Zaburi 74 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 74:1-23

Zaburi 74

Maombi Kwa Ajili Ya Taifa Kuokolewa

Utenzi wa Asafu.

174:1 Yer 23:1; Za 43:2; 44:23; 95:7; 79:13; 100:3; Eze 34:8, 31; Lk 12:32Ee Mungu, mbona umetukataa milele?

Mbona hasira yako inatoka moshi

juu ya kondoo wa malisho yako?

274:2 1Kor 6:20; Kum 32:7; Kut 34:9; 15:13, 16; Isa 48:20; Za 2:6; 43:3; 68:16; Isa 46:13; Oba 1:17; Yoe 3:17, 21Kumbuka watu uliowanunua zamani,

kabila la urithi wako, ambao uliwakomboa:

Mlima Sayuni, ambamo uliishi.

374:3 Isa 44:26; 52:9Geuza hatua zako kuelekea magofu haya ya kudumu,

uharibifu wote huu ambao adui ameuleta pale patakatifu.

474:4 Mao 2:7; Hes 2:2; Yer 4:6; Dan 6:27Adui zako wamenguruma pale ulipokutana nasi,

wanaweka bendera zao kama alama.

574:5 Yer 46:23Walifanya kama watu wanaotumia mashoka

kukata kichaka cha miti.

674:6 1Fal 6:18Walivunjavunja milango yote iliyonakshiwa

kwa mashoka na vishoka vyao.

774:7 Law 15:31; 20:3; Mdo 21:28; Za 75:1Waliteketeza kabisa mahali pako patakatifu,

wakayanajisi makao ya Jina lako.

874:8 2Fal 25:9; Za 83:4; 94:5; Yer 34:22; 52:13; 21:10; 2Nya 36:19Walisema mioyoni mwao,

“Tutawaponda kabisa!”

Walichoma kila mahali ambapo Mungu

aliabudiwa katika nchi.

974:9 Kut 4:17; 10:1; 1Sam 3:1; Mik 3:6; Mt 16:4Hatukupewa ishara za miujiza;

hakuna manabii waliobaki,

hakuna yeyote kati yetu ajuaye

hali hii itachukua muda gani.

1074:10 Za 6:3; 79:5; 80:4; 74:22; 44:16Ee Mungu, mtesi atakudhihaki mpaka lini?

Je, adui watalitukana jina lako milele?

1174:11 Kut 15:6; Neh 5:13; Eze 5:3Kwa nini unazuia mkono wako,

mkono wako wa kuume?

Uutoe kutoka makunjo ya vazi lako

na uwaangamize!

1274:12 Za 2:6; 24:7; 68:24; 44:4Lakini wewe, Ee Mungu, ni mfalme wangu tangu zamani,

unaleta wokovu duniani.

1374:13 Isa 51:9; 27:1; Eze 29:3; 32:2; Kut 14:21Ni wewe uliyeigawanya bahari kwa uweza wako;

ulivunja vichwa vya wanyama wakubwa wa kutisha katika maji.

1474:14 Hes 14:9; Za 72:9; Ay 3:8; Isa 13:21; 23:13; 34:14; Yer 50:39Ni wewe uliyeponda vichwa vya Lewiathani74:14 Lewiathani ni mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa.

nawe ukamtoa kama chakula

kwa viumbe vya jangwani.

1574:15 Kut 14:29; 17:6; Hes 20:11; Isa 11:16; Hab 3:9; Ufu 16:12; Yos 2:10Ni wewe uliyefungua chemchemi na vijito,

ulikausha mito ambayo ilikuwa ikitiririka daima.

1674:16 Mwa 1:16; Za 136:7-9Mchana ni wako, nao usiku ni wako pia,

uliziweka jua na mwezi.

1774:17 Mdo 17:26; Kum 32:8; Mwa 8:22Ni wewe uliyeiweka mipaka yote ya dunia,

ulifanya kiangazi na masika.

1874:18 Ufu 16:19; Kum 32:9Ee Bwana, kumbuka jinsi mtesi alivyokudhihaki,

jinsi watu wapumbavu walivyolitukana jina lako.

1974:19 Mwa 8:8; Isa 59:11; Za 9:18Usiukabidhi uhai wa njiwa wako kwa wanyama wakali wa mwitu;

usisahau kabisa uhai wa watu wako wanaoteseka milele.

2074:20 Mwa 6:18; 17:7; Law 26:44; Yer 33:21; Ay 34:22Likumbuke agano lako,

maana mara kwa mara mambo ya jeuri

yamejaa katika sehemu za giza nchini.

2174:21 Isa 58:10; Za 9:9, 18; 10:18; 103:6; 35:10Usiruhusu walioonewa warudi nyuma kwa aibu;

maskini na wahitaji hebu walisifu jina lako.

2274:22 Za 17:13; 53:1Inuka, Ee Mungu, ujitetee;

kumbuka jinsi wapumbavu

wanavyokudhihaki mchana kutwa.

2374:23 Isa 31:4; Za 65:7; 46:6; Hes 25:17Usipuuze makelele ya watesi wako,

ghasia za adui zako, zinazoinuka mfululizo.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

詩篇 74:1-23

第 74 篇

祈求上帝眷顧祂的子民

亞薩的訓誨詩。

1上帝啊,

你為何永遠丟棄了我們?

你為何對自己草場上的羊大發雷霆?

2求你眷顧你在古時所救贖的子民,

你揀選為產業的族類,

求你眷顧你所居住的錫安山。

3求你前去觀看那久已荒涼之地,

看看敵人對聖所的破壞。

4他們在你聖所中高聲叫嚷,

豎立起自己的旗幟。

5他們大肆毀壞,

好像人掄起斧頭砍伐樹林。

6他們用斧頭、錘子把雕刻的牆板都搗毀了。

7他們縱火焚燒你的聖所,

把它夷為平地,

褻瀆了你的居所。

8他們心裡說:「我們要徹底毀滅一切。」

於是他們燒毀了境內所有敬拜上帝的地方。

9我們再也看不到你的徵兆,

先知也沒有了。

無人知道這一切何時才會結束。

10上帝啊,

仇敵嘲笑你的名要到何時呢?

他們要永無休止地辱罵你嗎?

11你為何不伸出大能的右手?

求你出手給他們致命的一擊。

12上帝啊,

你自古以來就是我的王,

你給世上帶來拯救。

13你曾用大能分開海水,

打碎水中巨獸的頭。

14你曾打碎海怪的頭,

把牠丟給曠野的禽獸吃。

15你曾開闢泉源和溪流,

也曾使滔滔河水枯乾。

16白晝和黑夜都屬於你,

你設立了日月。

17你劃定大地的疆界,

又創造了盛夏和寒冬。

18耶和華啊,

求你記住敵人對你的嘲笑和愚妄人對你的褻瀆。

19求你不要把你的子民交給仇敵74·18-19 子民」希伯來文是「鴿子」;「仇敵」希伯來文是「野獸」。

不要永遠對你受苦的子民棄置不顧。

20求你顧念你的應許,

因地上黑暗之處充滿了暴力。

21求你不要讓受壓迫的人羞愧而去。

願貧窮困苦的人讚美你的名。

22上帝啊,求你起來維護自己,

別忘記愚妄人怎樣整天嘲笑你。

23不要對你仇敵的喧嚷置之不理,

與你為敵的人不停地叫囂。