Zekaria 14 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zekaria 14:1-21

Bwana Yuaja Kutawala

114:1 Isa 13:6; 23:18; Yoe 1:15; Mal 4:1Siku ya Bwana inakuja ambayo nyara zilizotekwa kwenu zitagawanywa miongoni mwenu.

214:2 Isa 2:3; Zek 12:3; 13:8; Eze 5:8; Mwa 34:29; Mao 5:11; Isa 13:6; Yoe 3:2Nitayakusanya mataifa yote huko Yerusalemu kupigana dhidi yake, mji utatekwa, nyumba zitavamiwa na kuporwa na wanawake watanajisiwa. Nusu ya mji watakwenda uhamishoni, lakini watakaobaki hawataondolewa kutoka mjini.

314:3 Zek 9:14-15; 8:9; Isa 8:9Kisha Bwana atatoka na kupigana dhidi ya watu wa yale mataifa, kama apiganavyo siku ya vita. 414:4 Eze 11:23; Hes 16:31; Mdo 1:11-12; Yoe 3:12Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, mashariki mwa Yerusalemu, nao Mlima wa Mizeituni utagawanyika mara mbili kuanzia mashariki hadi magharibi, ukifanya bonde kubwa, nusu ya mlima ukisogea kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini. 514:5 Isa 29:6; 66:15-16; Mt 16:27; 25:31; Yud 14; Mt 24:30; Yoe 3:11Nanyi mtakimbia kupitia katika bonde hilo la mlima wangu kwa kuwa litaenea hadi Aseli. Mtakimbia kama mlivyokimbia tetemeko la ardhi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda. Kisha Bwana Mungu wangu atakuja na watakatifu wote pamoja naye.

614:6 Isa 13:10; Yer 4:23Siku hiyo hakutakuwepo nuru, baridi wala theluji. 714:7 Yer 30:7; Ufu 21:23-25; 22:5; Isa 13:10; 30:26Itakuwa siku ya kipekee, isiyo na mchana wala usiku, siku ijulikanayo na Bwana. Jioni inapofika nuru itakuwepo.

814:8 Eze 47:1-12; Yn 7:38; Ufu 22:1-2; Isa 30:25; Yoe 2:20; Mwa 8:22Siku hiyo, maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu, nusu kwenda kwenye bahari ya mashariki,14:8 Yaani Bahari ya Chumvi au Bahari Mfu. na nusu kwenda kwenye bahari ya magharibi14:8 Yaani Bahari ya Mediterania. wakati wa kiangazi na wakati wa masika.

914:9 Za 22:28; 47:7; Oba 1:21; Kum 6:4; Isa 45:24; Ufu 15:1; Hab 2:14; Efe 4:5-6; Za 2:8Bwana atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo atakuwepo Bwana mmoja na jina lake litakuwa jina pekee.

1014:10 1Fal 15:22; Yos 15:32; Isa 2:2; Yer 20:2; 30:18; Amo 9:11; Zek 12:6; 2Fal 14:13; Neh 3:1Nchi yote kuanzia Geba, kaskazini mwa Yuda, hadi Rimoni, kusini mwa Yerusalemu, itakuwa kama Araba.14:10 Araba maana yake Nchi tambarare. Lakini Yerusalemu utainuliwa juu na kubaki mahali pake, toka Lango la Benyamini hadi mahali pa Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni na kutoka Mnara wa Hananeli hadi kwenye mashinikizo ya divai ya mfalme. 1114:11 Zek 2:4; Za 48:8; Eze 34:25-28; Yer 31:40Utakaliwa na watu, kamwe hautaharibiwa tena, Yerusalemu utakaa salama.

1214:12 Isa 11:4; Law 26:16; Kum 28:22; Ay 18:13Hii ndiyo tauni ambayo Bwana atapiga nayo mataifa yote ambayo yalipigana dhidi ya Yerusalemu: Nyama ya miili yao itaoza wangali wamesimama kwa miguu yao, macho yao yataoza kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza vinywani mwao. 1314:13 Mwa 35:5; Amu 7:22; Zek 11:6; 1Sam 14:15Katika siku hiyo Bwana atawatia wanaume hofu kuu. Kila mwanaume atakamata mkono wa mwenzake nao watashambuliana. 1414:14 Zek 12:2; Isa 23:18Yuda pia atapigana katika Yerusalemu. Utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka Yerusalemu utakusanywa, wingi wa dhahabu, fedha na nguo. 15Tauni ya aina iyo hiyo itapiga farasi na nyumbu, ngamia na punda, nao wanyama wote walioko kwenye kambi za adui.

1614:16 2Fal 19:31; Za 22:29; 86:9; Isa 19:21; 60:6-9; Oba 1:21; Kut 23:16; Isa 66:23; 1Tim 6:15; Law 23:34; Neh 8:14; Hos 12:9Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda. 1714:17 2Nya 32:23; Yer 14:4; Amo 4:7; Isa 60:12Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao. 1814:18 Mwa 27:29Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. Bwana ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda. 1914:19 Ezr 3:4Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.

2014:20 Kut 39:30; Eze 46:20; Zek 9:15Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: Takatifu kwa Bwana, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya Bwana vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu. 2114:21 Yer 31:40; Rum 14:6-7; 1Kor 10:31; Neh 8:10; 11:1; Eze 44:9; Kol 3:17; Isa 35:8; Ufu 21:27; Efe 2:19Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote.

Nueva Versión Internacional

Zacarías 14:1-21

El reinado venidero del Señor

1»¡Jerusalén! Viene el día del Señor cuando tus despojos serán repartidos en tus propias calles. 2Movilizaré a todas las naciones para que peleen contra ti. Te conquistarán, saquearán tus casas y violarán a tus mujeres. La mitad de tus habitantes irá al exilio, pero el resto del pueblo se quedará contigo. 3Entonces saldrá el Señor y peleará contra aquellas naciones, como cuando pelea en el día de la batalla.

4»En aquel día sus pies estarán en el monte de los Olivos que se encuentra al este de Jerusalén. El monte de los Olivos se partirá en dos de este a oeste, formará un gran valle, con una mitad del monte desplazándose al norte y la otra mitad al sur. 5Ustedes huirán por el valle de mi monte, porque se extenderá hasta Asal. Huirán como huyeron del terremoto en los días de Uzías, rey de Judá. Entonces vendrá el Señor mi Dios acompañado de todos los santos.

6»En aquel día no habrá luz ni hará frío. 7Será un día excepcional que solo el Señor conoce: no tendrá día ni noche, pues, cuando llegue la noche, seguirá alumbrando la luz.

8»En aquel día fluirá agua viva desde Jerusalén, tanto en verano como en invierno. Una mitad correrá hacia el mar Muerto y la otra, hacia el mar Mediterráneo. 9El Señor será rey sobre toda la tierra. En aquel día el Señor será el único Dios y su nombre será el único nombre.

10»Desde Gueba hasta Rimón, al sur de Jerusalén, todo el país se volverá un desierto.14:10 un desierto. Lit. como el Arabá. Pero Jerusalén se levantará y permanecerá en su lugar, desde la puerta de Benjamín hasta el sitio de la puerta Primera, hasta la puerta del Ángulo, y desde la torre de Jananel hasta los lagares del rey. 11Jerusalén volverá a ser habitada, estará segura y nunca más será destruida.

12»Esta es la plaga con la que el Señor herirá a todos los pueblos que pelearon contra Jerusalén: se les pudrirá la carne en vida, se les pudrirán los ojos en las cuencas y se les pudrirá la lengua en la boca. 13En aquel día el Señor los llenará de pánico. Cada uno levantará la mano contra el otro; se atacarán entre sí. 14También Judá peleará en Jerusalén. Se recogerán las riquezas de todas las naciones vecinas y grandes cantidades de oro, plata y ropa. 15Una plaga semejante herirá también a caballos y mulos, camellos y asnos, y a todo animal que esté en aquellos campamentos.

16»Entonces los sobrevivientes de todas las naciones que atacaron a Jerusalén subirán año tras año para adorar al Rey, al Señor de los Ejércitos, y para celebrar la fiesta de las Enramadas. 17Si alguno de los pueblos de la tierra no sube a Jerusalén para adorar al Rey, al Señor de los Ejércitos, tampoco recibirá lluvia. 18Y si el pueblo egipcio no sube ni participa, tampoco recibirá lluvia. El Señor enviará una plaga para castigar a las naciones que no suban a celebrar la fiesta de las Enramadas. 19¡Así será castigado Egipto y todas las naciones que no suban a celebrar la fiesta de las Enramadas!

20»En aquel día los cascabeles de los caballos llevarán esta inscripción: consagrado al Señor. Las ollas de cocina del Templo del Señor serán como los tazones sagrados que están frente al altar del sacrificio. 21Toda olla de Jerusalén y de Judá será consagrada al Señor de los Ejércitos. Además, todo el que vaya a sacrificar tomará algunas de esas ollas y cocinará en ellas. En aquel día no habrá más mercaderes14:21 mercaderes. Alt. cananeos. en el Templo del Señor de los Ejércitos».