Zaburi 73 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 73:1-28

KITABU CHA TATU

(Zaburi 73–89)

Zaburi 73

Haki Ya Mungu

Zaburi ya Asafu.

173:1 Za 24:4; 5:8Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli,

kwa wale ambao mioyo yao ni safi.

273:2 Kum 32:35; Za 69:2; Efe 4:27Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza;

nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.

373:3 Mit 3:31; 23:17; 24:1-2; Ay 9:24; 21:7; Yer 12:1; Mal 3:15Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna

nilipoona kufanikiwa kwa waovu.

4Wao hawana taabu,73:4 Tafsiri nyingine zinasema: hawana maumivu katika kufa kwao.

miili yao ina afya na nguvu.

573:5 Za 73:12; Eze 23:42Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine,

wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.

673:6 Law 26:19; Mwa 6:11; 41:42; Wim 4:9; Eze 16:11; Mit 4:17; Mhu 8:11Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao,

wamejivika jeuri.

773:7 Za 7:10Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi,

majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.

873:8 Za 10:7; 12:5; 41:5; Eze 25:15; Kol 3:8; 2Pet 2:18; Yud 16Hudhihaki na kusema kwa ukorofi,

katika majivuno yao wanatishia kutesa.

973:9 Ufu 13:6Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu,

nazo ndimi zao humiliki duniani.

10Kwa hiyo watu wao huwageukia

na kunywa maji tele.73:10 Au: na kupokea yote wasemayo.

1173:11 Ay 22:13; Za 94:7Wanasema, “Mungu awezaje kujua?

Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”

1273:12 Za 73:5; 49:6Hivi ndivyo walivyo waovu:

siku zote hawajali,

wanaongezeka katika utajiri.

1373:13 Ay 9:29-31; 21:15; Za 24:4; Mal 3:14; Mwa 44:16; Ebr 10:19-22Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure,

ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.

1473:14 Za 73:5Mchana kutwa nimetaabika,

nimeadhibiwa kila asubuhi.

15Kama ningesema, “Nitasema hivi,”

ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.

1673:16 Mhu 8:17Nilipojaribu kuelewa haya yote,

yalikuwa magumu kwangu kuelewa.

1773:17 Kut 15:17; Ay 8:13; Flp 3:19; Za 15:1; 77:13Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu,

ndipo nilipotambua mwisho wao.

1873:18 Kum 32:35; Za 35:6; 17:13Hakika unawaweka mahali pa utelezi,

unawaangusha chini kwa uharibifu.

1973:19 Kum 28:20; Mit 24:22; Isa 47:11; Mwa 19:15Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula,

wanatoweshwa kabisa na vitisho!

2073:20 Za 78:65; Isa 29:8; Ay 20:8; Mit 12:11; 28:19Kama ndoto mtu aamkapo,

hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana,

utawatowesha kama ndoto.

21Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa,

na roho yangu ilipotiwa uchungu,

2273:22 Za 49:10; 92:6; 49:12, 20; Mhu 3:18; 9:12nilikuwa mpumbavu na mjinga,

nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.

2373:23 Mwa 48:13Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote,

umenishika mkono wangu wa kuume.

2473:24 Za 48:14; 1Fal 22:5; Isa 58:8; Yn 14:3; 2Kor 5:1Unaniongoza kwa shauri lako,

hatimaye utaniingiza katika utukufu.

2573:25 Za 16:2; Flp 3:8Nani niliye naye mbinguni ila wewe?

Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.

2673:26 Kum 32:9; Za 18:1; 84:2; 31:10; 40:12Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa,

bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu

na fungu langu milele.

2773:27 Za 34:21; Law 6:2; Yer 5:11; Hos 4:12; 9:1Wale walio mbali nawe wataangamia,

unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.

2873:28 Sef 3:2; Yak 4:8; Za 40:5; 26:7; 9:9; Ebr 10:22Lakini kwangu mimi,

ni vyema kuwa karibu na Mungu.

Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu;

nami nitayasimulia matendo yako yote.

King James Version

Psalms 73:1-28

A Psalm of Asaph.

1Truly God is good to Israel, even to such as are of a clean heart.73.1 of: or, for73.1 Truly: or, Yet73.1 of…: Heb. clean of heart

2But as for me, my feet were almost gone; my steps had well nigh slipped.

3For I was envious at the foolish, when I saw the prosperity of the wicked.

4For there are no bands in their death: but their strength is firm.73.4 firm: Heb. fat

5They are not in trouble as other men; neither are they plagued like other men.73.5 in…: Heb. in the trouble of other men73.5 like: Heb. with

6Therefore pride compasseth them about as a chain; violence covereth them as a garment.

7Their eyes stand out with fatness: they have more than heart could wish.73.7 have…: Heb. pass the thoughts of the heart

8They are corrupt, and speak wickedly concerning oppression: they speak loftily.

9They set their mouth against the heavens, and their tongue walketh through the earth.

10Therefore his people return hither: and waters of a full cup are wrung out to them.

11And they say, How doth God know? and is there knowledge in the most High?

12Behold, these are the ungodly, who prosper in the world; they increase in riches.

13Verily I have cleansed my heart in vain, and washed my hands in innocency.

14For all the day long have I been plagued, and chastened every morning.73.14 chastened: Heb. my chastisement was

15If I say, I will speak thus; behold, I should offend against the generation of thy children.

16When I thought to know this, it was too painful for me;73.16 too…: Heb. labour in mine eyes

17Until I went into the sanctuary of God; then understood I their end.

18Surely thou didst set them in slippery places: thou castedst them down into destruction.

19How are they brought into desolation, as in a moment! they are utterly consumed with terrors.

20As a dream when one awaketh; so, O Lord, when thou awakest, thou shalt despise their image.

21Thus my heart was grieved, and I was pricked in my reins.

22So foolish was I, and ignorant: I was as a beast before thee.73.22 ignorant: Heb. I knew not73.22 before: Heb. with

23Nevertheless I am continually with thee: thou hast holden me by my right hand.

24Thou shalt guide me with thy counsel, and afterward receive me to glory.

25Whom have I in heaven but thee? and there is none upon earth that I desire beside thee.

26My flesh and my heart faileth: but God is the strength of my heart, and my portion for ever.73.26 strength: Heb. rock

27For, lo, they that are far from thee shall perish: thou hast destroyed all them that go a whoring from thee.

28But it is good for me to draw near to God: I have put my trust in the Lord GOD, that I may declare all thy works.