Zaburi 99 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 99:1-9

Zaburi 99

Mungu Mfalme Mkuu

199:1 1Nya 16:30, 31; Za 97:1; 2Sam 6:2; Kut 15:14; 25:22Bwana anatawala,

mataifa na yatetemeke;

anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi,

dunia na itikisike.

299:2 Za 48:1; 148:13; 2:6; 46:10; 97:9; 113:4; Kut 15:1Bwana ni mkuu katika Sayuni;

ametukuzwa juu ya mataifa yote.

399:3 Za 103:1; 33:21; 97:12; 76:1; 30:4; 106:47; 111:9; 145:21; 148:5; Kut 15:11Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa:

yeye ni mtakatifu!

499:4 1Fal 10:9; Za 98:9; Mwa 18:19, 25; Ufu 15:3; Ay 36:5; Kum 32:3, 4; Isa 11:3-5; Yer 23:5; Za 2:6Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki,

wewe umethibitisha adili;

katika Yakobo umefanya

yaliyo haki na sawa.

599:5 Isa 66:1; Kut 15:2; 1Nya 28:2; Za 132:7Mtukuzeni Bwana Mungu wetu,

na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake;

yeye ni mtakatifu.

699:6 Kut 24:6; 28:1; 1Sam 7:5; Za 4:3; 91:15Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,

Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake;

walimwita Bwana,

naye aliwajibu.

799:7 Kut 13:21; 19:9; Hes 11:25; 12:5Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu;

walizishika sheria zake na amri alizowapa.

899:8 Hes 14:20; Sef 3:7; Kum 9:20; Kut 22:27; Law 26:18Ee Bwana, wetu,

ndiwe uliyewajibu,

kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe,

ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.

9Mtukuzeni Bwana Mungu wetu,

mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu,

kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.

New International Version

Psalms 99:1-9

Psalm 99

1The Lord reigns,

let the nations tremble;

he sits enthroned between the cherubim,

let the earth shake.

2Great is the Lord in Zion;

he is exalted over all the nations.

3Let them praise your great and awesome name—

he is holy.

4The King is mighty, he loves justice—

you have established equity;

in Jacob you have done

what is just and right.

5Exalt the Lord our God

and worship at his footstool;

he is holy.

6Moses and Aaron were among his priests,

Samuel was among those who called on his name;

they called on the Lord

and he answered them.

7He spoke to them from the pillar of cloud;

they kept his statutes and the decrees he gave them.

8Lord our God,

you answered them;

you were to Israel a forgiving God,

though you punished their misdeeds.99:8 Or God, / an avenger of the wrongs done to them

9Exalt the Lord our God

and worship at his holy mountain,

for the Lord our God is holy.