پيدايش 27 – PCB & NEN

Persian Contemporary Bible

پيدايش 27:1‏-46

يعقوب بركت را از اسحاق می‌گيرد

1‏-2اسحاق پير شده و چشمانش تار گشته بود. روزی او پسر بزرگ خود عيسو را خواند و به وی گفت: «پسرم، من ديگر پير شده‌ام و پايان زندگيم فرا رسيده است. 3پس تير و كمان خود را بردار و به صحرا برو و شكاری كن 4و از آن، خوراكی مطابق ميلم آماده ساز تا بخورم و پيش از مرگم تو را بركت دهم.»

5اما ربكا سخنان آنها را شنيد. وقتی عيسو برای شكار به صحرا رفت، 6ربكا، يعقوب را نزد خود خوانده، گفت: «شنيدم كه پدرت به عيسو چنين می‌گفت: 7”مقداری گوشت شكار برايم بياور و از آن غذايی برايم بپز تا بخورم. من هم قبل از مرگم در حضور خداوند تو را بركت خواهم داد.“ 8حال ای پسرم هر چه به تو می‌گويم انجام بده. 9نزد گله برو و دو بزغالهٔ خوب جدا كن و نزد من بياور تا من از گوشت آنها غذايی را كه پدرت دوست می‌دارد برايش تهيه كنم. 10بعد تو آن را نزد پدرت ببر تا بخورد و قبل از مرگش تو را بركت دهد.»

11يعقوب جواب داد: «عيسو مردی است پُر مو، ولی بدن من مو ندارد. 12اگر پدرم به من دست بزند و بفهمد كه من عيسو نيستم، چه؟ آنگاه او پی خواهد برد كه من خواسته‌ام او را فريب بدهم و به جای بركت، مرا لعنت می‌كند!»

13ربكا گفت: «پسرم، لعنت او بر من باشد. تو فقط آنچه را كه من به تو می‌گويم انجام بده. برو و بزغاله‌ها را بياور.»

14يعقوب دستور مادرش را اطاعت كرد و بزغاله‌ها را آورد و ربكا خوراكی را كه اسحاق دوست می‌داشت، تهيه كرد. 15آنگاه بهترين لباس عيسو را كه در خانه بود به يعقوب داد تا بر تن كند. 16سپس پوست بزغاله را بر دستها و گردن او بست، 17و غذای خوش طعمی را كه درست كرده بود همراه با نانی كه پخته بود به دست يعقوب داد. 18يعقوب آن غذا را نزد پدرش برد و گفت: «پدرم!»

اسحاق جواب داد: «بلی، كيستی؟»

19يعقوب گفت: «من عيسو پسر بزرگ تو هستم. همانطور كه گفتی به شكار رفتم و غذايی را كه دوست می‌داری برايت پختم. بنشين، آن را بخور و مرا بركت بده.»

20اسحاق پرسيد: «پسرم، چطور توانستی به اين زودی شكاری پيدا كنی؟»

يعقوب جواب داد: «خداوند، خدای تو آن را سر راه من قرار داد.»

21اسحاق گفت: «نزديک بيا تا تو را لمس كنم و مطمئن شوم كه واقعاً عيسو هستی.»

22يعقوب نزد پدرش رفت و پدرش بر دستها و گردن او دست كشيد و گفت: «صدا، صدای يعقوب است، ولی دستها، دستهای عيسو!» 23اسحاق او را نشناخت، چون دستهايش مثل دستهای عيسو پرمو بود. پس يعقوب را بركت داده، 24پرسيد: «آيا تو واقعاً عيسو هستی؟»

يعقوب جواب داد: «بلی پدر.»

25اسحاق گفت: «پس غذا را نزد من بياور تا بخورم و بعد تو را بركت دهم.» يعقوب غذا را پيش او گذاشت و اسحاق آن را خورد و شرابی را هم كه يعقوب برايش آورده بود، نوشيد. 26بعد گفت: «پسرم، نزديک بيا و مرا ببوس.» 27يعقوب جلو رفت و صورتش را بوسيد. وقتی اسحاق لباسهای او را بوييد به او بركت داده، گفت: «بوی پسرم چون رايحهٔ خوشبوی صحرايی است كه خداوند آن را بركت داده است. 28خدا باران بر زمينت بباراند تا محصولت فراوان باشد و غله و شرابت افزوده گردد. 29قومهای بسياری تو را بندگی كنند، بر برادرانت سَروَری كنی و همهٔ خويشانت تو را تعظيم نمايند. لعنت بر كسانی كه تو را لعنت كنند و بركت بر آنانی كه تو را بركت دهند.»

30پس از اين كه اسحاق يعقوب را بركت داد، يعقوب از اتاق خارج شد. به محض خروج او، عيسو از شكار بازگشت. 31او نيز غذايی را كه پدرش دوست می‌داشت، تهيه كرد و برايش آورد و گفت: «اينک غذايی را كه دوست داری با گوشتِ شكار برايت پخته و آورده‌ام. برخيز؛ آن را بخور و مرا بركت بده.»

32اسحاق گفت: «تو كيستی؟»

عيسو پاسخ داد: «من پسر ارشد تو عيسو هستم.»

33اسحاق در حالی كه از شدت ناراحتی می‌لرزيد گفت: «پس شخصی كه قبل از تو برای من غذا آورد و من آن را خورده، او را بركت دادم چه كسی بود؟ هر كه بود بركت را از آنِ خود كرد.»

34عيسو وقتی سخنان پدرش را شنيد، فريادی تلخ و بلند برآورد و گفت: «پدر، مرا بركت بده! تمنّا می‌كنم مرا نيز بركت بده!»

35اسحاق جواب داد: «برادرت به اينجا آمده، مرا فريب داد و بركت تو را گرفت.»

36عيسو گفت: «بی‌دليل نيست كه او را يعقوب27‏:36 يعقوب يعنی «حيله‌گر».‏ ناميده‌اند، زيرا دو بار مرا فريب داده است. اول حق نخست‌زادگی مرا گرفت و حالا هم بركت مرا. ای پدر، آيا حتی يک بركت هم برای من نگه نداشتی؟»

37اسحاق پاسخ داد: «من او را سَروَر تو قرار دادم و همه خويشانش را غلامان وی گردانيدم. محصول غله و شراب را به او دادم. ديگر چيزی باقی نمانده كه به تو بدهم.»

38عيسو گفت: «آيا فقط همين بركت را داشتی؟ ای پدر، مرا هم بركت بده!» و زارزار گريست.

39اسحاق گفت: «باران بر زمينت نخواهد باريد و محصول زياد نخواهی داشت. 40به شمشير خود خواهی زيست و برادر خود را بندگی خواهی كرد، ولی سرانجام خود را از قيد او رها ساخته، آزاد خواهی شد.»

يعقوب به نزد لابان فرار می‌كند

41عيسو از يعقوب كينه به دل گرفت، زيرا پدرش او را بركت داده بود. او با خود گفت: «پدرم بزودی خواهد مُرد؛ آنگاه يعقوب را خواهم كُشت.» 42اما ربكا از نقشهٔ پسر بزرگ خود عيسو آگاه شد، پس به دنبال يعقوب پسر كوچک خود فرستاد و به او گفت كه عيسو قصد جان او را دارد.

43ربكا به يعقوب گفت: «كاری كه بايد بكنی اين است: به حران نزد دايی خود لابان فرار كن. 44مدتی نزد او بمان تا خشم برادرت فرو نشيند 45و آنچه را كه به او كرده‌ای فراموش كند؛ آنگاه برای تو پيغام می‌فرستم تا برگردی. چرا هر دو شما را در يک روز از دست بدهم؟»

46سپس ربكا نزد اسحاق رفته به او گفت: «از دست زنان حيتّی عيسو جانم به لب رسيده است. حاضرم بميرم و نبينم كه پسرم يعقوب يک دختر حيتّی را به زنی گرفته است.»

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 27:1-46

Yakobo Anaipata Baraka Ya Isaki

1Isaki alipokuwa mzee na macho yake yalipokuwa yamekosa nguvu asiweze kuona tena, akamwita Esau mwanawe mkubwa, akamwambia, “Mwanangu.”

Akajibu, “Mimi hapa.”

2Isaki akasema, “Mimi sasa ni mzee na sijui siku ya kifo changu. 327:3 Mwa 25:27Sasa basi, chukua silaha zako, podo na upinde, uende nyikani, ukawinde nyama pori kwa ajili yangu. 4Uniandalie aina ya chakula kitamu nikipendacho uniletee nile, ili niweze kukubariki kabla sijafa.”

5Basi Rebeka alikuwa akisikiliza Isaki alipokuwa akizungumza na mwanawe Esau. Esau alipoondoka kwenda nyikani kuwinda nyama pori na kuleta, 6Rebeka akamwambia Yakobo mwanawe, “Tazama, nimemsikia baba yako akimwambia ndugu yako Esau, 7‘Niletee mawindo, kisha ukaniandalie chakula kitamu nile, ili niweze kukubariki mbele za Bwana kabla sijafa.’ 827:8 Mwa 27:13, 43Sasa, mwanangu, nisikilize kwa makini na ufanye yale ninayokuambia: 9Nenda sasa katika kundi ukaniletee wana-mbuzi wawili wazuri, ili niandalie chakula kitamu kwa ajili ya baba yako, kama vile anavyopenda. 10Kisha umpelekee baba yako ale, ili apate kukubariki kabla hajafa.”

1127:11 Mwa 25:25Yakobo akamwambia Rebeka mama yake, “Lakini ndugu yangu Esau ana nywele mwilini, mimi nina ngozi nyororo. 1227:12 Mwa 27:22Itakuwaje kama baba yangu akinigusa? Itaonekana kwake kama niliyemfanyia ujanja na kuleta laana juu yangu badala ya baraka.”

13Mama yake akamwambia, “Mwanangu, laana na iwe juu yangu. Fanya tu ninalokuambia, nenda ukaniletee hao wana-mbuzi.”

14Kwa hiyo alikwenda akawaleta, akampa mama yake, akaandaa chakula kitamu, kama vile alivyopenda baba yake. 1527:15 Mwa 27:27Kisha Rebeka akachukua nguo nzuri za Esau mwanawe wa kwanza, alizokuwa nazo nyumbani, akamvika Yakobo mwanawe mdogo. 16Pia akamfunika mikononi na sehemu laini ya shingo kwa ngozi za mbuzi. 17Hatimaye akampa Yakobo hicho chakula kitamu pamoja na mkate aliouoka.

18Akamwendea baba yake akasema, “Baba yangu.”

Akajibu, “Naam, mwanangu, wewe ni nani?”

1927:19 Mwa 27:4Yakobo akamwambia baba yake, “Mimi ni Esau mzaliwa wako wa kwanza. Nimefanya kama ulivyoniambia. Tafadhali uketi, ule sehemu ya mawindo yangu ili uweze kunibariki.”

20Isaki akamuuliza mwanawe. “Umepataje haraka namna hii, mwanangu?”

Akajibu, “Bwana Mungu wako amenifanikisha.”

2127:21 Mwa 27:12Kisha Isaki akamwambia Yakobo, “Mwanangu tafadhali sogea karibu nami ili nikupapase, nione kama hakika ndiwe Esau mwanangu, au la.”

22Yakobo akasogea karibu na baba yake Isaki, ambaye alimpapasa na kusema, “Sauti ni ya Yakobo, bali mikono ni ya Esau.” 2327:23 Mwa 27:16Hakumtambua, kwa sababu mikono yake ilikuwa na nywele kama ya ndugu yake Esau, kwa hiyo akambariki. 24Akamuuliza, “Hivi kweli wewe ni mwanangu Esau?”

Akajibu, “Mimi ndiye.”

2527:25 Mwa 27:4Kisha akasema, “Mwanangu, niletee sehemu ya mawindo yako nile, ili nipate kukubariki.”

Yakobo akamletea naye akala, akamletea na divai akanywa. 26Kisha Isaki baba yake akamwambia, “Njoo hapa, mwanangu, unibusu.”

2727:27 Kut 4:27; Ebr 11:20Kwa hiyo akamwendea akambusu. Isaki aliposikia harufu ya nguo zake, akambariki, akasema,

“Aha, harufu ya mwanangu

ni kama harufu ya shamba

ambalo Bwana amelibariki.

2827:28 Kum 33:28; 33:11; 2Sam 1:21Mungu na akupe umande kutoka mbinguni

na utajiri wa duniani:

wingi wa nafaka na divai mpya.

2927:29 Mwa 9:25; 25:23; 12:3Mataifa na yakutumikie

na mataifa yakusujudie.

Uwe bwana juu ya ndugu zako,

na wana wa mama yako wakusujudie.

Walaaniwe wale wakulaanio,

nao wale wakubarikio wabarikiwe.”

3027:30 Mwa 31:54; Kut 18:12; 24:11Baada ya Isaki kumaliza kumbariki na baada tu ya Yakobo kuondoka kwa baba yake, ndugu yake Esau akaingia kutoka mawindoni. 3127:31 Mwa 21:23, 27Naye pia akaandaa chakula kitamu akamletea baba yake. Kisha akamwambia, “Baba yangu, keti ule sehemu ya mawindo yangu, ili upate kunibariki.”

3227:32 Mwa 27:18; 21:30Isaki baba yake akamuuliza, “Wewe ni nani?”

Akajibu, “Mimi ni mwanao, mzaliwa wako wa kwanza, Esau.”

3327:33 Mwa 21:14Isaki akatetemeka kwa nguvu sana, akasema, “Alikuwa nani basi, ambaye aliwinda mawindo akaniletea? Nilikula kabla tu hujaja na nikambariki, naye hakika atabarikiwa!”

3427:34 Ebr 12:17; Kut 12:32Esau aliposikia maneno haya ya baba yake, akalia sauti kubwa na ya uchungu, na kumwambia baba yake, “Nibariki mimi, mimi pia, baba yangu!”

3527:35 Yer 9:4Lakini akasema, “Ndugu yako amekuja kwa udanganyifu na akachukua baraka yako.”

3627:36 Mwa 25:26; Ebr 12:16-17Esau akasema, “Si ndiyo sababu anaitwa Yakobo? Amenidanganya mara hizi mbili: Alichukua haki yangu ya kuzaliwa na sasa amechukua baraka yangu!” Kisha akauliza, “Hukubakiza hata baraka moja kwa ajili yangu?”

3727:37 Mwa 27:28; Kum 16:13Isaki akamjibu Esau, “Nimemfanya yeye kuwa bwana juu yako, pia nimewafanya ndugu zako wote kuwa watumishi wake, nimemtegemeza kwa nafaka na divai mpya. Sasa nitaweza kukufanyia nini, mwanangu?”

3827:38 Rut 1:9; Ebr 12:17Esau akamwambia baba yake, “Je, baba yangu una baraka moja tu? Unibariki mimi pia, baba yangu!” Kisha Esau akalia kwa sauti kubwa.

3927:39 Ebr 11:20; Mwa 27:28Baba yake Isaki akamjibu, akamwambia,

“Makao yako yatakuwa

mbali na utajiri wa dunia,

mbali na umande wa mbinguni juu.

4027:40 2Sam 8:14; 2Fal 8:20-22Utaishi kwa upanga,

nawe utamtumikia ndugu yako,

lakini wakati utakapokuwa umejikomboa,

utatupa nira yake

kutoka shingoni mwako.”

Yakobo Anakimbilia Kwa Labani

4127:41 1Sam 17:28; Hos 10:14Esau akawa na kinyongo dhidi ya Yakobo kwa ajili ya baraka ambazo baba yake alikuwa amembariki. Akasema moyoni mwake, “Siku za kuomboleza kwa ajili ya baba yangu zimekaribia, ndipo nitamuua ndugu yangu Yakobo.”

42Rebeka alipokwisha kuambiwa yale aliyoyasema Esau mwanawe mkubwa, alimwita Yakobo mwanawe mdogo, akamwambia, “Ndugu yako Esau anajifariji kwa wazo la kukuua. 4327:43 Mwa 24:29; 11:31Sasa basi, mwanangu, fanya nisemalo: Kimbilia haraka kwa Labani ndugu yangu kule Harani. 44Ukae naye kwa muda mpaka ghadhabu ya ndugu yako itulie. 4527:45 Mwa 26:3Wakati ndugu yako atakapokuwa hana hasira nawe tena na amesahau uliyomtendea, nitakupelekea ujumbe urudi. Kwa nini niwapoteze wote wawili kwa siku moja?”

4627:46 Mwa 26:35; Ay 7:7Kisha Rebeka akamwambia Isaki, “Nimechukia kuishi kwa sababu ya hawa wanawake wa Kihiti. Ikiwa Yakobo ataoa mke miongoni mwa wanawake wa nchi hii, wanawake wa Kihiti kama hawa, sitakuwa na faida kuendelea kuishi.”