Zaburi 89 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 89:1-52

Zaburi 89

Wimbo Wakati Wa Taabu Ya Kitaifa

Utenzi wa Ethani Mwezrahi.

189:1 Za 59:16; 36:5; 40:10Nitaimba juu ya upendo mkuu wa Bwana milele;

kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako

ujulikane kwa vizazi vyote.

289:2 Za 36:5Nitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele

na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni.

389:3 Eze 34:23; Hes 3:5; Ebr 7:21; Mdo 2:30Ulisema, “Nimefanya agano na mteule wangu,

nimemwapia mtumishi wangu Daudi,

489:4 2Sam 7:12-16; Lk 1:32, 33; Mt 1:1; Isa 9:6, 7; Rum 1:3; 1Fal 9:5; 8:16; Eze 37:24, 25; Za 132:11, 12‘Nitaimarisha uzao wako milele

na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’ ”

589:5 Za 19:1; 1:5Ee Bwana, mbingu zinayasifu maajabu yako,

uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu.

689:6 Mwa 1:26; Kut 9:14; Za 18:31; 113:5Kwa kuwa ni nani katika mbingu

anayeweza kulinganishwa na Bwana?

Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni

aliye kama Bwana?

789:7 Ay 5:1; Za 11:1; 47:2Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana,

anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.

889:8 Isa 6:3; Za 71:19Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote,

ni nani aliye kama wewe?

Ee Bwana, wewe ni mwenye nguvu,

na uaminifu wako unakuzunguka.

989:9 Za 65:7; Ay 38:11; Nah 1:4; Mt 8:26Wewe unatawala bahari yenye msukosuko;

wakati mawimbi yake yanapoinuka, wewe unayatuliza.

1089:10 Ay 9:13; Za 59:11; 68:1; 92:9; Isa 30:9Wewe ulimponda Rahabu89:10 Rahabu hapa ina maana jina la Misri kwa fumbo, yaani mwenye majivuno (lakini sio Rahabu wa Yos 2).

kama mmojawapo wa waliochinjwa;

kwa mkono wako wenye nguvu,

uliwatawanya adui zako.

1189:11 Kum 10:14; Za 24:1; 115:6; 1Nya 29:11; Mwa 1:1Mbingu ni zako, nayo nchi pia ni yako,

uliuwekea ulimwengu msingi

pamoja na vyote vilivyomo.

1289:12 Yos 19:22; Kum 3:8; 4:48; Za 98:8; Yos 12:1; Amu 4:6Uliumba kaskazini na kusini;

Tabori na Hermoni wanaliimbia jina lako kwa furaha.

1389:13 Yos 4:24Mkono wako umejaa uwezo;

mkono wako una nguvu,

mkono wako wa kuume umetukuzwa.

1489:14 Za 97:2; 85:10, 11Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako cha enzi;

upendo na uaminifu vinakutangulia.

1589:15 Za 1:1; 44:3; Hes 10:10Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe,

wanaotembea katika mwanga

wa uwepo wako, Ee Bwana.

1689:16 Za 30:4; 105:3Wanashangilia katika jina lako mchana kutwa,

wanafurahi katika haki yako.

1789:17 Za 18:1, 24; 75:10; 92:10; 112:9; 148:14Kwa kuwa wewe ni utukufu na nguvu yao,

kwa wema wako unatukuza pembe89:17 Pembe inawakilisha nguvu. yetu.

1889:18 Hos 13:10; Za 18:2; 47:9; Isa 16:5; 33:17, 22Naam, ngao yetu ni mali ya Bwana,

na mfalme wetu mali ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.

19Ulizungumza wakati fulani katika maono,

kwa watu wako waaminifu, ukasema:

“Nimeweka nguvu kwa shujaa,

nimemwinua kijana miongoni mwa watu.

2089:20 Mdo 13:22; Za 78:70; Kut 29:7; 1Fal 1:39; 1Sam 2:35; 2Sam 22:51Nimemwona Daudi, mtumishi wangu,

na nimemtia mafuta yangu matakatifu.

2189:21 Za 89:13; 18:35Kitanga changu kitamtegemeza,

hakika mkono wangu utamtia nguvu.

2289:22 Amu 3:15; 2Sam 7:10Hakuna adui atakayemtoza ushuru,

hakuna mtu mwovu atakayemwonea.

2389:23 Za 18:40; 2Sam 7:9Nitawaponda adui zake mbele zake

na kuwaangamiza watesi wake.

2489:24 2Sam 7:15; Za 61:7Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye,

kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.

2589:25 Za 72:8Nitauweka mkono wake juu ya bahari,

mkono wake wa kuume juu ya mito.

2689:26 Za 62:2; Yer 3:4; 2Sam 7:14; 22:47; 1Nya 22:10; Yn 5:17; Ebr 1:5Naye ataniita kwa sauti, ‘Wewe ni Baba yangu,

Mungu wangu, Mwamba na Mwokozi wangu.’

2789:27 Kol 1:18; Hes 24:7; Za 2:6, 7; Ufu 1:5; 19:16Nitamteua pia awe mzaliwa wangu wa kwanza,

aliyetukuka kuliko wafalme wote wa dunia.

2889:28 Za 89:33-34; Isa 55:3Nitadumisha upendo wangu kwake milele,

na agano langu naye litakuwa imara.

2989:29 Isa 9:7; Yer 33:17; Dan 7:14; Kum 11:21; Za 89:4, 36Nitaudumisha uzao wake milele,

kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.

3089:30 2Sam 7:14; Yer 9:13“Kama wanae wataacha amri yangu

na wasifuate sheria zangu,

31kama wakihalifu maagizo yangu

na kutoshika amri zangu,

3289:32 2Sam 7:14nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo,

uovu wao kwa kuwapiga,

3389:33 2Sam 7:15lakini sitauondoa upendo wangu kwake,

wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.

3489:34 Hes 23:19Mimi sitavunja agano langu

wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.

3589:35 Za 110:4; Ebr 6:13, 17; Amo 4:2; 8:7Mara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu,

nami sitamdanganya Daudi:

3689:36 Za 89:4; 2Sam 7:18; Lk 1:33; Yn 12:34kwamba uzao wake utaendelea milele,

na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua;

3789:37 Yer 31:35; 33:20, 21kitaimarishwa milele kama mwezi,

shahidi mwaminifu angani.”

3889:38 1Nya 28:9; Isa 22:5; Mao 2:2Lakini wewe umemkataa, umemdharau,

umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.

3989:39 Mao 5:16Umelikana agano lako na mtumishi wako,

na umeinajisi taji yake mavumbini.

4089:40 Za 80:12; Isa 22:5; Mao 2:2Umebomoa kuta zake zote,

na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu.

4189:41 Amu 2:14; Za 44:13Wote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake;

amekuwa dharau kwa jirani zake.

4289:42 Za 13:2; 80:6Umeutukuza mkono wa kuume wa adui zake,

umewafanya watesi wake wote washangilie.

4389:43 Za 44:10Umegeuza makali ya upanga wake,

na hukumpa msaada katika vita.

44Umeikomesha fahari yake,

na kukiangusha kiti chake cha enzi.

4589:45 Za 39:5; 44:15; 109:29Umezifupisha siku za ujana wake,

umemfunika kwa vazi la aibu.

4689:46 Za 79:5Hata lini, Ee Bwana? Utajificha milele?

Ghadhabu yako itawaka kama moto hata lini?

4789:47 Mwa 47:9; Ay 7:7; Za 39:5; 1Pet 1:24Kumbuka jinsi maisha yangu yanavyopita haraka.

Ni kwa ubatili kiasi gani umemuumba mwanadamu!

4889:48 Mwa 5:24; Za 22:29; Ebr 11:5Ni mtu gani awezaye kuishi na asione kifo,

au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi?89:48 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

4989:49 2Sam 7:12; Isa 55:13Ee Bwana, uko wapi upendo wako mkuu wa mwanzoni,

ambao katika uaminifu wako ulimwapia Daudi?

5089:50 Za 69:19Bwana kumbuka jinsi mtumishi wako amesimangwa,

jinsi ninavyovumilia moyoni mwangu dhihaka za mataifa yote,

5189:51 Za 74:10dhihaka ambazo kwazo adui zako

wamenisimanga, Ee Bwana,

ambazo kwazo wamesimanga

kila hatua ya mpakwa mafuta wako.

5289:52 Za 41:13; 72:19Msifuni Bwana milele!

Amen na Amen.

Het Boek

Psalmen 89:1-53

1Een leerzaam gedicht van de Ezrahiet Ethan.

2Ik wil alleen nog maar zingen

van de goedheid en genade van de Here,

van alles wat Hij voor mij heeft gedaan.

Van generatie op generatie

zal ik getuigen van uw trouw.

3Ik zeg dan:

uw goedheid en liefde gelden eeuwig,

tot in de hemel blijkt hoe trouw U bent.

4De Here zegt:

Ik heb een verbond gesloten

met de man die Ik heb uitgekozen,

dat heb Ik gezworen aan mijn dienaar David.

5Ik zei tegen hem:

Ik zal uw nageslacht blijven zegenen,

van generatie op generatie

zullen uw kinderen op de troon blijven.

6Here, daarom wordt uw grote macht

tot in de hemel geprezen.

Alle gelovigen loven U om uw trouw.

7Kan in de hemel iemand

zich meten met de Here?

Is er op aarde

een god als onze Here?

8God dwingt ontzag en respect af

van de heilige engelen die Hem omringen.

9Here, God van de hemelse legers,

wie is zo groot en machtig als U?

Uw trouw omgeeft U.

10U beheerst de woede van de zee,

als de golven hoog oprijzen, brengt U ze tot rust.

11U hebt Egypte vernietigd

en al uw vijanden door uw kracht verspreid.

12De hemel is van U

en ook de aarde behoort U toe.

U hebt de wereld en alles wat erop leeft, geschapen.

13Van noord tot zuid hebt U alles gemaakt.

De bergen juichen U toe.

14Uw arm is machtig en uw hand is sterk.

Uw rechterhand is de hoogste op aarde.

15Alles wat U doet, is recht en rechtvaardig.

Goedheid, liefde en trouw

zijn alleen op U van toepassing.

16Gelukkig is het volk dat U eert, Here,

zij gaan hun weg met U, in uw licht.

17De hele dag prijzen zij uw naam

en dankzij uw rechtvaardigheid staan zij sterk.

18Want U bent het kenmerk van hun kracht,

door uw liefde en goedkeuring ontvangen wij een hoge positie.

19De Here beschermt ons

en de Heilige God van Israël is onze Koning.

20In het verleden hebt U tegen uw volgelingen gezegd:

‘Ik heb mijn hulp toegezegd aan een dapper man,

één man uit uw volk koos Ik speciaal uit.

21Ik vond mijn dienaar David

en heb hem met gewijde olie gezalfd.

22Mijn hand zal hem ondersteunen

en mijn arm zal hem sterk maken.

23De vijand zal hem niet in zijn macht krijgen

en geen misdadiger zal hem kwaad kunnen doen.

24Integendeel, Ik zal zijn tegenstanders voor hem vernietigen.

Wie hem haten, zullen Mij tegenkomen.

25Maar al mijn trouw en liefde zijn voor hem.

Dankzij Mij bekleedt hij een hoge positie.

26Ik geef hem zelfs gezag over zeeën en rivieren.

27Hij zal Mij zijn Vader noemen.

Ik zal zijn God zijn

en de rots waar hij zijn redding vindt.

28Ik zal hem behandelen als een oudste zoon,

als een van de hoogste koningen op aarde.

29Mijn goedheid en liefde zijn blijvend voor hem,

mijn verbond met hem kan niet meer worden verbroken.

30Zijn nageslacht zal altijd blijven bestaan

en zijn troon is onaantastbaar.

31Als zijn zonen mijn wetten negeren

en niet meer leven volgens mijn leefregels,

32als zij mijn voorschriften ontwijden

en mijn geboden niet meer houden,

33zal Ik hen straffen en allerlei plagen sturen.

34Maar mijn goedheid en liefde voor hem

blijven onveranderd, Ik blijf hem trouw.

35En ook mijn verbond met hem

blijf Ik trouw, dat is Mij heilig.

Wat Ik heb beloofd, zal Ik doen.

36Ik heb het immers eens bij Mij Zelf gezworen!

Ik kan David niet in de steek laten.

37Zijn nageslacht zal altijd voortleven

en zijn troon is onwankelbaar, net als de zon.

38Net als de maan zal hij er altijd zijn,

want Hij die vanuit de hemel getuigt, is trouw.’

39Maar toch hebt U uw uitverkorene

van U weggedaan en hem verworpen.

U bent boos op hem geworden.

40U hebt uw verbond met uw dienaar vernietigd

en hem de kroon van het hoofd gestoten.

41Zijn muren hebt U afgebroken

en zijn sterke burchten tot puin gemaakt.

42Mensen die langskwamen

hebben zijn bezittingen geplunderd.

Zijn buren dreven de spot met hem.

43Zijn tegenstanders bleken sterker

en zijn vijanden overwonnen hem.

44Ook zijn zwaard gaf hem geen overwinning

en hij moest zich in de oorlogen gewonnen geven.

45Er was geen eer meer voor hem over

en zijn troon hebt U omver geworpen.

46Hij werd vroeg oud en werd met schande overladen.

47Moet dit nog lang duren, Here?

Blijft U Zich voor mij verbergen?

Blijft uw toorn branden als het heetste vuur?

48Denk er alstublieft aan

dat ik maar een vergankelijk mens ben.

U hebt de mensen Zelf geschapen,

dus U weet hoe kort zij leven.

49Er is immers geen mens die niet zal sterven?

Niemand kan toch ontkomen aan het dodenrijk?

50Waar zijn nu de blijken van uw genade, Here?

U hebt die eens aan ons toegezegd,

zelfs met een eed aan David gezworen.

51Kijk toch, Here, hoe uw dienaren worden bespot

en hoe alle volken ons uitlachen.

52Hoe ook uw tegenstanders de spot met ons drijven, Here.

Zij drijven de spot met hem die door U tot koning is gezalfd!

53Alle lof en eer is voor de Here, tot in eeuwigheid.

Laat ieder die dit hoort daarmee instemmen.

Amen.