Zekaria 10 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zekaria 10:1-12

Bwana Ataitunza Yuda

110:1 Law 26:4; 1Fal 8:36; Za 104:13; 135:7; Ay 14:9; Yer 14:22; Yoe 2:32Mwombeni Bwana mvua wakati wa vuli;

ndiye Bwana atengenezaye mawingu ya tufani.

Huwapa watu manyunyu ya mvua,

pia mimea ya shambani kwa ajili ya kila mtu.

210:2 Eze 21:21; Isa 44:25; 40:19; Yer 23:16; Hes 27:17; Hos 3:4; Mt 9:36Sanamu huzungumza udanganyifu,

waaguzi huona maono ya uongo;

husimulia ndoto ambazo si za kweli,

wanatoa faraja batili.

Kwa hiyo watu wanatangatanga kama kondoo

walioonewa kwa kukosa mchungaji.

310:3 Isa 14:9; Yer 25:34; Eze 34:8-10; Kut 4:31; Rut 1:6; Sef 2:7; Lk 1:68; 1Pet 2:12“Hasira yangu inawaka dhidi ya wachungaji,

nami nitawaadhibu viongozi;

kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote

atalichunga kundi lake,

nyumba ya Yuda,

naye atawafanya kuwa kama farasi

mwenye kiburi akiwa vitani.

410:4 Za 118:22; Mdo 4:11; Isa 22:23; Zek 9:10Kutoka Yuda litatokea Jiwe la pembeni,

kutoka kwake vitatoka vigingi vya hema,

kutoka kwake utatoka upinde wa vita,

kutoka kwake atatoka kila mtawala.

510:5 2Sam 22:43; Mik 7:10; 5:8; Amo 2:15; Hag 2:22; Zek 12:4Kwa pamoja watakuwa kama mashujaa

wanaokanyaga barabara za matope

wakati wa vita.

Kwa sababu Bwana yu pamoja nao,

watapigana na kuwashinda wapanda farasi.

610:6 Eze 30:24; 36:37; Za 102:13; 34:17; Isa 37:19; 14:1; 58:9; 65:24; Zek 8:7-8; 13:9“Nitaiimarisha nyumba ya Yuda

na kuiokoa nyumba ya Yosefu.

Nitawarejesha kwa sababu

nina huruma juu yao.

Watakuwa kama watu ambao

sijawahi kuwakataa

kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wao,

nami nitawajibu.

710:7 Zek 9:15; 1Sam 2:1; Isa 60:5; Yoe 2:23Waefraimu watakuwa kama mashujaa,

mioyo yao itafurahi kana kwamba ni kwa divai.

Watoto wao wataona na kufurahi,

mioyo yao itashangilia katika Bwana.

810:8 Isa 5:26; Yer 33:22; Eze 36:11Nitawaashiria na kuwakusanya ndani.

Hakika nitawakomboa,

nao watakuwa wengi

kama walivyokuwa mwanzoni.

910:9 Isa 44:21; Eze 6:9Ijapokuwa niliwatawanya miongoni mwa mataifa,

hata hivyo wakiwa katika nchi za mbali

watanikumbuka mimi.

Wao na watoto wao watanusurika katika hatari

nao watarudi.

1010:10 Isa 11:11; 49:19; Zek 8:8; Yer 50:19; Rum 11:25; Kut 14:26-27Nitawarudisha kutoka Misri

na kuwakusanya toka Ashuru.

Nitawaleta katika nchi ya Gileadi na Lebanoni,

na hapo hapatakuwa na nafasi ya kuwatosha.

1110:11 Isa 19:5-7; 51:10; Sef 2:13; Eze 29:15; 30:13Watapita katika bahari ya mateso;

bahari iliyochafuka itatulizwa

na vilindi vyote vya Mto Naili vitakauka.

Kiburi cha Ashuru kitashushwa,

nayo fimbo ya utawala ya Misri itatoweka.

1210:12 Eze 30:24; Mik 4:5Nitawaimarisha katika Bwana,

na katika jina lake watatembea,”

asema Bwana.

Bibelen på hverdagsdansk

Zakariasʼ Bog 10:1-12

Herrens omsorg for sit folk

1Bed Herren om regn om foråret, for så vil regnen give vækst til markens planter. Det er jo Herren, der skaber tordenskyerne og sender regn. 2Husgudernes svar var falske, og sandsigernes syner var svindel. Alle deres drømme var kun tomme ord. Derfor fór I vild som får, der ingen hyrde har.

3„Jeg er vred på dem, som skulle være hyrder og ledere for mit folk,” siger Herren, den Almægtige. „Jeg vil velsigne min hjord, Judas folk. De skal ikke længere være som vildfarne får, men stærke som prægtige stridsheste. 4Jeg vil oprejse ledere iblandt dem, som skal give støtte, håb og sejr. 5Folket skal blive mægtige krigere for Herren og træde fjenderne ned i støvet under deres fødder. Herren er med dem i kampen, så deres fjender lider nederlag.

6Jeg gør Juda stærk og redder Israel. Jeg vil være barmhjertig imod dem og føre dem hjem. Det skal være, som om jeg aldrig havde forstødt dem, for jeg er Herren, deres Gud, og jeg hører deres råb om hjælp. 7Jeg gør dem stærke, som var de heltemodige krigere, og jeg gør dem glade, som havde de drukket vin. Deres børn skal se det og glæde sig, og alle skal juble over Herren. 8Jeg kalder dem hjem og samler dem sammen, for jeg har befriet dem. De skal igen blive talrige som før. 9Selv om jeg spredte dem blandt fjerne folkeslag, vil de aldrig glemme mig. Både de og deres børn skal vende hjem til deres eget land. 10Fra Egypten og Assyrien henter jeg dem og lader dem bosætte sig i Gilead og Libanon. Der vil ikke være plads til dem alle. 11Når jeg, Herren, fører mit folk gennem trængslens hav, lægger bølgerne sig. Nilens strømme tørrer ud, og Assyriens og Egyptens herredømme over mit folk får ende. 12Jeg gør mit folk stærkt, og hvor de end kommer frem, vil de vandre i min kraft, erklærer Herren.