Ezequiel 48 – OL & NEN

O Livro

Ezequiel 48:1-35

A divisão da terra

1Esta é a lista das tribos com o território que cada uma receberá.

Dan: desde a fronteira do norte, no Mediterrâneo, através de Hetlom até Hamate, e depois até Hazar-Enã, na fronteira entre Damasco, a sul, e Hamate, a norte. São esses os limites a leste e a oeste da terra.

2Aser: o seu território fica a sul do território de Dan e tem as mesmas fronteiras a leste e a oeste.

3Naftali: fica a sul de Aser e tem também as mesmas fronteiras a leste e a oeste.

4Manassés: fica a sul de Naftali, com os mesmos limites a leste e a oeste.

5A seguir, junto a Manassés para o sul, fica Efraim,

6depois ficará Rúben e,

7por fim Judá, todos com as mesmas linhas de limite a leste e a oeste.

8No território de Judá, desde a fronteira oriental até ao mar Mediterrâneo, a ocidente, será reservado um território que terá a mesma extensão que o de cada tribo, ou seja, 12,5 quilómetros de extensão. O templo será estabelecido no centro desta área.

9Além disso, haverá uma faixa de território com 12,5 quilómetros de comprimento e 5 quilómetros de largura, 10-11de norte a sul, rodeando o templo. Será para os sacerdotes, os filhos de Zadoque que me obedeceram e não pecaram com o povo de Israel e o resto da tribo de Levi. 12É porção especial de terra que lhe é atribuída, a mais santíssima de todas.

13A seguir a essa área há outra onde viverão os levitas. Será do mesmo tamanho e com a mesma forma que a primeira. Juntas medirão 12,5 quilómetros por 5 quilómetros. 14Nenhuma parte desta terra especial poderá ser vendida, negociada ou arrendada, pois pertence ao Senhor, é santa.

15A faixa de terra de 12,5 quilómetros de comprimento por 2,5 quilómetros de largura, a sul da secção atribuída ao templo, será para uso público com a cidade no centro. 16A própria cidade será quadrada e terá 2,5 quilómetros de largura. 17Uma terra aberta para pastagens rodeará a cidade e terá 125 metros de extensão. 18No exterior da cidade, estendendo-se numa faixa de 5 quilómetros a leste e a oeste, na margem da terra sagrada, haverá um campo para a agricultura, pertencente à cidade, para uso público. 19Estará aberto a quem trabalhar na cidade, seja qual for a sua origem em Israel.

20Toda esta área, incluindo as terras sagradas e as terras da cidade, será um quadrado com 12,5 quilómetros de largo.

21-22A terra em ambos os lados desta área, estendendo-se para leste e oeste até às fronteiras de Israel, pertencerá ao príncipe. Esta terra, que ficará entre as porções atribuídas a Judá e Benjamim, terá 12,5 quilómetros e será quadrada, de cada lado das terras, tanto da sagrada como da terra da cidade. No meio ficará a parte reservada ao templo.

23As secções dadas às tribos restantes são as seguintes. Benjamim: estende-se através de todo o território de Israel, desde a fronteira do oriente até à do ocidente.

24Ao sul fica a de Simeão, estendendo-se igualmente entre estas as fronteiras oriental e ocidental.

25Depois é Issacar com os mesmos limites.

26A seguir vem Zebulão com a mesma forma.

27Gad também com os mesmos limites.

28Mas a sua fronteira a sul vai de Tamar até às fontes de Meribá-Cades, seguindo depois pela Ribeira do Egito até ao Mediterrâneo.

29É este o loteamento que se fará entre cada tribo, conforme a palavra do Senhor Deus.

As portas da cidade

30-31Cada porta da cidade terá o nome de cada uma das tribos de Israel em sua honra. A norte, na sua muralha de 2,25 quilómetros, haverá três entradas, uma com o nome de Rúben, outra de Judá e outra de Levi. 32A leste, na muralha igualmente de 2,25 quilómetros, haverá também três portas, com os nomes de José, Benjamim e Dan. 33A sul, na muralha que terá o mesmo comprimento, haverá as portas de Simeão, Issacar e Zebulão. 34E a oeste, da mesma maneira, ver-se-ão as portas de Gad, Aser e Naftali.

35O perímetro total da cidade medirá 9 quilómetros e chamar-se-á:

o Senhor está ali.”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 48:1-35

Mgawanyo Wa Nchi

148:1 Mwa 30:6; Hes 34:7-9; Eze 47:15-20“Haya ndiyo majina ya makabila na sehemu zao: Kwenye mpaka wa kaskazini, Dani atakuwa na sehemu moja, mpaka huo utafuata barabara ya Hethloni hadi Lebo-Hamathi, Hasar-Enani hata mpaka wa kaskazini wa Dameski karibu na Hamathi utakuwa sehemu ya huo mpaka wake kuanzia upande wa mashariki hadi upande wa magharibi.

248:2 Yos 19:24-31“Asheri atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Dani kuanzia mashariki hadi upande wa magharibi.

348:3 Yos 19:32-39“Naftali atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Asheri kuanzia mashariki hadi magharibi.

448:4 Yos 17:1-11“Manase atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Naftali kuanzia mashariki hadi magharibi.

548:5 Yos 16:5-9; 17:7-10, 17“Efraimu atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Manase kuanzia mashariki hadi magharibi.

648:6 Yos 13:15-21“Reubeni atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Efraimu kuanzia mashariki hadi magharibi.

748:7 Yos 15:1-63“Yuda atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Reubeni kuanzia mashariki hadi magharibi.

848:8 Eze 45:1; 48:21“Kupakana na nchi ya Yuda kuanzia mashariki mpaka magharibi itakuwa ndiyo sehemu utakayoitoa ili kuwa toleo maalum. Itakuwa na upana wa dhiraa 25,00048:8 Dhiraa 25,000 ni sawa na kilomita 11.25. na urefu wake kuanzia mashariki mpaka magharibi utakuwa ule ule wa sehemu moja ya kabila, mahali patakatifu patakuwa katikati ya eneo hilo.

948:9 Eze 45:1“Hiyo sehemu maalum mtakayotoa kwa Bwana itakuwa na urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,00048:9 Dhiraa 10,000 ni sawa na kilomita 4.5. 1048:10 Eze 45:1-4Hii itakuwa ni sehemu takatifu kwa ajili ya makuhani. Itakuwa na urefu wa dhiraa 25,000 upande wa kaskazini, upana wa dhiraa 10,000 upande wa magharibi, dhiraa 10,000 upande wa mashariki na urefu wa dhiraa 25,000 upande wa kusini. Katikati yake patakuwa mahali patakatifu pa Bwana. 1148:11 2Sam 8:17; Law 8:35; Eze 14:11; 44:15; Yer 23:11; Neh 9:34Hii itakuwa kwa ajili ya makuhani waliowekwa wakfu, Wasadoki, waliokuwa waaminifu katika kunitumikia nao hawakupotoka kama Walawi walivyofanya wakati Waisraeli walipopotoka. 12Itakuwa toleo maalum kwao kutoka sehemu takatifu ya nchi, yaani, sehemu takatifu sana, inayopakana na nchi ya Walawi.

1348:13 Eze 45:5“Kando ya nchi ya makuhani, Walawi watakuwa na mgawo wa urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Urefu wake utakuwa jumla dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. 1448:14 Law 25:34; 27:10, 28Hawataruhusiwa kuuza wala kuibadilisha hata mojawapo. Hii ndiyo sehemu nzuri ya nchi kuliko nyingine zote, hivyo haitakuwa mikononi mwa watu wengine, kwa sababu ni takatifu kwa Bwana.

1548:15 Kum 20:5; Eze 42:20; 44:23; 45:6“Eneo linalobaki lenye upana wa dhiraa 5,00048:15 Dhiraa 5,000 ni sawa na kilomita 2.25. na urefu wa dhiraa 25,000, litakuwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya mji, kwa ajili ya ujenzi wa nyumba na malisho. Mji utakuwa katikati yake 1648:16 Ufu 21:16nao utakuwa na vipimo hivi: upande wa kaskazini dhiraa 4,500,48:16 Dhiraa 4,500 ni sawa na kilomita 2.025. upande wa kusini dhiraa 4,500, upande wa mashariki dhiraa 4,500 na upande wa magharibi dhiraa 4,500. 17Sehemu ya malisho kwa ajili ya mji itakuwa na eneo la dhiraa 25048:17 Dhiraa 250 ni sawa na sentimita 112.5. upande wa kaskazini, dhiraa 250 upande wa kusini, dhiraa 250 upande wa mashariki na dhiraa 250 upande wa magharibi. 1848:18 Eze 21:16Eneo linalobaki, linalopakana na sehemu takatifu likiwa na urefu sawa nalo, litakuwa dhiraa 10,000 upande wa mashariki na dhiraa 10,000 upande wa magharibi. Mazao yake yatawapa watumishi wa mji chakula. 1948:19 Eze 45:6; Ufu 7:5Watumishi wa mji wanaolima shamba hili watatoka katika makabila yote ya Israeli. 2048:20 Hes 24:5; Isa 33:20; Ufu 21:16Eneo lote la hiyo sehemu litakuwa mraba, yaani, dhiraa 25,000 kila upande. Kama toleo maalum mtatenga sehemu takatifu, pamoja na milki ya mji.

2148:21 Eze 45:7; Yos 18:1; Yn 12:32; Rum 15:9-12“Eneo linalobaki pande zote za eneo linalofanya sehemu takatifu na milki ya mji litakuwa mali ya mkuu atawalaye. Eneo hili litaenea upande wa mashariki kuanzia kwenye dhiraa 25,000 za sehemu takatifu hadi mpaka wa mashariki na kuelekea upande wa magharibi kuanzia kwenye dhiraa 25,000 hadi mpaka wa magharibi. Maeneo yote haya mawili yanayoenda sambamba na urefu wa sehemu za makabila yatakuwa ya mkuu anayetawala, na sehemu ile takatifu pamoja na mahali patakatifu pa Hekalu itakuwa katikati yake. 22Kwa hiyo milki ya Walawi na milki ya mji vitakuwa katikati ya eneo lile ambalo ni mali ya mkuu anayetawala. Eneo la mkuu anayetawala litakuwa kati ya mpaka wa Yuda na mpaka wa Benyamini.

2348:23 Yos 18:11-28“Kuhusu makabila yaliyobaki: Benyamini atakuwa na sehemu moja, itakayoanzia upande wa mashariki hadi upande wa magharibi.

2448:24 Mwa 29:33; Yos 19:1-9“Simeoni atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Benyamini kuanzia mashariki hadi magharibi.

2548:25 Yos 19:17-23“Isakari atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Simeoni kuanzia mashariki hadi magharibi.

2648:26 Yos 13:24-28“Zabuloni atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Isakari kuanzia mashariki hadi magharibi.

2748:27 Yos 13:24-28“Gadi atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Zabuloni kuanzia mashariki hadi magharibi.

2848:28 Mwa 14:7; Hes 34:6, 15; Mwa 15:18; Isa 27:12; Eze 47:19“Mpaka wa kusini wa Gadi utapita kusini kuanzia Tamari hadi maji ya Meriba-Kadeshi, kisha kupitia upande wa Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu.48:28 Bahari Kuu hapa ina maana ya Bahari ya Mediterania.

2948:29 Eze 47:14, 21, 22; 45:1“Hii ndiyo nchi mtakayogawanya kuwa urithi kwa makabila ya Israeli, nazo zitakuwa sehemu zao,” asema Bwana Mwenyezi.

Malango Ya Mji

30“Haya yatakuwa ndiyo malango ya mji ya kutokea: Kuanzia upande wa kaskazini, ambayo urefu wake ni dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu, 3148:31 Ufu 21:12; Isa 60:18malango hayo ya mji yatapewa majina ya makabila ya Israeli. Malango hayo matatu ya upande wa kaskazini moja litakuwa lango la Reubeni, lango la Yuda na lango la Lawi.

32“Upande wa mashariki, wenye urefu wa dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu: lango la Yosefu, lango la Benyamini na lango la Dani.

33“Upande wa kusini, wenye urefu wa dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu: lango la Simeoni, lango la Isakari na lango la Zabuloni.

3448:34 2Nya 4:4; Ufu 21:12-13“Upande wa magharibi, wenye urefu wa dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu: lango la Gadi, lango la Asheri na lango la Naftali.

3548:35 Za 72:8; Ufu 21:3; Zek 2:10; Amu 6:24; Isa 12:6; 24:23; Yer 31:17“Urefu wote kuzunguka utakuwa dhiraa 18,000.48:35 Dhiraa 18,000 ni sawa na kilomita 8.1.

“Nalo jina la mji huo kuanzia wakati huo na kuendelea litakuwa:

Bwana yupo hapa.”