Zaburi 64 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 64:1-10

Zaburi 64

Kuomba Ulinzi Dhidi Ya Maadui

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

164:1 Za 142:2; 140:1Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu,

uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.

264:2 Za 56:6; 59:2; 143:9; Kut 1:10Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu,

kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.

364:3 Za 7:13; 58:7; 57:4; 55:21; Isa 49:2Wananoa ndimi zao kama panga

na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.

464:4 Za 10:8; 11:2; 55:19; Ay 9:23Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia,

humrushia ghafula bila woga.

564:5 Za 91:3; 140:5; 119:110; 141:9; Ay 22:13Kila mmoja humtia moyo mwenzake

katika mipango mibaya;

huzungumza juu ya kuficha mitego yao,

nao husema, “Ni nani ataiona?”

6Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema,

“Tumebuni mpango mkamilifu!”

Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.

7Bali Mungu atawapiga kwa mishale,

nao ghafula wataangushwa.

864:8 Mit 12:13; 18:7; 2Fal 10:21; Za 109:25; 59:12; Kum 28:37Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao

na kuwaleta kwenye maangamizi;

wote wawaonao watatikisa vichwa vyao

kwa dharau.

964:9 Za 40:3; Yer 51:10Wanadamu wote wataogopa,

watatangaza kazi za Mungu

na kutafakari yale aliyoyatenda.

1064:10 Ay 22:19Wenye haki na wafurahi katika Bwana,

na wakimbilie kwake;

wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

King James Version

Psalms 64:1-10

To the chief Musician, A Psalm of David.

1Hear my voice, O God, in my prayer: preserve my life from fear of the enemy.

2Hide me from the secret counsel of the wicked; from the insurrection of the workers of iniquity:

3Who whet their tongue like a sword, and bend their bows to shoot their arrows, even bitter words:

4That they may shoot in secret at the perfect: suddenly do they shoot at him, and fear not.

5They encourage themselves in an evil matter: they commune of laying snares privily; they say, Who shall see them?64.5 matter: or, speech64.5 of…: Heb. to hide his snares

6They search out iniquities; they accomplish a diligent search: both the inward thought of every one of them, and the heart, is deep.64.6 they…: or, we are consumed by that which they have throughly searched64.6 a diligent…: Heb. a search searched

7But God shall shoot at them with an arrow; suddenly shall they be wounded.64.7 shall they…: Heb. their wound shall be

8So they shall make their own tongue to fall upon themselves: all that see them shall flee away.

9And all men shall fear, and shall declare the work of God; for they shall wisely consider of his doing.

10The righteous shall be glad in the LORD, and shall trust in him; and all the upright in heart shall glory.