Zaburi 66 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 66:1-20

Zaburi 66

Kusifu Mungu Kwa Ajili Ya Wema Wake

Kwa mwimbishaji. Wimbo. Zaburi.

166:1 Za 81:1; 84:8; 98:4; 100:1Mpigieni Mungu kelele za shangwe, dunia yote!

266:2 Za 79:9; 86:9; Isa 42:8, 12; 43:21Imbeni utukufu wa jina lake;

mpeni sifa zake kwa utukufu!

366:3 Kum 7:21; 10:21; Za 106:22; 111:6; 18:44; 65:5; 145:6; 2Sam 22:45Mwambieni Mungu, “Jinsi gani yalivyo ya kutisha matendo yako!

Uwezo wako ni mkuu mno kiasi kwamba

adui wananyenyekea mbele zako.

466:4 Za 22:27; 7:17; 67:3Dunia yote yakusujudia,

wanakuimbia wewe sifa,

wanaliimbia sifa jina lako.”

566:5 Za 66:3; 46:8; 106:22Njooni mwone yale Mungu aliyoyatenda,

mambo ya kutisha aliyoyatenda

miongoni mwa wanadamu!

666:6 Mwa 8:1; Kut 14:21, 22; Law 23:40; Yos 3:14; Za 78:13; Isa 63:13, 14; 1Kor 10:1Alifanya bahari kuwa nchi kavu,

wakapita kati ya maji kwa miguu,

njooni, tumshangilie.

766:7 Kut 15:18; 3:16; Hes 17:10; Za 11:4; 112:10; 140:8; 145:13Yeye hutawala kwa uwezo wake milele,

macho yake huangalia mataifa yote:

waasi wasithubutu kujiinua dhidi yake.

866:8 Za 22:23Enyi mataifa, msifuni Mungu wetu,

sauti ya sifa yake isikike,

966:9 Za 30:3; Kum 32:35; Ay 12:5ameyahifadhi maisha yetu

na kuizuia miguu yetu kuteleza.

1066:10 Kut 15:25; Ay 6:29; 28:1; Za 12:6; Zek 13:9Ee Mungu, wewe ulitujaribu,

ukatusafisha kama fedha.

1166:11 Za 38:4; 142:7; 146:7; Isa 61:1; 10:27; 42:7, 22; Mwa 3:17; Kut 1:14Umetuingiza kwenye nyavu

na umetubebesha mizigo mizito

migongoni mwetu.

1266:12 Isa 51:13; Za 18:19Uliwaruhusu watu watukalie vichwani,

tulipita kwenye moto na kwenye maji,

lakini ulituleta kwenye nchi

iliyojaa utajiri tele.

1366:13 Za 51:19; 22:25; 50:14; 116:14; Mhu 5:4; Yon 2:9Nitakuja hekaluni mwako na sadaka za kuteketezwa

na kukutimizia nadhiri zangu:

14nadhiri ambazo midomo yangu iliahidi

na nilizotamka kwa kinywa changu

nilipokuwa katika shida.

1566:15 Law 16:5; Za 51:19Nitakutolea dhabihu za wanyama wanono

na sadaka za kondoo dume,

nitakutolea mafahali na mbuzi.

1666:16 Za 34:11; 71:15, 24Njooni msikilize ninyi nyote mnaomcha Mungu,

nami niwaambie aliyonitendea.

17Nilimlilia kwa kinywa changu,

sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.

1866:18 Kum 1:45; 1Sam 8:18; Yak 4:3; Isa 1:15; Ay 11:14, 15; Mit 15:29Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu,

Bwana asingekuwa amenisikiliza;

1966:19 Za 18:6lakini hakika Mungu amenisikiliza

na amesikia sauti yangu katika maombi.

2066:20 Za 22:24Sifa apewe Mungu,

ambaye hakulikataa ombi langu

wala kunizuilia upendo wake!

New Russian Translation

Псалтирь 66:1-8

Псалом 66

1Дирижеру хора. На струнных инструментах. Псалом. Песнь.

2Будь милостив к нам, Боже, и благослови нас;

озари нас лицом Своим, Пауза

3чтобы земля познала Твои пути,

все народы – Твое спасение.

4Да прославят Тебя народы, Боже;

да прославят Тебя все народы!

5Пусть племена ликуют, поют от радости,

потому что Ты судишь народы по справедливости

и управляешь племенами земли. Пауза

6Да прославят Тебя народы, Боже;

да прославят Тебя все народы!

7Земля приносит свой урожай;

да благословит нас Бог, наш Бог!

8Да благословит нас Бог,

чтобы боялись Его все концы земли.