Zaburi 134
Wito Wa Kumsifu Mungu
Wimbo wa kwenda juu.
1134:1 Za 130:6; 113:1; 135:1, 2; Ufu 19:5; Lk 2:37; 1Nya 15:2; 23:30; Hes 16:9Msifuni Bwana, ninyi nyote watumishi wa Bwana,
ninyi mnaotumika usiku ndani ya nyumba ya Bwana.
2134:2 Za 33:2; 103:1; 28:2; 1Tim 2:8Inueni mikono yenu katika pale patakatifu
na kumsifu Bwana.
3134:3 Za 124:8; 20:2; 128:5; Law 25:21Naye Bwana, Muumba wa mbingu na dunia,
awabariki kutoka Sayuni.