Zekaria 4 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zekaria 4:1-14

Maono Ya Tano: Kinara Cha Taa Cha Dhahabu Na Mizeituni Miwili

14:1 Dan 8:18; Yer 31:26Kisha malaika aliyezungumza nami akarudi na kuniamsha, kama mtu aamshwavyo kutoka usingizi wake. 24:2 Yer 1:13; Kut 25:31; Ufu 1:12; 4:5Akaniuliza, “Unaona nini?”

Nikajibu, “Ninaona kinara cha taa cha dhahabu tupu, nacho kina bakuli juu yake na taa zake saba juu yake, tena iko mirija saba ya kuleta mafuta, kwenye taa zote zilizo juu yake. 34:3 Ufu 11:4; Za 1:3Pia kuna mizeituni miwili karibu yake, mmoja upande wa kuume wa bakuli na mwingine upande wa kushoto.”

4Nikamuuliza malaika aliyezungumza nami, “Hivi ni vitu gani, bwana wangu?”

54:5 Zek 1:9Akanijibu, “Hujui kuwa hivi ni vitu gani?”

Nikajibu, “Hapana, bwana wangu.”

64:6 1Nya 3:19; Ezr 5:2; 1Sam 2:9; 13:22; 1Fal 19:12; Neh 9:20; Dan 2:34; Isa 11:2-4Kisha akaniambia, “Hili ni neno la Bwana kwa Zerubabeli: ‘Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa Roho yangu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

74:7 Za 26:12; 118:22; Yer 51:25; 1Nya 15:28; Isa 40:3-4; Mt 21:21; Ezr 3:11“Wewe ni kitu gani, ee mlima mkubwa sana? Mbele ya Zerubabeli wewe utakuwa ardhi tambarare. Kisha ataweka jiwe la juu kabisa la mwisho na watu wakipiga kelele wakisema, ‘Mungu libariki! Mungu libariki!’ ”

8Kisha neno la Bwana likanijia: 94:9 Ezr 3:11; 6:15; Zek 2:9; 6:12; 1Kor 2:4“Mikono ya Zerubabeli iliweka msingi wa Hekalu hili, mikono yake pia italimalizia. Kisha mtajua ya kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma mimi kwenu.

104:10 Hag 2:23; Ezr 5:1; Neh 12:1; Ay 38:5; 2Nya 16:9; Ufu 5:6“Ni nani anayeidharau siku ya mambo madogo? Watu watashangilia watakapoona timazi mkononi mwa Zerubabeli.

“(Hizi saba ni macho ya Bwana ambayo huzunguka duniani kote.)”

114:11 Ufu 11:4Kisha nikamuuliza yule malaika, “Hii mizeituni miwili iliyoko upande wa kuume na wa kushoto wa kinara cha taa ni nini?”

12Tena nikamuuliza, “Haya matawi mawili ya mizeituni karibu na hiyo mirija miwili ya dhahabu inayomimina mafuta ya dhahabu ni nini?”

13Akajibu, “Hujui kuwa haya ni nini?”

Nikamjibu, “Hapana, bwana wangu.”

144:14 Kut 29:7; 40:15; Za 45:7; Isa 20:3; Dan 9:24-26Kwa hiyo akasema, “Hawa ni wawili ambao wamepakwa mafuta ili kumtumikia Bwana wa dunia yote.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

撒迦利亚书 4:1-14

金灯台和橄榄树

1那位与我说话的天使又来唤醒我,像唤醒睡觉的人一样。 2他问我:“你看见了什么?”

我说:“我看见一个纯金的灯台,上面有一个油碗,灯台上有七盏灯,每盏灯有七个灯芯。 3灯台旁边有两棵橄榄树,左右各一棵。” 4我问与我说话的天使:“主啊,这是什么意思?” 5他说:“你不知道吗?”我说:“主啊,我不知道。”

6他对我说:“这是耶和华对所罗巴伯讲的话。万军之耶和华说,‘不靠权势,不靠才能,乃靠我的灵。 7大山啊,你算什么?你必在所罗巴伯面前化为平地。他必搬出那块封殿顶的石头,伴随着欢呼声——愿恩典、恩典归于这殿!’”

8耶和华的话又传给了我,说: 9所罗巴伯的手奠立这殿的根基,他的手也必完成这项工程。那时你便知道是万军之耶和华差遣我到你们这里来的。 10谁敢藐视这微不足道的日子?人们看见所罗巴伯手中拿着线锤时,就必欢喜。

“这七盏灯是耶和华遍察天下的眼睛。”

11我又问天使:“灯台左右的两棵橄榄树是什么意思?” 12然后我又问道:“流出橄榄油的两个金管旁边的两根橄榄枝是什么意思?” 13他说:“你不知道吗?”我说:“主啊,我不知道。” 14他说:“这是侍立在天下之主旁边的两位受膏者。”