamlaumu mtu yeyote

kwa kutenda mabaya.

24:13 Ay 38:15; 1The 5:4-5; Za 18:28; Efe 5:8-14“Wako wale wanaoiasi nuru,

wasiofahamu njia zake

wala hawakai katika mapito yake.

24:14 Isa 3:15; Mik 3:3; Ay 20:19; Za 37:32; 10:9Wakati mwanga wa mchana unapotoweka, muuaji huinuka

naye huwaua maskini na mhitaji;

wakati wa usiku hunyemelea kama mwizi.

24:15 Mit 7:8-9; Za 10:11Jicho la mzinzi hungojea wakati wa giza,

naye hufikiri, ‘Hakuna jicho litakaloniona,’

naye huuficha uso wake.

24:16 Kut 22:2; Mt 6:19; Yn 3:20Katika giza, huvunja majumba,

lakini wakati wa mchana hujifungia ndani;

hawataki kufanya lolote nuruni.

24:17 Ay 18:11; 15:22; 18:5Kwa wote hawa, giza nene ndiyo asubuhi yao;

hujifanya rafiki na vitisho vya gizani.

24:18 Ay 9:26; 22:16; Yud 23; Isa 57:20“Lakini wao ni povu juu ya maji;

sehemu yao juu ya nchi imelaaniwa,

hivyo hakuna hata mmoja

aendaye kwenye shamba la mizabibu.

24:19 Ay 6:17; 21:13Kama vile joto na hari vinyakuavyo theluji iliyoyeyuka,

ndivyo kuzimu kuwanyakuavyo waliotenda dhambi.

24:20 Ay 18:17; Mit 10:7; Dan 4:14; Za 31:12Tumbo lililowazaa huwasahau,

nao huwa karamu ya mabuu;

watu waovu hawakumbukwi tena,

lakini huvunjika kama mti.

24:21 Ay 22:9Huwafanya mawindo wanawake tasa na wasio na watoto,

nao hawaonyeshi huruma kwa wajane.

24:22 Kum 28:66; Mt 6:27Lakini Mungu huwakokota wenye nguvu kwa uwezo wake;

ingawa wamestawi, hawana hakika ya maisha.

24:23 Ay 9:24; Amo 6:1; 2Nya 16:9; Ay 10:4Aweza akawaacha wakapumzika wakijihisi salama,

lakini macho yake yanaona njia zao.

24:24 2Fal 19:35; Za 37:35-36; 83:13; Isa 17:5Kwa kitambo kidogo hutukuka, hatimaye hutoweka;

hushushwa na kukusanywa kama wengine wote,

hukatwa kama masuke ya nafaka.

24:25 Ay 16:17; 27:4“Kama hili sivyo, ni nani awezaye kunithibitisha kuwa mwongo,

na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?”

Read More of Ayubu 24