Zaburi 78 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 78:1-72

Zaburi 78

Mungu Na Watu Wake

Utenzi wa Asafu.

178:1 Kut 19:5; Kum 32:29; Isa 51:4; 55:3Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu,

sikilizeni maneno ya kinywa changu.

278:2 Za 49:4; Mt 13:35Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo,

nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:

378:3 Za 44:1; Amu 6:13yale ambayo tuliyasikia na kuyajua,

yale ambayo baba zetu walituambia.

478:4 Kut 12:26; Yos 4:6, 7; Kum 4:9; 11:19; 32:7; Za 71:18; 26:7; 71:17Hatutayaficha kwa watoto wao;

tutakiambia kizazi kijacho

matendo yastahiliyo sifa ya Bwana,

uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.

578:5 Za 19:7; 81:5; 147:19Aliagiza amri kwa Yakobo

na akaweka sheria katika Israeli,

ambazo aliwaamuru baba zetu

wawafundishe watoto wao,

678:6 Za 22:31; 102:18ili kizazi kijacho kizijue,

pamoja na watoto ambao watazaliwa,

nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.

778:7 Kum 6:12; 5:29Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu,

nao wasingesahau matendo yake,

bali wangalizishika amri zake.

878:8 2Nya 30:7; Kut 32:9; 23:21; Kum 21:18; Isa 30:9; 65:2Ili wasifanane na baba zao,

waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi,

ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake,

ambao roho zao hazikumwamini.

978:9 Za 78:57; 1Nya 12:2; Hos 7:16; Amu 20:39Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde,

walikimbia siku ya vita.

1078:10 Yos 7:10; 2Fal 17:15; Kut 16:28; Yer 11:8Hawakulishika agano la Mungu

na walikataa kuishi kwa sheria yake.

1178:11 Za 106:13; Isa 17:10; Yer 2:32Walisahau aliyokuwa ameyatenda,

maajabu aliyokuwa amewaonyesha.

1278:12 Neh 9:17; Za 106:22; Kut 11:9; Hes 13:22; Mwa 32:3; Isa 19:11Alitenda miujiza machoni mwa baba zao,

huko Soani, katika nchi ya Misri.

1378:13 Kut 14:21, 22; 15:8; Za 66:6; 136:13Aliigawanya bahari akawapitisha,

alifanya maji yasimame imara kama ukuta.

1478:14 Kut 13:21; Za 105:39Aliwaongoza kwa wingu mchana

na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.

1578:15 Hes 20:11; 1Kor 10:4; Kut 17; 6; Za 105:41; Isa 41:18Alipasua miamba jangwani

na akawapa maji tele kama bahari,

1678:16 Kum 9:21alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka,

akayafanya maji yatiririke kama mito.

1778:17 Za 78:32Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake,

wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.

1878:18 Kut 15:24; 17:2; 1Kor 10:9; Hes 11:4Kwa makusudi walimjaribu Mungu,

wakidai vyakula walivyovitamani.

1978:19 Hes 11:4; 21:5Walinena dhidi ya Mungu, wakisema,

“Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?

2078:20 Hes 20:11; Kut 17:6Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu,

vijito vikatiririka maji mengi.

Lakini je, aweza kutupa chakula pia?

Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”

2178:21 Hes 11:1Bwana alipowasikia, alikasirika sana,

moto wake ukawa dhidi ya Yakobo,

na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,

2278:22 Kum 1:32; Ebr 3:19; 3:10kwa kuwa hawakumwamini Mungu,

wala kuutumainia ukombozi wake.

2378:23 Mwa 7:11; Kum 28:12; 2Fal 7:2Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu

na kufungua milango ya mbingu,

2478:24 Kut 16:4; Yn 6:31; Neh 9:15, 20; 1Kor 10:3akawanyeshea mana ili watu wale;

aliwapa nafaka ya mbinguni.

25Watu walikula mkate wa malaika,

akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.

2678:26 Hes 11:31Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu

na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.

2778:27 Kut 16:13; Hes 11:31Aliwanyeshea nyama kama mavumbi,

ndege warukao kama mchanga wa pwani.

28Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao,

kuzunguka mahema yao yote.

2978:29 Hes 11:20Walikula na kusaza,

kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.

3078:30 Hes 11:33Kabla hawajamaliza kula walichokitamani,

hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,

3178:31 Isa 10:16hasira ya Mungu ikawaka juu yao,

akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao,

akiwaangusha vijana wa Israeli.

3278:32 Za 78:11, 17, 22Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi,

licha ya maajabu yake, hawakuamini.

3378:33 Hes 14:29, 35Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili

na miaka yao katika vitisho.

3478:34 Kum 4:29; Hos 5:15; Hes 5:15Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao,

waliosalia walimtafuta,

walimgeukia tena kwa shauku.

3578:35 Mwa 49:24; Kum 9:26Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao,

kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.

3678:36 Eze 33:31Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao,

wakisema uongo kwa ndimi zao,

3778:37 Za 78:8; Mdo 8:21mioyo yao haikuwa thabiti kwake,

wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.

3878:38 Kut 34:6; Neh 9:17; Za 25:11; 85:2; 86:15; 1Fal 21:29; Isa 1:25; 27:9; 48:9, 10; 30:18; Mik 7:18; Rum 2:4; Dan 11:35Hata hivyo alikuwa na huruma,

alisamehe maovu yao

na hakuwaangamiza.

Mara kwa mara alizuia hasira yake,

wala hakuchochea ghadhabu yake yote.

3978:39 Mwa 6:3; Isa 29:5; Ay 7:7; Yak 4:14; Yn 3:6Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu,

upepo upitao ambao haurudi.

4078:40 Kut 23:21; Za 95:8; 106:14; Efe 4:30Mara ngapi walimwasi jangwani

na kumhuzunisha nyikani!

4178:41 Kut 17:2; 2Fal 19:22; Za 71:22; 89:18Walimjaribu Mungu mara kwa mara,

wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

4278:42 Amu 3:7; Neh 9:17; Za 27:11Hawakukumbuka uwezo wake,

siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,

4378:43 Kut 10:1; 3:20siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri,

maajabu yake huko Soani.

4478:44 Kut 7:20, 21; Za 105:29; 78:45Aligeuza mito yao kuwa damu,

hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.

4578:45 Kut 8:2, 6, 24; Za 105Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala,

na vyura wakawaharibu.

4678:46 Nah 3:15; Kut 10:13Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao,

mazao yao kwa nzige.

4778:47 Za 105:32; 147:17; Kut 9:23Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe

na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.

4878:48 Kut 9:25Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe,

akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.

4978:49 Kut 15:7; Mwa 19:13; 1Kor 10:10; Rum 2:8Aliwafungulia hasira yake kali,

ghadhabu yake, hasira na uadui,

na kundi la malaika wa kuharibu.

50Aliitengenezea njia hasira yake,

hakuwaepusha na kifo,

bali aliwaachia tauni.

5178:51 Mwa 9:12; Kut 12:12; Za 135:8; 105:23; 106:22Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,

matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.

5278:52 Ay 21:11; Za 28:9; 77:20Lakini aliwatoa watu wake kama kundi,

akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.

5378:53 Kut 14:28; 15:7; Za 106:10Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa,

bali bahari iliwameza adui zao.

5478:54 Kut 15:17; Za 44:3Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu,

hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.

5578:55 Za 44:2; Kum 1:38; Yos 13:7; Mdo 13:19Aliyafukuza mataifa mbele yao,

na kuwagawia nchi zao kama urithi,

aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.

56Lakini wao walimjaribu Mungu,

na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana,

wala hawakuzishika sheria zake.

5778:57 2Nya 30:7; Za 78:9; Eze 20:27; Hos 7:16Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu,

wakawa wasioweza kutegemewa

kama upinde wenye kasoro.

5878:58 Amu 2:12; Law 26:30; Kut 20:4; Kum 12:2; 5:8; 32:21; Hes 33:51Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu,

wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.

5978:59 Za 55:19; Law 26:28; Hes 32:14; Kum 32:19; Ebr 4:13Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana,

akamkataa Israeli kabisa.

6078:60 Yos 18:1; Eze 8:6; 1Sam 4:11; Yer 7:12Akaiacha hema ya Shilo,

hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.

6178:61 Amu 18:30; 1Sam 4:12; Za 132:8; 1Sam 4:17Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani,

utukufu wake mikononi mwa adui.

6278:62 Kum 28:25; 1Sam 10:1Aliachia watu wake wauawe kwa upanga,

akaukasirikia sana urithi wake.

6378:63 1Fal 4:32; Yer 7:32; 16:9; 25:10; Hes 11:1Moto uliwaangamiza vijana wao,

na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,

6478:64 Ay 27:15; 1Sam 4:17makuhani wao waliuawa kwa upanga,

wala wajane wao hawakuweza kulia.

6578:65 Za 44:23; Isa 42:13Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini,

kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.

6678:66 1Sam 5:6Aliwapiga na kuwashinda adui zake,

akawatia katika aibu ya milele.

6778:67 Yer 7:15; Hos 9:13; 12:1Ndipo alipozikataa hema za Yosefu,

hakulichagua kabila la Efraimu,

6878:68 Hes 1:7; Kut 15:17; Za 68:16; 108:8lakini alilichagua kabila la Yuda,

Mlima Sayuni, ambao aliupenda.

6978:69 Za 15:1; 1Fal 6:1Alijenga patakatifu pake kama vilele,

kama dunia ambayo aliimarisha milele.

7078:70 1Sam 16:1Akamchagua Daudi mtumishi wake

na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.

7178:71 Mwa 37:2; Za 28:9; 2Sam 5:2; 1Nya 11:2; Mik 5:2-4; Zek 11:4Kutoka kuchunga kondoo alimleta

kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo,

wa Israeli urithi wake.

7278:72 1Fal 9:4; Mwa 17:1Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo,

kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

New International Version

Psalms 78:1-72

Psalm 78

A maskilTitle: Probably a literary or musical term of Asaph.

1My people, hear my teaching;

listen to the words of my mouth.

2I will open my mouth with a parable;

I will utter hidden things, things from of old—

3things we have heard and known,

things our ancestors have told us.

4We will not hide them from their descendants;

we will tell the next generation

the praiseworthy deeds of the Lord,

his power, and the wonders he has done.

5He decreed statutes for Jacob

and established the law in Israel,

which he commanded our ancestors

to teach their children,

6so the next generation would know them,

even the children yet to be born,

and they in turn would tell their children.

7Then they would put their trust in God

and would not forget his deeds

but would keep his commands.

8They would not be like their ancestors—

a stubborn and rebellious generation,

whose hearts were not loyal to God,

whose spirits were not faithful to him.

9The men of Ephraim, though armed with bows,

turned back on the day of battle;

10they did not keep God’s covenant

and refused to live by his law.

11They forgot what he had done,

the wonders he had shown them.

12He did miracles in the sight of their ancestors

in the land of Egypt, in the region of Zoan.

13He divided the sea and led them through;

he made the water stand up like a wall.

14He guided them with the cloud by day

and with light from the fire all night.

15He split the rocks in the wilderness

and gave them water as abundant as the seas;

16he brought streams out of a rocky crag

and made water flow down like rivers.

17But they continued to sin against him,

rebelling in the wilderness against the Most High.

18They willfully put God to the test

by demanding the food they craved.

19They spoke against God;

they said, “Can God really

spread a table in the wilderness?

20True, he struck the rock,

and water gushed out,

streams flowed abundantly,

but can he also give us bread?

Can he supply meat for his people?”

21When the Lord heard them, he was furious;

his fire broke out against Jacob,

and his wrath rose against Israel,

22for they did not believe in God

or trust in his deliverance.

23Yet he gave a command to the skies above

and opened the doors of the heavens;

24he rained down manna for the people to eat,

he gave them the grain of heaven.

25Human beings ate the bread of angels;

he sent them all the food they could eat.

26He let loose the east wind from the heavens

and by his power made the south wind blow.

27He rained meat down on them like dust,

birds like sand on the seashore.

28He made them come down inside their camp,

all around their tents.

29They ate till they were gorged—

he had given them what they craved.

30But before they turned from what they craved,

even while the food was still in their mouths,

31God’s anger rose against them;

he put to death the sturdiest among them,

cutting down the young men of Israel.

32In spite of all this, they kept on sinning;

in spite of his wonders, they did not believe.

33So he ended their days in futility

and their years in terror.

34Whenever God slew them, they would seek him;

they eagerly turned to him again.

35They remembered that God was their Rock,

that God Most High was their Redeemer.

36But then they would flatter him with their mouths,

lying to him with their tongues;

37their hearts were not loyal to him,

they were not faithful to his covenant.

38Yet he was merciful;

he forgave their iniquities

and did not destroy them.

Time after time he restrained his anger

and did not stir up his full wrath.

39He remembered that they were but flesh,

a passing breeze that does not return.

40How often they rebelled against him in the wilderness

and grieved him in the wasteland!

41Again and again they put God to the test;

they vexed the Holy One of Israel.

42They did not remember his power—

the day he redeemed them from the oppressor,

43the day he displayed his signs in Egypt,

his wonders in the region of Zoan.

44He turned their river into blood;

they could not drink from their streams.

45He sent swarms of flies that devoured them,

and frogs that devastated them.

46He gave their crops to the grasshopper,

their produce to the locust.

47He destroyed their vines with hail

and their sycamore-figs with sleet.

48He gave over their cattle to the hail,

their livestock to bolts of lightning.

49He unleashed against them his hot anger,

his wrath, indignation and hostility—

a band of destroying angels.

50He prepared a path for his anger;

he did not spare them from death

but gave them over to the plague.

51He struck down all the firstborn of Egypt,

the firstfruits of manhood in the tents of Ham.

52But he brought his people out like a flock;

he led them like sheep through the wilderness.

53He guided them safely, so they were unafraid;

but the sea engulfed their enemies.

54And so he brought them to the border of his holy land,

to the hill country his right hand had taken.

55He drove out nations before them

and allotted their lands to them as an inheritance;

he settled the tribes of Israel in their homes.

56But they put God to the test

and rebelled against the Most High;

they did not keep his statutes.

57Like their ancestors they were disloyal and faithless,

as unreliable as a faulty bow.

58They angered him with their high places;

they aroused his jealousy with their idols.

59When God heard them, he was furious;

he rejected Israel completely.

60He abandoned the tabernacle of Shiloh,

the tent he had set up among humans.

61He sent the ark of his might into captivity,

his splendor into the hands of the enemy.

62He gave his people over to the sword;

he was furious with his inheritance.

63Fire consumed their young men,

and their young women had no wedding songs;

64their priests were put to the sword,

and their widows could not weep.

65Then the Lord awoke as from sleep,

as a warrior wakes from the stupor of wine.

66He beat back his enemies;

he put them to everlasting shame.

67Then he rejected the tents of Joseph,

he did not choose the tribe of Ephraim;

68but he chose the tribe of Judah,

Mount Zion, which he loved.

69He built his sanctuary like the heights,

like the earth that he established forever.

70He chose David his servant

and took him from the sheep pens;

71from tending the sheep he brought him

to be the shepherd of his people Jacob,

of Israel his inheritance.

72And David shepherded them with integrity of heart;

with skillful hands he led them.