Zaburi 89 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 89:1-52

Zaburi 89

Wimbo Wakati Wa Taabu Ya Kitaifa

Utenzi wa Ethani Mwezrahi.

189:1 Za 59:16; 36:5; 40:10Nitaimba juu ya upendo mkuu wa Bwana milele;

kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako

ujulikane kwa vizazi vyote.

289:2 Za 36:5Nitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele

na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni.

389:3 Eze 34:23; Hes 3:5; Ebr 7:21; Mdo 2:30Ulisema, “Nimefanya agano na mteule wangu,

nimemwapia mtumishi wangu Daudi,

489:4 2Sam 7:12-16; Lk 1:32, 33; Mt 1:1; Isa 9:6, 7; Rum 1:3; 1Fal 9:5; 8:16; Eze 37:24, 25; Za 132:11, 12‘Nitaimarisha uzao wako milele

na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’ ”

589:5 Za 19:1; 1:5Ee Bwana, mbingu zinayasifu maajabu yako,

uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu.

689:6 Mwa 1:26; Kut 9:14; Za 18:31; 113:5Kwa kuwa ni nani katika mbingu

anayeweza kulinganishwa na Bwana?

Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni

aliye kama Bwana?

789:7 Ay 5:1; Za 11:1; 47:2Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana,

anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.

889:8 Isa 6:3; Za 71:19Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote,

ni nani aliye kama wewe?

Ee Bwana, wewe ni mwenye nguvu,

na uaminifu wako unakuzunguka.

989:9 Za 65:7; Ay 38:11; Nah 1:4; Mt 8:26Wewe unatawala bahari yenye msukosuko;

wakati mawimbi yake yanapoinuka, wewe unayatuliza.

1089:10 Ay 9:13; Za 59:11; 68:1; 92:9; Isa 30:9Wewe ulimponda Rahabu89:10 Rahabu hapa ina maana jina la Misri kwa fumbo, yaani mwenye majivuno (lakini sio Rahabu wa Yos 2).

kama mmojawapo wa waliochinjwa;

kwa mkono wako wenye nguvu,

uliwatawanya adui zako.

1189:11 Kum 10:14; Za 24:1; 115:6; 1Nya 29:11; Mwa 1:1Mbingu ni zako, nayo nchi pia ni yako,

uliuwekea ulimwengu msingi

pamoja na vyote vilivyomo.

1289:12 Yos 19:22; Kum 3:8; 4:48; Za 98:8; Yos 12:1; Amu 4:6Uliumba kaskazini na kusini;

Tabori na Hermoni wanaliimbia jina lako kwa furaha.

1389:13 Yos 4:24Mkono wako umejaa uwezo;

mkono wako una nguvu,

mkono wako wa kuume umetukuzwa.

1489:14 Za 97:2; 85:10, 11Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako cha enzi;

upendo na uaminifu vinakutangulia.

1589:15 Za 1:1; 44:3; Hes 10:10Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe,

wanaotembea katika mwanga

wa uwepo wako, Ee Bwana.

1689:16 Za 30:4; 105:3Wanashangilia katika jina lako mchana kutwa,

wanafurahi katika haki yako.

1789:17 Za 18:1, 24; 75:10; 92:10; 112:9; 148:14Kwa kuwa wewe ni utukufu na nguvu yao,

kwa wema wako unatukuza pembe89:17 Pembe inawakilisha nguvu. yetu.

1889:18 Hos 13:10; Za 18:2; 47:9; Isa 16:5; 33:17, 22Naam, ngao yetu ni mali ya Bwana,

na mfalme wetu mali ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.

19Ulizungumza wakati fulani katika maono,

kwa watu wako waaminifu, ukasema:

“Nimeweka nguvu kwa shujaa,

nimemwinua kijana miongoni mwa watu.

2089:20 Mdo 13:22; Za 78:70; Kut 29:7; 1Fal 1:39; 1Sam 2:35; 2Sam 22:51Nimemwona Daudi, mtumishi wangu,

na nimemtia mafuta yangu matakatifu.

2189:21 Za 89:13; 18:35Kitanga changu kitamtegemeza,

hakika mkono wangu utamtia nguvu.

2289:22 Amu 3:15; 2Sam 7:10Hakuna adui atakayemtoza ushuru,

hakuna mtu mwovu atakayemwonea.

2389:23 Za 18:40; 2Sam 7:9Nitawaponda adui zake mbele zake

na kuwaangamiza watesi wake.

2489:24 2Sam 7:15; Za 61:7Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye,

kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.

2589:25 Za 72:8Nitauweka mkono wake juu ya bahari,

mkono wake wa kuume juu ya mito.

2689:26 Za 62:2; Yer 3:4; 2Sam 7:14; 22:47; 1Nya 22:10; Yn 5:17; Ebr 1:5Naye ataniita kwa sauti, ‘Wewe ni Baba yangu,

Mungu wangu, Mwamba na Mwokozi wangu.’

2789:27 Kol 1:18; Hes 24:7; Za 2:6, 7; Ufu 1:5; 19:16Nitamteua pia awe mzaliwa wangu wa kwanza,

aliyetukuka kuliko wafalme wote wa dunia.

2889:28 Za 89:33-34; Isa 55:3Nitadumisha upendo wangu kwake milele,

na agano langu naye litakuwa imara.

2989:29 Isa 9:7; Yer 33:17; Dan 7:14; Kum 11:21; Za 89:4, 36Nitaudumisha uzao wake milele,

kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.

3089:30 2Sam 7:14; Yer 9:13“Kama wanae wataacha amri yangu

na wasifuate sheria zangu,

31kama wakihalifu maagizo yangu

na kutoshika amri zangu,

3289:32 2Sam 7:14nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo,

uovu wao kwa kuwapiga,

3389:33 2Sam 7:15lakini sitauondoa upendo wangu kwake,

wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.

3489:34 Hes 23:19Mimi sitavunja agano langu

wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.

3589:35 Za 110:4; Ebr 6:13, 17; Amo 4:2; 8:7Mara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu,

nami sitamdanganya Daudi:

3689:36 Za 89:4; 2Sam 7:18; Lk 1:33; Yn 12:34kwamba uzao wake utaendelea milele,

na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua;

3789:37 Yer 31:35; 33:20, 21kitaimarishwa milele kama mwezi,

shahidi mwaminifu angani.”

3889:38 1Nya 28:9; Isa 22:5; Mao 2:2Lakini wewe umemkataa, umemdharau,

umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.

3989:39 Mao 5:16Umelikana agano lako na mtumishi wako,

na umeinajisi taji yake mavumbini.

4089:40 Za 80:12; Isa 22:5; Mao 2:2Umebomoa kuta zake zote,

na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu.

4189:41 Amu 2:14; Za 44:13Wote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake;

amekuwa dharau kwa jirani zake.

4289:42 Za 13:2; 80:6Umeutukuza mkono wa kuume wa adui zake,

umewafanya watesi wake wote washangilie.

4389:43 Za 44:10Umegeuza makali ya upanga wake,

na hukumpa msaada katika vita.

44Umeikomesha fahari yake,

na kukiangusha kiti chake cha enzi.

4589:45 Za 39:5; 44:15; 109:29Umezifupisha siku za ujana wake,

umemfunika kwa vazi la aibu.

4689:46 Za 79:5Hata lini, Ee Bwana? Utajificha milele?

Ghadhabu yako itawaka kama moto hata lini?

4789:47 Mwa 47:9; Ay 7:7; Za 39:5; 1Pet 1:24Kumbuka jinsi maisha yangu yanavyopita haraka.

Ni kwa ubatili kiasi gani umemuumba mwanadamu!

4889:48 Mwa 5:24; Za 22:29; Ebr 11:5Ni mtu gani awezaye kuishi na asione kifo,

au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi?89:48 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

4989:49 2Sam 7:12; Isa 55:13Ee Bwana, uko wapi upendo wako mkuu wa mwanzoni,

ambao katika uaminifu wako ulimwapia Daudi?

5089:50 Za 69:19Bwana kumbuka jinsi mtumishi wako amesimangwa,

jinsi ninavyovumilia moyoni mwangu dhihaka za mataifa yote,

5189:51 Za 74:10dhihaka ambazo kwazo adui zako

wamenisimanga, Ee Bwana,

ambazo kwazo wamesimanga

kila hatua ya mpakwa mafuta wako.

5289:52 Za 41:13; 72:19Msifuni Bwana milele!

Amen na Amen.

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Забур 89:1-17

Четвёртая книга

Песнь 89

1Молитва пророка Мусо.

2Владыка, Ты был для нас прибежищем

из поколения в поколение.

3Прежде чем родились горы

и Ты образовал землю и весь мир,

от века и до века Ты – Бог.

4Ты возвращаешь человека в тление

и говоришь: «Вернитесь, смертные».

5Тысяча лет в глазах Твоих, как день вчерашний, что минул,

как несколько часов в ночи.

6Как наводнением уносишь людей;

они проходят, как сон.

Они – как трава, что утром взошла:

утром она цветёт и зеленеет,

а вечером вянет и засыхает.

7Мы исчезаем от Твоего гнева,

мы в смятении от Твоей ярости.

8Ты поставил наши беззакония перед Собою

и наши тайные грехи – перед лицом Своим.

9Наши дни проходят в Твоём гневе;

мы завершаем свои годы со стоном.

10Дней нашей жизни – лет семьдесят,

а для тех, кто покрепче, – лет восемьдесят,

и большая часть их – труд и скорбь;

быстро они проходят, и мы исчезаем.

11Кто познал силу Твоего гнева?

Ярость Твоя столь же велика,

сколь велик страх перед Тобой.

12Научи нас вести счёт нашим дням,

чтобы мы обрели сердце мудрое.

13Возвратись, Вечный! Как долго ещё будешь гневаться?

Сжалься над Своими рабами!

14Насыщай нас по утрам милостью Своей,

чтобы мы радовались и веселились все наши дни.

15Возвесели нас за дни, когда Ты наказывал нас,

и за годы, в которые мы испытывали бедствие.

16Да откроется взору рабов Твоих дело Твоё,

и слава Твоя – их детям.

17И да пребудет на нас милость Владыки, нашего Бога.

Укрепи наше дело,

укрепи для нас дело наших рук.