Zaburi 66
Kusifu Mungu Kwa Ajili Ya Wema Wake
Kwa mwimbishaji. Wimbo. Zaburi.
166:1 Za 81:1; 84:8; 98:4; 100:1Mpigieni Mungu kelele za shangwe, dunia yote!
266:2 Za 79:9; 86:9; Isa 42:8, 12; 43:21Imbeni utukufu wa jina lake;
mpeni sifa zake kwa utukufu!
366:3 Kum 7:21; 10:21; Za 106:22; 111:6; 18:44; 65:5; 145:6; 2Sam 22:45Mwambieni Mungu, “Jinsi gani yalivyo ya kutisha matendo yako!
Uwezo wako ni mkuu mno kiasi kwamba
adui wananyenyekea mbele zako.
466:4 Za 22:27; 7:17; 67:3Dunia yote yakusujudia,
wanakuimbia wewe sifa,
wanaliimbia sifa jina lako.”
566:5 Za 66:3; 46:8; 106:22Njooni mwone yale Mungu aliyoyatenda,
mambo ya kutisha aliyoyatenda
miongoni mwa wanadamu!
666:6 Mwa 8:1; Kut 14:21, 22; Law 23:40; Yos 3:14; Za 78:13; Isa 63:13, 14; 1Kor 10:1Alifanya bahari kuwa nchi kavu,
wakapita kati ya maji kwa miguu,
njooni, tumshangilie.
766:7 Kut 15:18; 3:16; Hes 17:10; Za 11:4; 112:10; 140:8; 145:13Yeye hutawala kwa uwezo wake milele,
macho yake huangalia mataifa yote:
waasi wasithubutu kujiinua dhidi yake.
866:8 Za 22:23Enyi mataifa, msifuni Mungu wetu,
sauti ya sifa yake isikike,
966:9 Za 30:3; Kum 32:35; Ay 12:5ameyahifadhi maisha yetu
na kuizuia miguu yetu kuteleza.
1066:10 Kut 15:25; Ay 6:29; 28:1; Za 12:6; Zek 13:9Ee Mungu, wewe ulitujaribu,
ukatusafisha kama fedha.
1166:11 Za 38:4; 142:7; 146:7; Isa 61:1; 10:27; 42:7, 22; Mwa 3:17; Kut 1:14Umetuingiza kwenye nyavu
na umetubebesha mizigo mizito
migongoni mwetu.
1266:12 Isa 51:13; Za 18:19Uliwaruhusu watu watukalie vichwani,
tulipita kwenye moto na kwenye maji,
lakini ulituleta kwenye nchi
iliyojaa utajiri tele.
1366:13 Za 51:19; 22:25; 50:14; 116:14; Mhu 5:4; Yon 2:9Nitakuja hekaluni mwako na sadaka za kuteketezwa
na kukutimizia nadhiri zangu:
14nadhiri ambazo midomo yangu iliahidi
na nilizotamka kwa kinywa changu
nilipokuwa katika shida.
1566:15 Law 16:5; Za 51:19Nitakutolea dhabihu za wanyama wanono
na sadaka za kondoo dume,
nitakutolea mafahali na mbuzi.
1666:16 Za 34:11; 71:15, 24Njooni msikilize ninyi nyote mnaomcha Mungu,
nami niwaambie aliyonitendea.
17Nilimlilia kwa kinywa changu,
sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.
1866:18 Kum 1:45; 1Sam 8:18; Yak 4:3; Isa 1:15; Ay 11:14, 15; Mit 15:29Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu,
Bwana asingekuwa amenisikiliza;
1966:19 Za 18:6lakini hakika Mungu amenisikiliza
na amesikia sauti yangu katika maombi.
2066:20 Za 22:24Sifa apewe Mungu,
ambaye hakulikataa ombi langu
wala kunizuilia upendo wake!
Псалом 66
1Дирижеру хора. На струнных инструментах. Псалом. Песнь.
2Будь милостив к нам, Боже, и благослови нас;
озари нас лицом Своим, Пауза
3чтобы земля познала Твои пути,
все народы – Твое спасение.
4Да прославят Тебя народы, Боже;
да прославят Тебя все народы!
5Пусть племена ликуют, поют от радости,
потому что Ты судишь народы по справедливости
и управляешь племенами земли. Пауза
6Да прославят Тебя народы, Боже;
да прославят Тебя все народы!
7Земля приносит свой урожай;
да благословит нас Бог, наш Бог!
8Да благословит нас Бог,
чтобы боялись Его все концы земли.