Zaburi 78 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 78:1-72

Zaburi 78

Mungu Na Watu Wake

Utenzi wa Asafu.

178:1 Kut 19:5; Kum 32:29; Isa 51:4; 55:3Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu,

sikilizeni maneno ya kinywa changu.

278:2 Za 49:4; Mt 13:35Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo,

nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:

378:3 Za 44:1; Amu 6:13yale ambayo tuliyasikia na kuyajua,

yale ambayo baba zetu walituambia.

478:4 Kut 12:26; Yos 4:6, 7; Kum 4:9; 11:19; 32:7; Za 71:18; 26:7; 71:17Hatutayaficha kwa watoto wao;

tutakiambia kizazi kijacho

matendo yastahiliyo sifa ya Bwana,

uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.

578:5 Za 19:7; 81:5; 147:19Aliagiza amri kwa Yakobo

na akaweka sheria katika Israeli,

ambazo aliwaamuru baba zetu

wawafundishe watoto wao,

678:6 Za 22:31; 102:18ili kizazi kijacho kizijue,

pamoja na watoto ambao watazaliwa,

nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.

778:7 Kum 6:12; 5:29Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu,

nao wasingesahau matendo yake,

bali wangalizishika amri zake.

878:8 2Nya 30:7; Kut 32:9; 23:21; Kum 21:18; Isa 30:9; 65:2Ili wasifanane na baba zao,

waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi,

ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake,

ambao roho zao hazikumwamini.

978:9 Za 78:57; 1Nya 12:2; Hos 7:16; Amu 20:39Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde,

walikimbia siku ya vita.

1078:10 Yos 7:10; 2Fal 17:15; Kut 16:28; Yer 11:8Hawakulishika agano la Mungu

na walikataa kuishi kwa sheria yake.

1178:11 Za 106:13; Isa 17:10; Yer 2:32Walisahau aliyokuwa ameyatenda,

maajabu aliyokuwa amewaonyesha.

1278:12 Neh 9:17; Za 106:22; Kut 11:9; Hes 13:22; Mwa 32:3; Isa 19:11Alitenda miujiza machoni mwa baba zao,

huko Soani, katika nchi ya Misri.

1378:13 Kut 14:21, 22; 15:8; Za 66:6; 136:13Aliigawanya bahari akawapitisha,

alifanya maji yasimame imara kama ukuta.

1478:14 Kut 13:21; Za 105:39Aliwaongoza kwa wingu mchana

na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.

1578:15 Hes 20:11; 1Kor 10:4; Kut 17; 6; Za 105:41; Isa 41:18Alipasua miamba jangwani

na akawapa maji tele kama bahari,

1678:16 Kum 9:21alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka,

akayafanya maji yatiririke kama mito.

1778:17 Za 78:32Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake,

wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.

1878:18 Kut 15:24; 17:2; 1Kor 10:9; Hes 11:4Kwa makusudi walimjaribu Mungu,

wakidai vyakula walivyovitamani.

1978:19 Hes 11:4; 21:5Walinena dhidi ya Mungu, wakisema,

“Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?

2078:20 Hes 20:11; Kut 17:6Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu,

vijito vikatiririka maji mengi.

Lakini je, aweza kutupa chakula pia?

Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”

2178:21 Hes 11:1Bwana alipowasikia, alikasirika sana,

moto wake ukawa dhidi ya Yakobo,

na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,

2278:22 Kum 1:32; Ebr 3:19; 3:10kwa kuwa hawakumwamini Mungu,

wala kuutumainia ukombozi wake.

2378:23 Mwa 7:11; Kum 28:12; 2Fal 7:2Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu

na kufungua milango ya mbingu,

2478:24 Kut 16:4; Yn 6:31; Neh 9:15, 20; 1Kor 10:3akawanyeshea mana ili watu wale;

aliwapa nafaka ya mbinguni.

25Watu walikula mkate wa malaika,

akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.

2678:26 Hes 11:31Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu

na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.

2778:27 Kut 16:13; Hes 11:31Aliwanyeshea nyama kama mavumbi,

ndege warukao kama mchanga wa pwani.

28Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao,

kuzunguka mahema yao yote.

2978:29 Hes 11:20Walikula na kusaza,

kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.

3078:30 Hes 11:33Kabla hawajamaliza kula walichokitamani,

hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,

3178:31 Isa 10:16hasira ya Mungu ikawaka juu yao,

akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao,

akiwaangusha vijana wa Israeli.

3278:32 Za 78:11, 17, 22Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi,

licha ya maajabu yake, hawakuamini.

3378:33 Hes 14:29, 35Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili

na miaka yao katika vitisho.

3478:34 Kum 4:29; Hos 5:15; Hes 5:15Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao,

waliosalia walimtafuta,

walimgeukia tena kwa shauku.

3578:35 Mwa 49:24; Kum 9:26Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao,

kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.

3678:36 Eze 33:31Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao,

wakisema uongo kwa ndimi zao,

3778:37 Za 78:8; Mdo 8:21mioyo yao haikuwa thabiti kwake,

wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.

3878:38 Kut 34:6; Neh 9:17; Za 25:11; 85:2; 86:15; 1Fal 21:29; Isa 1:25; 27:9; 48:9, 10; 30:18; Mik 7:18; Rum 2:4; Dan 11:35Hata hivyo alikuwa na huruma,

alisamehe maovu yao

na hakuwaangamiza.

Mara kwa mara alizuia hasira yake,

wala hakuchochea ghadhabu yake yote.

3978:39 Mwa 6:3; Isa 29:5; Ay 7:7; Yak 4:14; Yn 3:6Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu,

upepo upitao ambao haurudi.

4078:40 Kut 23:21; Za 95:8; 106:14; Efe 4:30Mara ngapi walimwasi jangwani

na kumhuzunisha nyikani!

4178:41 Kut 17:2; 2Fal 19:22; Za 71:22; 89:18Walimjaribu Mungu mara kwa mara,

wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

4278:42 Amu 3:7; Neh 9:17; Za 27:11Hawakukumbuka uwezo wake,

siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,

4378:43 Kut 10:1; 3:20siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri,

maajabu yake huko Soani.

4478:44 Kut 7:20, 21; Za 105:29; 78:45Aligeuza mito yao kuwa damu,

hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.

4578:45 Kut 8:2, 6, 24; Za 105Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala,

na vyura wakawaharibu.

4678:46 Nah 3:15; Kut 10:13Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao,

mazao yao kwa nzige.

4778:47 Za 105:32; 147:17; Kut 9:23Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe

na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.

4878:48 Kut 9:25Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe,

akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.

4978:49 Kut 15:7; Mwa 19:13; 1Kor 10:10; Rum 2:8Aliwafungulia hasira yake kali,

ghadhabu yake, hasira na uadui,

na kundi la malaika wa kuharibu.

50Aliitengenezea njia hasira yake,

hakuwaepusha na kifo,

bali aliwaachia tauni.

5178:51 Mwa 9:12; Kut 12:12; Za 135:8; 105:23; 106:22Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,

matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.

5278:52 Ay 21:11; Za 28:9; 77:20Lakini aliwatoa watu wake kama kundi,

akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.

5378:53 Kut 14:28; 15:7; Za 106:10Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa,

bali bahari iliwameza adui zao.

5478:54 Kut 15:17; Za 44:3Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu,

hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.

5578:55 Za 44:2; Kum 1:38; Yos 13:7; Mdo 13:19Aliyafukuza mataifa mbele yao,

na kuwagawia nchi zao kama urithi,

aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.

56Lakini wao walimjaribu Mungu,

na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana,

wala hawakuzishika sheria zake.

5778:57 2Nya 30:7; Za 78:9; Eze 20:27; Hos 7:16Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu,

wakawa wasioweza kutegemewa

kama upinde wenye kasoro.

5878:58 Amu 2:12; Law 26:30; Kut 20:4; Kum 12:2; 5:8; 32:21; Hes 33:51Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu,

wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.

5978:59 Za 55:19; Law 26:28; Hes 32:14; Kum 32:19; Ebr 4:13Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana,

akamkataa Israeli kabisa.

6078:60 Yos 18:1; Eze 8:6; 1Sam 4:11; Yer 7:12Akaiacha hema ya Shilo,

hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.

6178:61 Amu 18:30; 1Sam 4:12; Za 132:8; 1Sam 4:17Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani,

utukufu wake mikononi mwa adui.

6278:62 Kum 28:25; 1Sam 10:1Aliachia watu wake wauawe kwa upanga,

akaukasirikia sana urithi wake.

6378:63 1Fal 4:32; Yer 7:32; 16:9; 25:10; Hes 11:1Moto uliwaangamiza vijana wao,

na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,

6478:64 Ay 27:15; 1Sam 4:17makuhani wao waliuawa kwa upanga,

wala wajane wao hawakuweza kulia.

6578:65 Za 44:23; Isa 42:13Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini,

kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.

6678:66 1Sam 5:6Aliwapiga na kuwashinda adui zake,

akawatia katika aibu ya milele.

6778:67 Yer 7:15; Hos 9:13; 12:1Ndipo alipozikataa hema za Yosefu,

hakulichagua kabila la Efraimu,

6878:68 Hes 1:7; Kut 15:17; Za 68:16; 108:8lakini alilichagua kabila la Yuda,

Mlima Sayuni, ambao aliupenda.

6978:69 Za 15:1; 1Fal 6:1Alijenga patakatifu pake kama vilele,

kama dunia ambayo aliimarisha milele.

7078:70 1Sam 16:1Akamchagua Daudi mtumishi wake

na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.

7178:71 Mwa 37:2; Za 28:9; 2Sam 5:2; 1Nya 11:2; Mik 5:2-4; Zek 11:4Kutoka kuchunga kondoo alimleta

kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo,

wa Israeli urithi wake.

7278:72 1Fal 9:4; Mwa 17:1Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo,

kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Salmo 78:1-72

Salmo 78

Masquil de Asaf.

1Pueblo mío, atiende a mi enseñanza;

presta oído a las palabras de mi boca.

2Mis labios pronunciarán parábolas

y evocarán misterios de antaño,

3cosas que hemos oído y conocido,

y que nuestros padres nos han contado.

4No las esconderemos de sus descendientes;

hablaremos a la generación venidera

del poder del Señor, de sus proezas,

y de las maravillas que ha realizado.

5Él promulgó un decreto para Jacob,

dictó una ley para Israel;

ordenó a nuestros antepasados

enseñarlos a sus descendientes,

6para que los conocieran las generaciones venideras

y los hijos que habrían de nacer,

que a su vez los enseñarían a sus hijos.

7Así ellos pondrían su confianza en Dios

y no se olvidarían de sus proezas,

sino que cumplirían sus mandamientos.

8Así no serían como sus antepasados:

generación obstinada y rebelde,

gente de corazón fluctuante,

cuyo espíritu no se mantuvo fiel a Dios.

9La tribu de Efraín, con sus diestros arqueros,

se puso en fuga el día de la batalla.

10No cumplieron con el pacto de Dios,

sino que se negaron a seguir sus enseñanzas.

11Echaron al olvido sus proezas,

las maravillas que les había mostrado,

12los milagros que hizo a la vista de sus padres

en la tierra de Egipto, en la región de Zoán.

13Partió el mar en dos para que ellos lo cruzaran,

mientras mantenía las aguas firmes como un muro.

14De día los guio con una nube,

y toda la noche con luz de fuego.

15En el desierto partió en dos las rocas,

y les dio a beber torrentes de aguas;

16hizo que brotaran arroyos de la peña

y que las aguas fluyeran como ríos.

17Pero ellos volvieron a pecar contra él;

en el desierto se rebelaron contra el Altísimo.

18Con toda intención pusieron a Dios a prueba,

y le exigieron comida a su antojo.

19Murmuraron contra Dios, y aun dijeron:

«¿Podrá Dios prepararnos una mesa en el desierto?

20Cuando golpeó la roca,

el agua brotó en torrentes;

pero ¿podrá también darnos de comer?,

¿podrá proveerle carne a su pueblo?»

21Cuando el Señor oyó esto, se puso muy furioso;

su enojo se encendió contra Jacob,

su ira ardió contra Israel.

22Porque no confiaron en Dios,

ni creyeron que él los salvaría.

23Desde lo alto dio una orden a las nubes,

y se abrieron las puertas de los cielos.

24Hizo que les lloviera maná, para que comieran;

pan del cielo les dio a comer.

25Todos ellos comieron pan de ángeles;

Dios les envió comida hasta saciarlos.

26Desató desde el cielo el viento solano,

y con su poder levantó el viento del sur.

27Cual lluvia de polvo, hizo que les lloviera carne;

¡nubes de pájaros, como la arena del mar!

28Los hizo caer en medio de su campamento

y en los alrededores de sus tiendas.

29Comieron y se hartaron,

pues Dios les cumplió su capricho.

30Pero el capricho no les duró mucho:

aún tenían la comida en la boca

31cuando el enojo de Dios vino sobre ellos:

dio muerte a sus hombres más robustos;

abatió a la flor y nata de Israel.

32A pesar de todo, siguieron pecando

y no creyeron en sus maravillas.

33Por tanto, Dios hizo que sus días

se esfumaran como un suspiro,

que sus años acabaran en medio del terror.

34Si Dios los castigaba, entonces lo buscaban,

y con ansias se volvían de nuevo a él.

35Se acordaban de que Dios era su roca,

de que el Dios Altísimo era su redentor.

36Pero entonces lo halagaban con la boca,

y le mentían con la lengua.

37No fue su corazón sincero para con Dios;

no fueron fieles a su pacto.

38Sin embargo, él tuvo compasión de ellos;

les perdonó su maldad y no los destruyó.

Una y otra vez contuvo su enojo,

y no se dejó llevar del todo por la ira.

39Se acordó de que eran simples mortales,

un efímero suspiro que jamás regresa.

40¡Cuántas veces se rebelaron contra él en el desierto,

y lo entristecieron en los páramos!

41Una y otra vez ponían a Dios a prueba;

provocaban al Santo de Israel.

42Jamás se acordaron de su poder,

de cuando los rescató del opresor,

43ni de sus señales milagrosas en Egipto,

ni de sus portentos en la región de Zoán,

44cuando convirtió en sangre los ríos egipcios

y no pudieron ellos beber de sus arroyos;

45cuando les envió tábanos que los devoraban,

y ranas que los destruían;

46cuando entregó sus cosechas a los saltamontes,

y sus sembrados a la langosta;

47cuando con granizo destruyó sus viñas,

y con escarcha sus higueras;

48cuando entregó su ganado al granizo,

y sus rebaños a las centellas;

49cuando lanzó contra ellos el ardor de su ira,

de su furor, indignación y hostilidad:

¡todo un ejército de ángeles destructores!

50Dio rienda suelta a su enojo

y no los libró de la muerte,

sino que los entregó a la plaga.

51Dio muerte a todos los primogénitos de Egipto,

a las primicias de su raza en los campamentos de Cam.

52A su pueblo lo guio como a un rebaño;

los llevó por el desierto, como a ovejas,

53infundiéndoles confianza para que no temieran.

Pero a sus enemigos se los tragó el mar.

54Trajo a su pueblo a su tierra santa,

a estas montañas que su diestra conquistó.

55Al paso de los israelitas expulsó naciones,

cuyas tierras dio a su pueblo en heredad;

¡así estableció en sus tiendas a las tribus de Israel!

56Pero ellos pusieron a prueba a Dios:

se rebelaron contra el Altísimo

y desobedecieron sus estatutos.

57Fueron desleales y traidores, como sus padres;

¡tan falsos como un arco defectuoso!

58Lo irritaron con sus santuarios paganos;

con sus ídolos despertaron sus celos.

59Dios lo supo y se puso muy furioso,

por lo que rechazó completamente a Israel.

60Abandonó el tabernáculo de Siló,

que era su santuario aquí en la tierra,

61y dejó que el símbolo de su poder y gloria

cayera cautivo en manos enemigas.

62Tan furioso estaba contra su pueblo

que dejó que los mataran a filo de espada.

63A sus jóvenes los consumió el fuego,

y no hubo cantos nupciales para sus muchachas;

64a filo de espada cayeron sus sacerdotes,

y sus viudas no pudieron hacerles duelo.

65Despertó entonces el Señor,

como quien despierta de un sueño,

como un guerrero que, a causa del vino,

lanza gritos desaforados.

66Hizo retroceder a sus enemigos,

y los puso en vergüenza para siempre.

67Rechazó a los descendientes78:67 a los descendientes. Lit. al tabernáculo. de José,

y no escogió a la tribu de Efraín;

68más bien, escogió a la tribu de Judá

y al monte Sión, al cual ama.

69Construyó su santuario, alto como los cielos,78:69 santuario, alto como los cielos. Lit. santuario como las alturas.

como la tierra, que él afirmó para siempre.

70Escogió a su siervo David,

al que sacó de los apriscos de las ovejas,

71y lo quitó de andar arreando los rebaños

para que fuera el pastor de Jacob, su pueblo;

el pastor de Israel, su herencia.

72Y David los pastoreó con corazón sincero;

con mano experta los dirigió.