Zekaria 7 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zekaria 7:1-14

Haki Na Rehema, Sio Kufunga

17:1 Ezr 5:1; Neh 1:1Katika mwaka wa nne wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria siku ya nne ya mwezi wa tisa, mwezi wa Kisleu. 27:2 Yer 26:19; Zek 8:21; Hag 2:10-14Watu wa Betheli walikuwa wamemtuma Shareza na Regem-Meleki pamoja na watu wao, kumsihi Bwana 37:3 Zek 12:12-14; 2Fal 25:9; Yer 52:12-14; Kum 17:9; Mal 2:7kwa kuwauliza makuhani wa nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na manabii, “Je, imempasa kuomboleza na kufunga katika mwezi wa tano, kama ambavyo nimekuwa nikifanya kwa miaka mingi?”

4Kisha neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote likanijia kusema: 57:5 Isa 58:5; 2Fal 25:25; Dan 9:2; Zek 1:12; Mt 6:16; Rum 14:6“Waulize watu wote wa nchi na makuhani, ‘Je, mlipofunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba kwa miaka sabini iliyopita, mlifunga kweli kwa ajili yangu? 67:6 Isa 43:23Na mlipokuwa mkila na kunywa, je, hamkuwa mnasherehekea kwa ajili ya nafsi zenu? 77:7 Isa 1:11-20; Yer 22:21; 17:26; 44:4-5Je, haya sio maneno ya Bwana aliyosema kupitia manabii waliotangulia, wakati Yerusalemu pamoja na miji inayoizunguka ilipokuwa katika hali ya utulivu na ya mafanikio, wakati Negebu na Shefala zikiwa zimekaliwa na watu?’ ”

8Neno la Bwana likamjia tena Zekaria: 97:9 Yer 22:3; 42:5; Zek 8:16; Kum 22:1“Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Fanyeni hukumu za haki, onyesheni rehema na huruma ninyi kwa ninyi. 107:10 Yer 49:11; Kut 22:21-22; Law 25:17; Isa 1:23; Ay 35:8; Eze 45:9; Mik 6:8Msimwonee mjane wala yatima, mgeni wala maskini. Msiwaziane mabaya mioyoni mwenu ninyi kwa ninyi.’

117:11 Isa 9:9; Yer 32:33; 11:10; 17:23; 8:5; Eze 5:6“Lakini wakakataa kusikiliza, wakanipa kisogo kwa ukaidi na kuziba masikio yao. 127:12 Yer 5:3; 17:1; 42:21; Eze 11:19; Neh 9:29; Dan 9:12Wakaifanya mioyo yao migumu kama jiwe gumu na hawakuisikiliza sheria au maneno ambayo Bwana Mwenye Nguvu Zote aliyatuma kwa njia ya Roho wake kupitia manabii waliotangulia. Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote alikasirika sana.

137:13 Yer 7:27; 11:11; 14:12; Mit 1:28; Isa 1:15; Mao 3:44; Eze 20:31“ ‘Wakati nilipoita, hawakusikiliza, kwa hiyo walipoita, sikusikiliza,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. 147:14 Kum 4:27; 28:64-67; Law 26:33; Yer 7:34; 23:19; 44:6; Za 44:11; Isa 33:8; Eze 12:19‘Niliwatawanya kwa upepo wa kisulisuli miongoni mwa mataifa yote, mahali ambapo walikuwa wageni. Nchi ikaachwa ukiwa nyuma yao kiasi kwamba hakuna aliyeweza kuingia au kutoka. Hivi ndivyo walivyoifanya ile nchi iliyokuwa imependeza kuwa ukiwa.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

撒迦利亞書 7:1-14

呼籲公義和憐憫

1大流士王四年九月,即基斯流月四日,耶和華的話傳給了撒迦利亞2那時,伯特利人差遣沙利色利堅米勒及其隨從去向耶和華求恩。 3他們問萬軍之耶和華殿裡的祭司和先知:「我們還要照多年的慣例在五月哀傷、禁食嗎?」

4萬軍之耶和華的話傳給了我,說: 5「你要對境內的民眾和祭司說,『七十年來,你們在五月和七月禁食、哀傷,難道真的是為了我嗎? 6你們吃喝,難道不是為自己吃、為自己喝嗎? 7這些不是耶和華藉從前的先知所宣告的嗎?當時耶路撒冷和周圍的城邑人口興盛、繁榮,南地和丘陵都有人居住。』」

8耶和華的話又傳給了撒迦利亞,說: 9「萬軍之耶和華曾對你們的祖先說,『要秉公行義,彼此以慈愛和憐憫相待。 10不可欺壓寡婦、孤兒、寄居者和窮人,不可設陰謀彼此相害。』 11他們卻不理會,背過身去,充耳不聞, 12心如鐵石,不遵從律法,也不遵從萬軍之耶和華藉著祂的靈指示從前的先知所說的話。因此,萬軍之耶和華非常憤怒。 13祂說,『我曾呼喚他們,他們不聽;將來他們呼求我,我也不聽。 14我要用旋風把他們吹散到陌生的萬國中,使他們的土地荒涼、杳無人跡,因為他們使美好的土地一片荒涼。』」