Zekaria 14 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zekaria 14:1-21

Bwana Yuaja Kutawala

114:1 Isa 13:6; 23:18; Yoe 1:15; Mal 4:1Siku ya Bwana inakuja ambayo nyara zilizotekwa kwenu zitagawanywa miongoni mwenu.

214:2 Isa 2:3; Zek 12:3; 13:8; Eze 5:8; Mwa 34:29; Mao 5:11; Isa 13:6; Yoe 3:2Nitayakusanya mataifa yote huko Yerusalemu kupigana dhidi yake, mji utatekwa, nyumba zitavamiwa na kuporwa na wanawake watanajisiwa. Nusu ya mji watakwenda uhamishoni, lakini watakaobaki hawataondolewa kutoka mjini.

314:3 Zek 9:14-15; 8:9; Isa 8:9Kisha Bwana atatoka na kupigana dhidi ya watu wa yale mataifa, kama apiganavyo siku ya vita. 414:4 Eze 11:23; Hes 16:31; Mdo 1:11-12; Yoe 3:12Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, mashariki mwa Yerusalemu, nao Mlima wa Mizeituni utagawanyika mara mbili kuanzia mashariki hadi magharibi, ukifanya bonde kubwa, nusu ya mlima ukisogea kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini. 514:5 Isa 29:6; 66:15-16; Mt 16:27; 25:31; Yud 14; Mt 24:30; Yoe 3:11Nanyi mtakimbia kupitia katika bonde hilo la mlima wangu kwa kuwa litaenea hadi Aseli. Mtakimbia kama mlivyokimbia tetemeko la ardhi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda. Kisha Bwana Mungu wangu atakuja na watakatifu wote pamoja naye.

614:6 Isa 13:10; Yer 4:23Siku hiyo hakutakuwepo nuru, baridi wala theluji. 714:7 Yer 30:7; Ufu 21:23-25; 22:5; Isa 13:10; 30:26Itakuwa siku ya kipekee, isiyo na mchana wala usiku, siku ijulikanayo na Bwana. Jioni inapofika nuru itakuwepo.

814:8 Eze 47:1-12; Yn 7:38; Ufu 22:1-2; Isa 30:25; Yoe 2:20; Mwa 8:22Siku hiyo, maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu, nusu kwenda kwenye bahari ya mashariki,14:8 Yaani Bahari ya Chumvi au Bahari Mfu. na nusu kwenda kwenye bahari ya magharibi14:8 Yaani Bahari ya Mediterania. wakati wa kiangazi na wakati wa masika.

914:9 Za 22:28; 47:7; Oba 1:21; Kum 6:4; Isa 45:24; Ufu 15:1; Hab 2:14; Efe 4:5-6; Za 2:8Bwana atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo atakuwepo Bwana mmoja na jina lake litakuwa jina pekee.

1014:10 1Fal 15:22; Yos 15:32; Isa 2:2; Yer 20:2; 30:18; Amo 9:11; Zek 12:6; 2Fal 14:13; Neh 3:1Nchi yote kuanzia Geba, kaskazini mwa Yuda, hadi Rimoni, kusini mwa Yerusalemu, itakuwa kama Araba.14:10 Araba maana yake Nchi tambarare. Lakini Yerusalemu utainuliwa juu na kubaki mahali pake, toka Lango la Benyamini hadi mahali pa Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni na kutoka Mnara wa Hananeli hadi kwenye mashinikizo ya divai ya mfalme. 1114:11 Zek 2:4; Za 48:8; Eze 34:25-28; Yer 31:40Utakaliwa na watu, kamwe hautaharibiwa tena, Yerusalemu utakaa salama.

1214:12 Isa 11:4; Law 26:16; Kum 28:22; Ay 18:13Hii ndiyo tauni ambayo Bwana atapiga nayo mataifa yote ambayo yalipigana dhidi ya Yerusalemu: Nyama ya miili yao itaoza wangali wamesimama kwa miguu yao, macho yao yataoza kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza vinywani mwao. 1314:13 Mwa 35:5; Amu 7:22; Zek 11:6; 1Sam 14:15Katika siku hiyo Bwana atawatia wanaume hofu kuu. Kila mwanaume atakamata mkono wa mwenzake nao watashambuliana. 1414:14 Zek 12:2; Isa 23:18Yuda pia atapigana katika Yerusalemu. Utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka Yerusalemu utakusanywa, wingi wa dhahabu, fedha na nguo. 15Tauni ya aina iyo hiyo itapiga farasi na nyumbu, ngamia na punda, nao wanyama wote walioko kwenye kambi za adui.

1614:16 2Fal 19:31; Za 22:29; 86:9; Isa 19:21; 60:6-9; Oba 1:21; Kut 23:16; Isa 66:23; 1Tim 6:15; Law 23:34; Neh 8:14; Hos 12:9Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda. 1714:17 2Nya 32:23; Yer 14:4; Amo 4:7; Isa 60:12Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao. 1814:18 Mwa 27:29Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. Bwana ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda. 1914:19 Ezr 3:4Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.

2014:20 Kut 39:30; Eze 46:20; Zek 9:15Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: Takatifu kwa Bwana, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya Bwana vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu. 2114:21 Yer 31:40; Rum 14:6-7; 1Kor 10:31; Neh 8:10; 11:1; Eze 44:9; Kol 3:17; Isa 35:8; Ufu 21:27; Efe 2:19Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

撒迦利亞書 14:1-21

耶和華的日子

1看啊,耶和華的日子快到了,那時你那裡的財物必被搶掠、瓜分。 2因為我必招聚萬國去攻打耶路撒冷。那時,城必失守,房屋必被洗劫,婦女必被玷污。半城的人必被擄去,剩下的人必留在城中,不會被剷除。 3那時,耶和華必出來與列國爭戰,像從前爭戰的日子一樣。 4到那天,祂的腳必踏在耶路撒冷東面的橄欖山上,這山必從東至西分成兩半,一半向北移,一半向南移,中間形成極大的山谷。 5你們要從我的這山谷逃跑,因為山谷必延伸到亞薩。你們必像猶大烏西雅年間的人躲避大地震一樣逃跑。我的上帝耶和華必帶著所有的聖者降臨。 6到那天,將沒有光、嚴寒和冰霜。 7那將是奇特的日子,沒有晝夜之分,晚上仍然有光,只有上帝知道那日何時來臨。

8到那天,必有活水從耶路撒冷湧出,一半流向死海,一半流向地中海,冬夏不變。 9耶和華必做普世的王。到那天,必唯祂獨尊,唯祂的名獨尊。 10迦巴直到耶路撒冷南邊的臨門,整個地區都要變為平原。從便雅憫門到舊門,再到角門,從哈楠業樓到王的榨酒池——耶路撒冷必仍然矗立在原處。 11城內必有人居住,不再遭毀滅的咒詛。耶路撒冷必安享太平。

12耶和華必降瘟疫給攻打耶路撒冷的列邦,使他們活著的時候皮肉已經腐爛,眼睛在眼眶中腐爛,舌頭在口中腐爛。 13到那天,耶和華必使他們慌亂不堪,彼此揪住,互相毆打。 14猶大也必在耶路撒冷爭戰,四圍列國的財物——大量的金銀和衣服必被收聚起來。 15同樣的瘟疫也必降在馬匹、騾子、駱駝、驢和營中的其他牲畜身上。

16前來攻打耶路撒冷的列國中的倖存者,必每年上來敬拜大君王——萬軍之耶和華,並且守住棚節。 17地上萬族中若有人不上耶路撒冷敬拜大君王——萬軍之耶和華,他們必沒有雨水。 18埃及人若不上來敬拜,也必沒有雨水,耶和華必使他們和不上來守住棚節的列國一樣遭受瘟疫。 19這將是埃及和不上來守住棚節的列國所得的懲罰。 20到那天,馬鈴上也必刻上「獻給耶和華」的字樣。耶和華殿內的鍋必像祭壇前的碗一樣聖潔。 21耶路撒冷猶大的鍋都是萬軍之耶和華的聖物,來獻祭的人都可以用這些鍋煮祭肉。到那天,萬軍之耶和華的殿中必再也沒有商人。