Zaburi 62 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 62:1-12

Zaburi 62

Mungu Kimbilio La Pekee

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa Yeduthuni. Zaburi ya Daudi.

162:1 Za 5:3Kwa Mungu peke yake nafsi yangu inapata pumziko;

wokovu wangu watoka kwake.

262:2 Kut 15:2; Za 18:31; 89:26; 59:9; Ay 29:18Yeye peke yake ndiye mwamba wangu na wokovu wangu;

yeye ni ngome yangu, sitatikisika kamwe.

362:3 Isa 30:13Mtamshambulia mtu hata lini?

Je, ninyi nyote mtamtupa chini,

ukuta huu ulioinama na uzio huu unaotikisika?

462:4 Za 28:3; 55:21Walikusudia kikamilifu kumwangusha

toka mahali pake pa fahari;

wanafurahia uongo.

Kwa vinywa vyao hubariki,

lakini ndani ya mioyo yao hulaani.

562:5 Mik 7:7, 10; Za 62:1Ee nafsi yangu, upumzike, kwa Mungu peke yake,

tumaini langu latoka kwake.

6Yeye peke yake ndiye mwamba wangu na wokovu wangu;

ndiye ngome yangu, sitatikisika.

762:7 Za 61:3Wokovu wangu na heshima yangu viko kwa Mungu,

ndiye mwamba wangu wenye nguvu

na kimbilio langu.

862:8 Isa 26:4; 1Sam 1:15; Za 37:5; 42:4; Mt 26:36-46Enyi watu, mtumainini yeye wakati wote,

miminieni mioyo yenu kwake,

kwa kuwa Mungu ni kimbilio letu.

962:9 Za 49:2; Ay 7:7; Isa 40:15Binadamu wa ngazi ya chini ni pumzi tu,

nao wa ngazi ya juu ni uongo tu;

wakipimwa kwenye mizani, si chochote;

wote kwa pamoja ni pumzi tu.

1062:10 Za 12:5; Isa 61:8; 26:4; 1Tim 6:17; Eze 22:29; Nah 3:1; Lk 12:15; Ay 31:25; Mt 19:23, 24; 1Tim 6:6-10; Mk 10:23Usitumainie vya udhalimu

wala usijivune kwa vitu vya wizi;

ingawa utajiri wako utaongezeka,

usiviwekee moyo wako.

1162:11 1Nya 29:11; Ufu 19:1Jambo moja Mungu amelisema,

mambo mawili nimeyasikia:

kwamba, Ee Mungu,

wewe una nguvu,

1262:12 Za 130:7; 103:8; 86:5; 28:4; Ay 21:31; Mt 16:27; Rum 2:6; 1Kor 3:8; Kol 3:25; 1Pet 1:17na kwamba, Ee Bwana,

wewe ni mwenye upendo.

Hakika utampa kila mtu thawabu

kwa kadiri ya alivyotenda.

Hoffnung für Alle

Psalm 62:1-13

Bei Gott komme ich zur Ruhe

1Ein Lied von David. Für Jedutun.

2Nur bei Gott komme ich zur Ruhe;

geduldig warte ich auf seine Hilfe.

3Nur er ist ein schützender Fels und eine sichere Burg.

Er steht mir bei, und niemand kann mich zu Fall bringen.

4Wie lange noch wollt ihr euch alle über einen hermachen

und ihm den letzten Stoß versetzen

wie einer Wand, die sich schon bedrohlich neigt,

oder einer Mauer, die bereits einstürzt?

5Ja, sie unternehmen alles,

um meinen guten Namen in den Dreck zu ziehen.

Es macht ihnen Freude, Lügen über mich zu verbreiten.

Wenn sie mit mir reden, sprechen sie Segenswünsche aus,

doch im Herzen verfluchen sie mich.

6Nur bei Gott komme ich zur Ruhe;

er allein gibt mir Hoffnung.

7Nur er ist ein schützender Fels und eine sichere Burg.

Er steht mir bei, und niemand kann mich zu Fall bringen.

8Gott rettet mich, er steht für meine Ehre ein.

Er schützt mich wie ein starker Fels,

bei ihm bin ich geborgen.

9Ihr Menschen, vertraut ihm jederzeit

und schüttet euer Herz bei ihm aus!

Gott ist unsere Zuflucht.

10Die Menschen vergehen wie ein Hauch;

ob einfach oder vornehm – sie sind wie ein Trugbild, das verschwindet.

Legt man sie auf die Waagschale, dann schnellt sie nach oben,

als wären die Menschen nur Luft.

11Verlasst euch nicht auf erpresstes Gut,

lasst euch nicht blenden von unrecht erworbenem Reichtum!

Wenn euer Wohlstand wächst,

dann hängt euer Herz nicht daran!

12Mehr als einmal habe ich gehört,

wie Gott gesagt hat:

»Ich allein habe alle Macht!«

13Du, Herr, bist ein gnädiger Gott;

du vergiltst jedem, wie er es verdient.