Zekaria 1 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zekaria 1:1-21

Wito Wa Kumrudia Bwana

11:1 Ezr 4:24; 6:15; Mt 23:35; Lk 11:51; Neh 12:4Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:

21:2 2Nya 36:16Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani. 31:3 Yak 4:8; Mal 3:7; Ay 22:2; Yer 25:5; Mik 7:19; Lk 15:20Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. 41:4 2Nya 7:14; 24:19; 36:15; Zek 7:7; 2Fal 17:13; Za 78:8; 106:6; Yer 6:17; 17:23; 23:22; Eze 20:18; 33:4; Isa 1:16-17; Yer 3:12; Eze 33:11; Hos 14:1; Mit 3:8-9; Mdo 3:19Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana. 5Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele? 61:6 Isa 44:26; Kum 28:2; Dan 9:12; Hos 5:9; Yer 12:14-17; 39:16; 23:20; 44:17; Mao 2:17; Isa 55:1; Mao 1:18Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?”

“Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’ ”

Maono Ya Kwanza: Mtu Katikati Ya Miti Ya Mihadasi

7Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.

81:8 Ufu 6:4; Zek 6:2-7; Yos 5:13Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.

91:9 Zek 4:1-5; 5:5; Dan 7:16Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?”

Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”

101:10 Zek 6:5-8; Za 91:11; Ebr 1:14Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”

111:11 Isa 14:7; Mwa 16:7; Za 102:20Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”

121:12 Za 6:3; 40:11; Yer 40:5; 2Nya 36:21; Dan 9:2; Za 103:13; Ufu 6:10; Zek 7:5Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?” 131:13 Isa 35:4; Ay 15:11; Zek 4:1; Isa 40:1-2; Yer 29:10Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.

141:14 Isa 26:11; Yoe 2:18; Zek 8:2Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni, 151:15 Yer 48:11; 2Nya 28:9; Za 69:26; 123:3-4; Amo 1:11; Isa 47:6lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’

161:16 Zek 2:1-2; 8:3; Ay 38:5; Isa 12:1“Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

171:17 Isa 14:1; 40:1; 54:8-10; 61:4; Ezr 9:9; Za 51:18; Isa 51:3; Zek 3:2“Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’ ”

Maono Ya Pili: Pembe Nne Na Mafundi Wanne

18Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne! 191:19 Amo 6:13; Ezr 4:1; Hab 3:14Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?”

Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”

20Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne. 211:21 1Fal 22:11; Za 75:4, 10; Isa 54:16-17; Zek 12:9Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?”

Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

撒迦利亚书 1:1-21

呼唤人民归向耶和华

1大流士王二年八月,耶和华对易多的孙子、比利迦的儿子撒迦利亚先知说: 2“耶和华曾对你们的祖先大发怒气。 3因此,你要告诉百姓,万军之耶和华说,‘你们要归向我,我就回到你们那里。这是万军之耶和华说的。 4不要像你们的祖先一样。以前的先知曾呼唤他们要听从万军之耶和华的话,改邪归正,停止作恶,他们却置若罔闻,不予理会。这是耶和华说的。 5现在你们的祖先在哪里呢?那些先知能活到永远吗? 6然而,我吩咐我仆人——众先知的训言和律例岂不应验在你们祖先的头上了吗?后来他们悔改了,说,万军之耶和华按着我们的所作所为报应了我们,正如祂所言。’”

有关骑士的异象

7大流士王二年十一月,即细罢特月二十四日,耶和华的话传给了易多的孙子、比利迦的儿子撒迦利亚先知。 8我在夜间看到异象,见有人骑着一匹红马,站在谷中的番石榴树林间,后面有红马、棕马和白马骑士。 9我就问:“主啊,这是什么意思?”那位跟我说话的天使说:“我会告诉你这是什么意思。” 10站在番石榴树林间的那位对我说:“这些是耶和华派来巡视大地的。” 11其他骑士向站在番石榴树林间的那位耶和华的天使报告说:“我们已经巡视了大地,到处都安宁平静。”

12耶和华的天使说:“万军之耶和华啊,你向耶路撒冷犹大的城邑发怒已经七十年了,还要多久你才会怜悯他们呢?” 13耶和华用仁慈、安慰的话回答那位与我说话的天使。

14那位天使对我说:“你要宣告,万军之耶和华说,‘我对耶路撒冷,对锡安充满了火热的爱。 15我对安逸的列国充满愤怒,因为我只是对我的子民稍微不满,列国却大肆祸害他们。’ 16因此,耶和华说,‘我必怀着怜悯的心回到耶路撒冷,我的殿必在那里重建,必有准绳丈量耶路撒冷。这是万军之耶和华说的。’ 17你还要宣告,万军之耶和华说,‘我的城邑必再次繁荣昌盛,耶和华必再次安慰锡安,拣选耶路撒冷。’”

有关角和工匠的异象

18我又举目观看,见有四个角。 19于是,我问与我说话的天使:“这是什么?”他回答说:“这些是驱散犹大以色列耶路撒冷的角。” 20耶和华又让我看见四个工匠。 21于是我问:“他们来做什么?”他说:“这些角驱散了犹大,以致无人能抬头,但这些工匠是来威吓列国,并打掉他们用来攻击和驱散犹大的角。”