Zaburi 99 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 99:1-9

Zaburi 99

Mungu Mfalme Mkuu

199:1 1Nya 16:30, 31; Za 97:1; 2Sam 6:2; Kut 15:14; 25:22Bwana anatawala,

mataifa na yatetemeke;

anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi,

dunia na itikisike.

299:2 Za 48:1; 148:13; 2:6; 46:10; 97:9; 113:4; Kut 15:1Bwana ni mkuu katika Sayuni;

ametukuzwa juu ya mataifa yote.

399:3 Za 103:1; 33:21; 97:12; 76:1; 30:4; 106:47; 111:9; 145:21; 148:5; Kut 15:11Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa:

yeye ni mtakatifu!

499:4 1Fal 10:9; Za 98:9; Mwa 18:19, 25; Ufu 15:3; Ay 36:5; Kum 32:3, 4; Isa 11:3-5; Yer 23:5; Za 2:6Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki,

wewe umethibitisha adili;

katika Yakobo umefanya

yaliyo haki na sawa.

599:5 Isa 66:1; Kut 15:2; 1Nya 28:2; Za 132:7Mtukuzeni Bwana Mungu wetu,

na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake;

yeye ni mtakatifu.

699:6 Kut 24:6; 28:1; 1Sam 7:5; Za 4:3; 91:15Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,

Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake;

walimwita Bwana,

naye aliwajibu.

799:7 Kut 13:21; 19:9; Hes 11:25; 12:5Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu;

walizishika sheria zake na amri alizowapa.

899:8 Hes 14:20; Sef 3:7; Kum 9:20; Kut 22:27; Law 26:18Ee Bwana, wetu,

ndiwe uliyewajibu,

kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe,

ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.

9Mtukuzeni Bwana Mungu wetu,

mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu,

kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Salmo 99:1-9

Salmo 99

1El Señor es rey:

que tiemblen las naciones.

Él tiene su trono entre querubines:

que se estremezca la tierra.

2Grande es el Señor en Sión,

¡excelso sobre todos los pueblos!

3Sea alabado su nombre grandioso e imponente:

¡él es santo!

4Rey poderoso, que amas la justicia:

tú has establecido la equidad

y has actuado en Jacob con justicia y rectitud.

5Exaltad al Señor nuestro Dios;

adoradlo ante el estrado de sus pies:

¡él es santo!

6Moisés y Aarón se contaban entre sus sacerdotes,

y Samuel, entre los que invocaron su nombre.

Invocaron al Señor, y él les respondió;

7les habló desde la columna de nube.

Cumplieron con sus estatutos,

con los decretos que él les entregó.

8Señor y Dios nuestro, tú les respondiste;

fuiste para ellos un Dios perdonador,

aun cuando castigaste sus rebeliones.

9Exaltad al Señor nuestro Dios;

adoradlo en su santo monte:

¡Santo es el Señor nuestro Dios!