2พงศ์กษัตริย์ 12 – TNCV & NEN

Thai New Contemporary Bible

2พงศ์กษัตริย์ 12:1-21

โยอาชทรงซ่อมแซมพระวิหาร

(2พศด.24:1-14; 24:23-27)

1โยอาชขึ้นเป็นกษัตริย์ตรงกับปีที่เจ็ดของรัชกาลกษัตริย์เยฮู พระองค์ทรงครองราชย์ในกรุงเยรูซาเล็มอยู่สี่สิบปี ราชมารดาคือศิบียาห์จากเบเออร์เชบา 2โยอาชทรงทำสิ่งที่ถูกต้องในสายพระเนตรขององค์พระผู้เป็นเจ้าตลอดหลายปีที่มีปุโรหิตเยโฮยาดาคอยถวายคำปรึกษา 3แต่สถานบูชาบนที่สูงทั้งหลายยังไม่ถูกทำลาย ประชากรยังคงไปถวายเครื่องบูชาและเผาเครื่องหอมที่นั่น

4โยอาชตรัสกับเหล่าปุโรหิตว่า “จงรวบรวมเงินที่ผู้คนนำมาถวายที่พระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้า คือเงินที่เรียกเก็บรายบุคคลจากการทำสำมะโนประชากร เงินถวายตามคำปฏิญาณ และเงินถวายตามความสมัครใจให้แก่พระวิหาร 5ให้ปุโรหิตทุกคนรับเงินจากผู้ดูแลรักษาเงินคนใดคนหนึ่ง แล้วใช้เงินนั้นซ่อมแซมพระวิหารส่วนที่ชำรุด”

6แต่จนถึงปีที่ยี่สิบสามแห่งรัชกาลโยอาช บรรดาปุโรหิตก็ยังไม่ได้ซ่อมแซมพระวิหาร 7โยอาชจึงเรียกเยโฮยาดาและปุโรหิตอื่นๆ มาเข้าเฝ้าและตรัสถามว่า “เหตุใดท่านทั้งหลายจึงยังไม่ได้ซ่อมแซมพระวิหารส่วนที่ชำรุด? ต่อแต่นี้ไปอย่ารับเงินจากผู้ดูแลรักษาเงินอีกเลย แต่จงมอบไว้สำหรับการบูรณะซ่อมแซมพระวิหาร” 8บรรดาปุโรหิตจึงตกลงกันว่าจะไม่รับเงินจากประชาชนอีกต่อไป และจะไม่ดำเนินการซ่อมแซมพระวิหารเอง

9ปุโรหิตเยโฮยาดาเจาะรูไว้ที่ฝาหีบใหญ่ และนำหีบมาตั้งไว้ที่ข้างขวาแท่นบูชา ตรงทางเข้าพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้า ปุโรหิตที่เฝ้าประตูจะนำเงินถวายทั้งหมดที่คนนำมาถวายที่พระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้าหย่อนลงในหีบ 10เมื่อใดก็ตามที่เห็นว่าในหีบมีเงินมากแล้ว ราชเลขาและมหาปุโรหิตจะนับเงินที่นำมาถวายในพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้าและเก็บใส่ถุง 11หลังจากจัดสรรเงินที่นับแล้วก็นำไปมอบให้ผู้ควบคุมการก่อสร้างพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้า เพื่อจ่ายให้ช่างไม้ ช่างก่อสร้าง 12ช่างก่อ ช่างสกัดหิน เพื่อซื้อไม้ซุงและหินสกัด และเพื่อค่าใช้จ่ายอื่นๆ สำหรับการซ่อมแซมพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้า

13เงินถวายนี้ไม่ได้ใช้สำหรับทำอ่างเงิน กรรไกรตัดไส้ตะเกียง อ่างประพรม แตร หรือภาชนะเงินหรือทองในพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้า 14แต่จ่ายให้กับคนงานเพื่อการซ่อมแซมพระวิหารเท่านั้น 15ไม่จำเป็นต้องมีรายงานบัญชีจากผู้ควบคุมการก่อสร้างเหล่านี้ เพราะพวกเขาทำงานด้วยความซื่อสัตย์สุจริตอย่างแท้จริง 16ส่วนเงินที่นำมาถวายเป็นเครื่องบูชาลบมลทินและเครื่องบูชาไถ่บาปนั้นให้เป็นของปุโรหิต ไม่ต้องนำมาในพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้า

17ครั้งนั้นกษัตริย์ฮาซาเอลแห่งอารัมมาโจมตีเมืองกัทและยึดเมืองไว้ได้ แล้วเคลื่อนทัพมุ่งหน้าจะมาโจมตีกรุงเยรูซาเล็ม 18แต่กษัตริย์โยอาชแห่งยูดาห์นำสิ่งของศักดิ์สิทธิ์ซึ่งบรรพบุรุษ คือเยโฮชาฟัท เยโฮรัม และกษัตริย์อาหัสยาห์แห่งยูดาห์ได้ถวาย พร้อมทั้งสิ่งของที่โยอาชเองได้ถวาย รวมถึงทองคำทั้งหมดในคลังพระวิหารขององค์พระผู้เป็นเจ้าและของพระราชวัง ส่งไปให้กษัตริย์ฮาซาเอลแห่งอารัม ฮาซาเอลจึงถอนทัพจากเยรูซาเล็ม

19เหตุการณ์อื่นๆ ในรัชกาลของโยอาช และพระราชกิจทั้งปวงมีบันทึกไว้ในจดหมายเหตุกษัตริย์แห่งยูดาห์ไม่ใช่หรือ? 20ข้าราชการของโยอาชสมคบกันปลงพระชนม์พระองค์ที่เบธมิลโลบนเส้นทางจะไปสิลลา 21ผู้ปลงพระชนม์คือโยซาบาดบุตรชิเมอัท และเยโฮซาบาดบุตรโชเมอร์ โยอาชสิ้นพระชนม์และถูกฝังไว้ร่วมกับบรรพบุรุษในเมืองดาวิด แล้วอามาซิยาห์โอรสของพระองค์ก็ขึ้นครองราชย์แทน

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 12:1-21

Yoashi Anakarabati Hekalu

112:1 2Fal 11:2Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba. 212:2 Kum 12:25; 2Sam 8:15Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza. 312:3 2Fal 18:4Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.

412:4 Hes 18:19; Kut 30:12Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni. 5Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”

6Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu. 7Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.” 8Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.

912:9 Yer 35:4; Mk 12:41Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana. 1012:10 2Sam 8:17Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko. 11Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi, 1212:12 2Fal 22:5-6waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.

1312:13 1Fal 7:51Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana; 14zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu. 1512:15 2Fal 22:7; 1Kor 4:2Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote. 1612:16 Law 5:14-19Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.

1712:17 2Fal 8:12Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu. 1812:18 1Fal 15:18; 2Fal 15:20Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.

19Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 2012:20 2Fal 14:5; Amu 9:6Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila. 21Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.