Isaías 38 – NVI & NEN

Nueva Versión Internacional

Isaías 38:1-22

Enfermedad de Ezequías

38:1-82R 20:1-11; 2Cr 32:24-26

1Por aquellos días Ezequías se enfermó gravemente y estuvo a punto de morir. El profeta Isaías, hijo de Amoz, fue a verlo y le dijo: «Así dice el Señor: “Pon tu casa en orden, porque vas a morir; no te recuperarás”».

2Ezequías volvió el rostro hacia la pared y rogó al Señor: 3«Recuerda, Señor, que yo me he conducido delante de ti con lealtad e integridad y he hecho lo que te agrada». Y Ezequías lloró amargamente.

4Entonces la palabra del Señor vino a Isaías: 5«Ve y dile a Ezequías: “Así dice el Señor, Dios de su antepasado David: He escuchado tu oración y he visto tus lágrimas. Voy a darte quince años más de vida. 6Y a ti y a esta ciudad los libraré de caer en manos del rey de Asiria. Yo defenderé esta ciudad.

7»”Esta es la señal que el Señor te dará para confirmar lo que te ha prometido: 8Haré que en la escala de Acaz la sombra del sol retroceda las diez gradas que ya ha bajado”». ¡Entonces, la luz del sol retrocedió las diez gradas que ya había bajado!

Escrito de Ezequías

9Después de su enfermedad y recuperación, Ezequías, rey de Judá, escribió:

10«Yo decía: “¿En la plenitud de mi vida,

debo pasar por las puertas de la muerte38:10 de la muerte. Lit. del Seol.

y ser privado del resto de mis días?”.

11Yo decía: “Ya no veré más al Señor

en esta tierra de los vivientes;

ya no contemplaré más a los seres humanos,

a los que habitan este mundo”.38:11 este mundo (mss. hebreos); el lugar de cesación (TM).

12Me quitaron mi casa, me la arrebataron,

como si fuera la tienda de campaña de un pastor.

Como un tejedor enrollé mi vida

y él me la arrancó del telar.

¡De la noche a la mañana acabó conmigo!

13Pacientemente esperé hasta la aurora,

pero él, como león, me quebró todos los huesos.

¡De la noche a la mañana acabó conmigo!

14Chillé como golondrina, como grulla;

gemí como paloma.

Mis ojos se cansaron de mirar al cielo.

¡Angustiado estoy, Señor!

¡Acude en mi ayuda!

15»Pero ¿qué puedo decir?

Él mismo me lo anunció y así lo ha hecho.

Toda mi vida andaré humildemente,

por causa de la amargura de mi alma.

16Señor, por tales cosas viven los hombres

y también mi espíritu encuentra vida en ellas.

Tú me devolviste la salud

y me diste vida.

17Sin duda, fue para mi bien

pasar por tal angustia.

Con tu amor me guardaste

de la fosa destructora,

y les diste la espalda

a todos mis pecados.

18El sepulcro38:18 sepulcro. Lit. Seol. nada te agradece;

la muerte no te alaba.

Los que descienden a la fosa

nada esperan de tu fidelidad.

19Los que viven y solo los que viven, son los que te alaban,

como hoy te alabo yo.

Los padres hablarán a sus hijos

de tu fidelidad.

20»El Señor me salvará,

y en el Templo del Señor

todos los días de nuestra vida

cantaremos con instrumentos de cuerda».

21Isaías había dicho: «Preparen una pasta de higos, aplíquensela en la llaga y él se recuperará».

22Y Ezequías había preguntado: «¿Qué señal recibiré de que se me permitirá subir al Templo del Señor?».

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 38:1-22

Kuugua Kwa Mfalme Hezekia

(2 Wafalme 20:1-11; 2 Nyakati 32:24-26)

138:1 Isa 37:2-3; 2Sam 17:23; 2Fal 8:10Katika siku hizo Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Nabii Isaya mwana wa Amozi akaenda kwake na kumwambia, “Hili ndilo asemalo Bwana: Tengeneza mambo ya nyumba yako, kwa sababu utakufa, hutapona.”

2Hezekia akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana: 338:3 Neh 5:19; 13:14; Kum 6:18; Za 26:3; 1Fal 8:61; 2Nya 29:19; Za 6:8“Ee Bwana, kumbuka jinsi nilivyoenenda mbele zako kwa uaminifu na kujitoa kwa moyo wangu wote, na kufanya yaliyo mema machoni pako.” Naye Hezekia akalia kwa uchungu.

438:4 1Sam 13:13; Isa 39:5Ndipo neno la Bwana likamjia Isaya, kusema: 538:5 2Fal 18:2-3; Za 6:6“Nenda ukamwambie Hezekia, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa baba yako Daudi: Nimeyasikia maombi yako na nimeona machozi yako. Nitakuongezea miaka kumi na mitano katika maisha yako. 638:6 Isa 31:5; 37:35Nami nitakuokoa wewe pamoja na mji huu mkononi mwa mfalme wa Ashuru. Nitaulinda mji huu.

738:7 Mwa 24:14; 2Fal 20:8; 2Nya 32:31; Isa 7:11, 14; 20:3“ ‘Hii ndiyo ishara ya Bwana kwako ya kwamba Bwana atafanya kile alichoahidi: 838:8 Yos 10:13Nitafanya kivuli cha jua kwenye ngazi iliyojengwa na Ahazi kirudi nyuma madaraja kumi.’ ” Hivyo jua likarudi nyuma madaraja kumi ambayo lilikuwa limeshuka.

9Maandiko ya Hezekia mfalme wa Yuda baada ya kuugua kwake na kupona:

1038:10 Ay 17:16; Za 102:24; 2Kor 1:9; Ay 17:11; Za 107:18Nilisema, “Katika ustawi wa maisha yangu,

je, ni lazima nipite katika malango ya mauti,38:10 Mauti hapa maana yake ni Kuzimu.

na kupokonywa miaka yangu iliyobaki?”

1138:11 Za 27:13; Ay 28:13; 35:14; Isa 12:2; Za 116:5Nilisema, “Sitamwona tena Bwana,

Bwana katika nchi ya walio hai,

wala sitamtazama tena mwanadamu,

wala kuwa na wale ambao sasa wanakaa katika ulimwengu huu.

1238:12 2Kor 5:4; Ay 4:21; Isa 33:20; Ebr 1:12; Hes 11:15; Za 32:4; 1Pet 1:13-14Kama hema la mchunga mifugo,

nyumba yangu imebomolewa na kutwaliwa kutoka kwangu.

Kama mfumaji nimevingirisha maisha yangu,

naye amenikatilia mbali kutoka kitanda cha mfumi.

Mchana na usiku uliyakomesha maisha yangu.

1338:13 Ay 9:17; Mao 3:4; Yer 34:17; Za 37:7; 51:8; Ay 10:16; Dan 6:24Nilingoja kwa uvumilivu hadi mapambazuko,

lakini alivunja mifupa yangu yote kama simba.

Mchana na usiku uliyakomesha maisha yangu.

1438:14 Isa 59:11; Mwa 50:24; Ay 17:3; Mwa 8:8; Za 6:7Nililia kama mbayuwayu au korongo,

niliomboleza kama hua aombolezaye.

Macho yangu yalififia nilipotazama mbinguni.

Ee Bwana, ninataabika, njoo unisaidie!”

1538:15 Ay 7:11; 1Fal 21:27; Za 39:9; 2Sam 7:20Lakini niseme nini?

Amesema nami, naye yeye mwenyewe amelitenda hili.

Nitatembea kwa unyenyekevu

katika miaka yangu yote

kwa sababu ya haya maumivu makali

ya nafsi yangu.

1638:16 Ebr 12:9; Za 119:25Bwana, kwa mambo kama haya watu huishi,

nayo roho yangu hupata uzima katika hayo pia.

Uliniponya

na kuniacha niishi.

1738:17 Yer 31:34; Mik 7:19; Ay 17:16; Za 103:3, 12; Rum 8:28; Ebr 12:11; Isa 43:25Hakika ilikuwa ya faida yangu

ndiyo maana nikapata maumivu makali.

Katika upendo wako ukaniokoa

kutoka shimo la uharibifu;

umeziweka dhambi zangu zote

nyuma yako.

1838:18 Mhu 9:10; Hes 16:30; Za 6:5; 30:9; 88:10-11; 115:17Kwa maana kaburi38:18 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. haliwezi kukusifu,

mauti haiwezi kuimba sifa zako;

wale washukao chini shimoni

hawawezi kuutarajia uaminifu wako.

1938:19 Kum 6:7; 11:19; Za 78:3; 118:7; 119:175Walio hai, walio hai: hao wanakusifu,

kama ninavyofanya leo.

Baba huwaambia watoto wao

habari za uaminifu wako.

2038:20 Za 68:25; 9:13; 45:8; 116:17-19; 63:4; 23:6Bwana ataniokoa,

nasi tutaimba kwa vyombo vya nyuzi

siku zote za maisha yetu

katika Hekalu la Bwana.

21Isaya alikuwa amesema, “Tengenezeni dawa ya kubandika ya tini, mweke juu ya jipu, naye atapona.”

22Hezekia alikuwa ameuliza, “Kutakuwa na ishara gani kwamba nitapanda kwenda Hekalu la Bwana?”