Zaburi 89 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 89:1-52

Zaburi 89

Wimbo Wakati Wa Taabu Ya Kitaifa

Utenzi wa Ethani Mwezrahi.

189:1 Za 59:16; 36:5; 40:10Nitaimba juu ya upendo mkuu wa Bwana milele;

kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako

ujulikane kwa vizazi vyote.

289:2 Za 36:5Nitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele

na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni.

389:3 Eze 34:23; Hes 3:5; Ebr 7:21; Mdo 2:30Ulisema, “Nimefanya agano na mteule wangu,

nimemwapia mtumishi wangu Daudi,

489:4 2Sam 7:12-16; Lk 1:32, 33; Mt 1:1; Isa 9:6, 7; Rum 1:3; 1Fal 9:5; 8:16; Eze 37:24, 25; Za 132:11, 12‘Nitaimarisha uzao wako milele

na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’ ”

589:5 Za 19:1; 1:5Ee Bwana, mbingu zinayasifu maajabu yako,

uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu.

689:6 Mwa 1:26; Kut 9:14; Za 18:31; 113:5Kwa kuwa ni nani katika mbingu

anayeweza kulinganishwa na Bwana?

Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni

aliye kama Bwana?

789:7 Ay 5:1; Za 11:1; 47:2Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana,

anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.

889:8 Isa 6:3; Za 71:19Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote,

ni nani aliye kama wewe?

Ee Bwana, wewe ni mwenye nguvu,

na uaminifu wako unakuzunguka.

989:9 Za 65:7; Ay 38:11; Nah 1:4; Mt 8:26Wewe unatawala bahari yenye msukosuko;

wakati mawimbi yake yanapoinuka, wewe unayatuliza.

1089:10 Ay 9:13; Za 59:11; 68:1; 92:9; Isa 30:9Wewe ulimponda Rahabu89:10 Rahabu hapa ina maana jina la Misri kwa fumbo, yaani mwenye majivuno (lakini sio Rahabu wa Yos 2).

kama mmojawapo wa waliochinjwa;

kwa mkono wako wenye nguvu,

uliwatawanya adui zako.

1189:11 Kum 10:14; Za 24:1; 115:6; 1Nya 29:11; Mwa 1:1Mbingu ni zako, nayo nchi pia ni yako,

uliuwekea ulimwengu msingi

pamoja na vyote vilivyomo.

1289:12 Yos 19:22; Kum 3:8; 4:48; Za 98:8; Yos 12:1; Amu 4:6Uliumba kaskazini na kusini;

Tabori na Hermoni wanaliimbia jina lako kwa furaha.

1389:13 Yos 4:24Mkono wako umejaa uwezo;

mkono wako una nguvu,

mkono wako wa kuume umetukuzwa.

1489:14 Za 97:2; 85:10, 11Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako cha enzi;

upendo na uaminifu vinakutangulia.

1589:15 Za 1:1; 44:3; Hes 10:10Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe,

wanaotembea katika mwanga

wa uwepo wako, Ee Bwana.

1689:16 Za 30:4; 105:3Wanashangilia katika jina lako mchana kutwa,

wanafurahi katika haki yako.

1789:17 Za 18:1, 24; 75:10; 92:10; 112:9; 148:14Kwa kuwa wewe ni utukufu na nguvu yao,

kwa wema wako unatukuza pembe89:17 Pembe inawakilisha nguvu. yetu.

1889:18 Hos 13:10; Za 18:2; 47:9; Isa 16:5; 33:17, 22Naam, ngao yetu ni mali ya Bwana,

na mfalme wetu mali ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.

19Ulizungumza wakati fulani katika maono,

kwa watu wako waaminifu, ukasema:

“Nimeweka nguvu kwa shujaa,

nimemwinua kijana miongoni mwa watu.

2089:20 Mdo 13:22; Za 78:70; Kut 29:7; 1Fal 1:39; 1Sam 2:35; 2Sam 22:51Nimemwona Daudi, mtumishi wangu,

na nimemtia mafuta yangu matakatifu.

2189:21 Za 89:13; 18:35Kitanga changu kitamtegemeza,

hakika mkono wangu utamtia nguvu.

2289:22 Amu 3:15; 2Sam 7:10Hakuna adui atakayemtoza ushuru,

hakuna mtu mwovu atakayemwonea.

2389:23 Za 18:40; 2Sam 7:9Nitawaponda adui zake mbele zake

na kuwaangamiza watesi wake.

2489:24 2Sam 7:15; Za 61:7Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye,

kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.

2589:25 Za 72:8Nitauweka mkono wake juu ya bahari,

mkono wake wa kuume juu ya mito.

2689:26 Za 62:2; Yer 3:4; 2Sam 7:14; 22:47; 1Nya 22:10; Yn 5:17; Ebr 1:5Naye ataniita kwa sauti, ‘Wewe ni Baba yangu,

Mungu wangu, Mwamba na Mwokozi wangu.’

2789:27 Kol 1:18; Hes 24:7; Za 2:6, 7; Ufu 1:5; 19:16Nitamteua pia awe mzaliwa wangu wa kwanza,

aliyetukuka kuliko wafalme wote wa dunia.

2889:28 Za 89:33-34; Isa 55:3Nitadumisha upendo wangu kwake milele,

na agano langu naye litakuwa imara.

2989:29 Isa 9:7; Yer 33:17; Dan 7:14; Kum 11:21; Za 89:4, 36Nitaudumisha uzao wake milele,

kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.

3089:30 2Sam 7:14; Yer 9:13“Kama wanae wataacha amri yangu

na wasifuate sheria zangu,

31kama wakihalifu maagizo yangu

na kutoshika amri zangu,

3289:32 2Sam 7:14nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo,

uovu wao kwa kuwapiga,

3389:33 2Sam 7:15lakini sitauondoa upendo wangu kwake,

wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.

3489:34 Hes 23:19Mimi sitavunja agano langu

wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.

3589:35 Za 110:4; Ebr 6:13, 17; Amo 4:2; 8:7Mara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu,

nami sitamdanganya Daudi:

3689:36 Za 89:4; 2Sam 7:18; Lk 1:33; Yn 12:34kwamba uzao wake utaendelea milele,

na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua;

3789:37 Yer 31:35; 33:20, 21kitaimarishwa milele kama mwezi,

shahidi mwaminifu angani.”

3889:38 1Nya 28:9; Isa 22:5; Mao 2:2Lakini wewe umemkataa, umemdharau,

umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.

3989:39 Mao 5:16Umelikana agano lako na mtumishi wako,

na umeinajisi taji yake mavumbini.

4089:40 Za 80:12; Isa 22:5; Mao 2:2Umebomoa kuta zake zote,

na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu.

4189:41 Amu 2:14; Za 44:13Wote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake;

amekuwa dharau kwa jirani zake.

4289:42 Za 13:2; 80:6Umeutukuza mkono wa kuume wa adui zake,

umewafanya watesi wake wote washangilie.

4389:43 Za 44:10Umegeuza makali ya upanga wake,

na hukumpa msaada katika vita.

44Umeikomesha fahari yake,

na kukiangusha kiti chake cha enzi.

4589:45 Za 39:5; 44:15; 109:29Umezifupisha siku za ujana wake,

umemfunika kwa vazi la aibu.

4689:46 Za 79:5Hata lini, Ee Bwana? Utajificha milele?

Ghadhabu yako itawaka kama moto hata lini?

4789:47 Mwa 47:9; Ay 7:7; Za 39:5; 1Pet 1:24Kumbuka jinsi maisha yangu yanavyopita haraka.

Ni kwa ubatili kiasi gani umemuumba mwanadamu!

4889:48 Mwa 5:24; Za 22:29; Ebr 11:5Ni mtu gani awezaye kuishi na asione kifo,

au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi?89:48 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

4989:49 2Sam 7:12; Isa 55:13Ee Bwana, uko wapi upendo wako mkuu wa mwanzoni,

ambao katika uaminifu wako ulimwapia Daudi?

5089:50 Za 69:19Bwana kumbuka jinsi mtumishi wako amesimangwa,

jinsi ninavyovumilia moyoni mwangu dhihaka za mataifa yote,

5189:51 Za 74:10dhihaka ambazo kwazo adui zako

wamenisimanga, Ee Bwana,

ambazo kwazo wamesimanga

kila hatua ya mpakwa mafuta wako.

5289:52 Za 41:13; 72:19Msifuni Bwana milele!

Amen na Amen.

King James Version

Psalms 89:1-52

Maschil of Ethan the Ezrahite.

1I will sing of the mercies of the LORD for ever: with my mouth will I make known thy faithfulness to all generations.89.1 Maschil…: or, A Psalm for Ethan the Ezrahite, to give instruction89.1 to all…: Heb. to generation and generation

2For I have said, Mercy shall be built up for ever: thy faithfulness shalt thou establish in the very heavens.

3I have made a covenant with my chosen, I have sworn unto David my servant,

4Thy seed will I establish for ever, and build up thy throne to all generations. Selah.

5And the heavens shall praise thy wonders, O LORD: thy faithfulness also in the congregation of the saints.

6For who in the heaven can be compared unto the LORD? who among the sons of the mighty can be likened unto the LORD?

7God is greatly to be feared in the assembly of the saints, and to be had in reverence of all them that are about him.

8O LORD God of hosts, who is a strong LORD like unto thee? or to thy faithfulness round about thee?

9Thou rulest the raging of the sea: when the waves thereof arise, thou stillest them.

10Thou hast broken Rahab in pieces, as one that is slain; thou hast scattered thine enemies with thy strong arm.89.10 Rahab: or, Egypt89.10 thy…: Heb. the arm of thy strength

11The heavens are thine, the earth also is thine: as for the world and the fulness thereof, thou hast founded them.89.11 the fulness…: or, all it containeth

12The north and the south thou hast created them: Tabor and Hermon shall rejoice in thy name.

13Thou hast a mighty arm: strong is thy hand, and high is thy right hand.89.13 a…: Heb. an arm with might

14Justice and judgment are the habitation of thy throne: mercy and truth shall go before thy face.89.14 habitation: or, establishment

15Blessed is the people that know the joyful sound: they shall walk, O LORD, in the light of thy countenance.

16In thy name shall they rejoice all the day: and in thy righteousness shall they be exalted.

17For thou art the glory of their strength: and in thy favour our horn shall be exalted.

18For the LORD is our defence; and the Holy One of Israel is our king.89.18 the LORD…: or, our shield is of the LORD, and our king is of the Holy One of Israel

19Then thou spakest in vision to thy holy one, and saidst, I have laid help upon one that is mighty; I have exalted one chosen out of the people.

20I have found David my servant; with my holy oil have I anointed him:

21With whom my hand shall be established: mine arm also shall strengthen him.

22The enemy shall not exact upon him; nor the son of wickedness afflict him.

23And I will beat down his foes before his face, and plague them that hate him.

24But my faithfulness and my mercy shall be with him: and in my name shall his horn be exalted.

25I will set his hand also in the sea, and his right hand in the rivers.

26He shall cry unto me, Thou art my father, my God, and the rock of my salvation.

27Also I will make him my firstborn, higher than the kings of the earth.

28My mercy will I keep for him for evermore, and my covenant shall stand fast with him.

29His seed also will I make to endure for ever, and his throne as the days of heaven.

30If his children forsake my law, and walk not in my judgments;

31If they break my statutes, and keep not my commandments;89.31 break: Heb. profane

32Then will I visit their transgression with the rod, and their iniquity with stripes.

33Nevertheless my lovingkindness will I not utterly take from him, nor suffer my faithfulness to fail.89.33 will…: Heb. I will not make void from him89.33 to fail: Heb. to lie

34My covenant will I not break, nor alter the thing that is gone out of my lips.

35Once have I sworn by my holiness that I will not lie unto David.89.35 that…: Heb. if I lie

36His seed shall endure for ever, and his throne as the sun before me.

37It shall be established for ever as the moon, and as a faithful witness in heaven. Selah.

38But thou hast cast off and abhorred, thou hast been wroth with thine anointed.

39Thou hast made void the covenant of thy servant: thou hast profaned his crown by casting it to the ground.

40Thou hast broken down all his hedges; thou hast brought his strong holds to ruin.

41All that pass by the way spoil him: he is a reproach to his neighbours.

42Thou hast set up the right hand of his adversaries; thou hast made all his enemies to rejoice.

43Thou hast also turned the edge of his sword, and hast not made him to stand in the battle.

44Thou hast made his glory to cease, and cast his throne down to the ground.89.44 glory: Heb. brightness

45The days of his youth hast thou shortened: thou hast covered him with shame. Selah.

46How long, LORD? wilt thou hide thyself for ever? shall thy wrath burn like fire?

47Remember how short my time is: wherefore hast thou made all men in vain?

48What man is he that liveth, and shall not see death? shall he deliver his soul from the hand of the grave? Selah.

49Lord, where are thy former lovingkindnesses, which thou swarest unto David in thy truth?

50Remember, Lord, the reproach of thy servants; how I do bear in my bosom the reproach of all the mighty people;

51Wherewith thine enemies have reproached, O LORD; wherewith they have reproached the footsteps of thine anointed.

52Blessed be the LORD for evermore. Amen, and Amen.