2 Wakorintho 5:1-10 NEN

2 Wakorintho 5:1-10

Makao Yetu Ya Mbinguni

5:1 1Kor 15:47; Isa 38:12; 1Pet 1:13-14Kwa maana twajua kama hema yetu ya dunia tunayoishi ikiharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba iliyo ya milele kule mbinguni, isiyojengwa kwa mikono ya wanadamu. Katika hema hii twalia kwa uchungu, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni, kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena kuwa uchi. 5:4 1Kor 15:33, 54; Rum 8:23; 2Kor 5:2; 1Kor 15:51Kwa kuwa tukiwa bado katika hema hii twalia kwa uchungu na kulemewa, kwa sababu hatutaki kuvuliwa bali kuvikwa makao yetu ya mbinguni ili kwamba kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima. 5:5 Rum 8:23; 2Kor 1:22; Efe 1:13-14Basi Mungu ndiye alitufanya kwa ajili ya jambo lilo hilo naye ametupa Roho Mtakatifu kuwa amana, akituhakikishia ahadi ya kile kijacho.

5:6 Ebr 11:13Kwa hiyo siku zote tunalo tumaini, hata ingawa tunajua kwamba wakati tukiwa katika mwili huu, tuko mbali na Bwana, 5:7 1Kor 13:12; 2Kor 4:18kwa maana twaenenda kwa imani wala si kwa kuona. 5:8 Yn 12:26; Flp 1:23Naam, tunalo tumaini na ingekuwa bora zaidi kuuacha mwili huu na kwenda kukaa na Bwana. 5:9 Rum 14:18; Efe 5:10; Kol 1:10; 1The 4:1Kwa hiyo, kama tuko katika mwili huu au tuko mbali nao, lengo letu ni kumpendeza Bwana. 5:10 Mt 16:27; Mdo 10:42; Rum 2:16; 14:10; Efe 6:8Kwa kuwa sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apate kulipwa kwa ajili ya yale ambayo yametendwa katika mwili wake, yakiwa mema au mabaya.

Read More of 2 Wakorintho 5