Zaburi 86 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 86:1-17

Zaburi 86

Kuomba Msaada

Maombi ya Daudi.

186:1 Za 17:6Ee Bwana, sikia na unijibu,

kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.

286:2 Za 25:2; 31:14Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako,

wewe ni Mungu wangu,

mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.

386:3 Za 4:1; 9:13; 57:1; 88:9Ee Bwana, nihurumie mimi,

kwa maana ninakuita mchana kutwa.

486:4 Za 46:5; 143:8Mpe mtumishi wako furaha,

kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana,

ninainua nafsi yangu.

586:5 Yoe 2:13; Yon 4:2; Neh 9:17; Za 103:8; 145:8; 130:7, 8; Kut 34:6Ee Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe,

umejaa upendo kwa wote wakuitao.

686:6 Za 5:2; 17:1Ee Bwana, sikia maombi yangu,

sikiliza kilio changu unihurumie.

786:7 Za 3:4; 4:3; 27:5; 50:15; 94:13; 80:18; 91:15; Isa 30:19; 58:9; 65:24; Ay 22:27; Zek 13:9; Hab 3:16Katika siku ya shida yangu nitakuita,

kwa maana wewe utanijibu.

886:8 Ay 21:22; Za 18:31; 1Sam 2:2; Kut 8:10; 15:11; Kum 3:24; 2Sam 7:22Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe,

hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.

986:9 Za 65:2; 66:4; Isa 19:21; 27:13; 49:7; Zek 8:20-22; 14:6; Ufu 15:4; Isa 43:7; 44:23; Za 95:6, 7Ee Bwana, mataifa yote uliyoyafanya

yatakuja na kuabudu mbele zako;

wataliletea utukufu jina lako.

1086:10 2Sam 7:22; Kut 3:20; Kum 6:4; Za 48:1; 71:17; 72:18; 1Kor 8:4; Isa 37:16; 43:10; Mk 12:29; Efe 4:6Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu;

wewe peke yako ndiwe Mungu.

1186:11 Kut 33:13; 1Sam 12:23; Za 25:5; Eze 11:19; Za 26:3; Kum 6:24; Yer 24:7; 32:39; 1Kor 7:35Ee Bwana, nifundishe njia yako,

nami nitakwenda katika kweli yako;

nipe moyo usiositasita,

ili niweze kulicha jina lako.

1286:12 Za 9:1Ee Bwana wangu, nitakusifu kwa moyo wote;

nitaliadhimisha jina lako milele.

1386:13 Za 56:13; 116:8; 34:4; 49:15; 16:10Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu;

umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi.86:13 Yaani Kuzimu.

1486:14 Za 54:3Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia;

kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu:

watu wasiokuheshimu wewe.

1586:15 Za 116:5; 103:8; 111:4; 145:8; 51:1; Hes 14:18; Za 86:5; Kut 34:6; Yoe 2:13; Neh 9:17Lakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu wa huruma na neema,

si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.

1686:16 Za 6:4; 9:13; 18:1; 116:16Nigeukie na unihurumie;

mpe mtumishi wako nguvu zako,

mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.86:16 Au: mwokoe mwanao mwaminifu.

1786:17 Kut 3:12; Mt 24:3; Yn 2:11Nipe ishara ya wema wako,

ili adui zangu waione nao waaibishwe,

kwa kuwa wewe, Ee Bwana,

umenisaidia na kunifariji.

Ketab El Hayat

مزمور 86:1-17

الْمَزْمُورُ السَّادِسُ وَالثَّمَانُونَ

صَلاةٌ رَفَعَهَا دَاوُدُ

1أَرْهِفْ يَا رَبُّ إِلَيَّ أُذُنَكَ، اسْتَجِبْ لِي، فَإِنِّي مِسْكِينٌ وَبَائِسٌ. 2احْفَظْ نَفْسِي فَإِنِّي تَقِيٌّ يَا إِلَهِي، خَلِّصْ أَنْتَ عَبْدَكَ الْوَاثِقَ بِكَ. 3ارْحَمْنِي يَا رَبُّ فَإِنِّي بِكَ أَسْتَغِيثُ طَوَالَ النَّهَارِ. 4فَرِّحْ نَفْسَ عَبْدِكَ، فَإِنِّي إِلَيْكَ أَيُّهَا السَّيِّدُ أَرْفَعُ نَفْسِي. 5لأَنَّكَ أَنْتَ يَا رَبُّ طَيِّبٌ وَغَفُورٌ، وَكَثِيرُ الرَّحْمَةِ لِجَمِيعِ الَّذِينَ يَدْعُونَكَ.

6يَا رَبُّ أَصْغِ إِلَى صَلاتِي وَاسْتَمِعْ إِلَى صَوْتِ تَضَرُّعَاتِي. 7فِي يَوْمِ ضِيقِي أَدْعُوكَ لأَنَّكَ تَسْتَجِيبُنِي. 8لَا نَظِيرَ لَكَ بَيْنَ الآلِهَةِ يَا رَبُّ، وَلَيْسَ مَنْ يَعْمَلُ كَأَعْمَالِكَ. 9تُقْبِلُ جَمِيعُ الأُمَمِ الَّتِي صَنَعْتَهَا لِتَسْجُدَ أَمَامَكَ يَا رَبُّ وَتُمَجِّدَ اسْمَكَ. 10فَإِنَّكَ عَظِيمٌ وَصَانِعٌ عَجَائِبَ. أَنْتَ اللهُ وَحْدَكَ.

11يَا رَبُّ عَلِّمْنِي طَرِيقَكَ فَأَسْلُكَ بِمُوجِبِ حَقِّكَ. وَحِّدْ قَلْبِي لِيَخَافَ اسْمَكَ. 12أَحْمَدُكَ يَا رَبُّ إِلَهِي بِكَامِلِ قَلْبِي، وَأُمَجِّدُ اسْمَكَ إِلَى الأَبَدِ. 13لأَنَّ رَحْمَتَكَ عَظِيمَةٌ نَحْوِي، وَقَدْ نَجَّيْتَ نَفْسِي مِنَ الْهَاوِيَةِ السُّفْلَى.

14يَا اللهُ قَدْ ثَارَ عَلَيَّ الْمُتَكَبِّرُونَ، وَجَمَاعَةُ الظَّالِمِينَ يَطْلُبُونَ قَتْلِي، غَيْرَ عَابِئِينَ بِكَ. 15إِنَّمَا أَنْتَ يَا رَبُّ إِلَهٌ رَحِيمٌ وَرَؤُوفٌ وَبَطِيءُ الْغَضَبِ وَوَافِرُ الرَّحْمَةِ وَالْحَقِّ. 16الْتَفِتْ إِلَيَّ وَارْحَمْنِي. أَعْطِنِي أَنَا عَبْدَكَ قُوَّتَكَ، وَخَلِّصْنِي أَنَا ابْنَ أَمَتِكَ. 17اصْنَعْ مَعِي آيَةً لِلْخَيْرِ، فَيَرَاهَا مُبْغِضِيَّ وَيَعْتَرِيَهُمُ الْخِزْيُ، فَإِنَّكَ أَنْتَ يَا رَبُّ قَدْ أَعَنْتَنِي وَعَزَّيْتَنِي.