Zaburi 55
Maombi Ya Mtu Aliyesalitiwa Na Rafiki
Kwa mwimbishaji. Na ala za uimbaji. Utenzi wa Daudi.
155:1 Za 27:9; Mao 3:56Ee Mungu, sikiliza maombi yangu,
wala usidharau hoja yangu.
255:2 1Sam 1:15-16; Za 4:1; 77:3; 86:6-7; 142:2Nisikie na unijibu.
Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa
355:3 2Sam 16:6-8; 17:9; Za 143:3; 44:16; 71:11kwa sauti ya adui,
kwa kukaziwa macho na waovu,
kwa sababu wananiletea mateso juu yangu
na kunitukana kwa hasira zao.
455:4 Ay 18:11; Za 6:3; 102:3-5; Yn 12:27; Mt 26:37, 38; 2Kor 1:8-10Moyo wangu umejaa uchungu,
hofu ya kifo imenishambulia.
555:5 Ay 4:14; Eze 7:18; 2Kor 7:15; Isa 21:4; Kum 28:67; Yer 46:5; 49:5Woga na kutetemeka vimenizunguka,
hofu kuu imenigharikisha.
6Nilisema, “Laiti ningekuwa na mbawa za njiwa!
Ningeruka niende mbali kupumzika.
755:7 1Sam 23:14Ningalitorokea mbali sana
na kukaa jangwani,
855:8 Za 31:20; 77:18; Isa 4:6; 25:4; 28:2; 29:6; 32:2ningaliharakisha kwenda mahali pa salama,
mbali na tufani kali na dhoruba.”
955:9 Mwa 4:17; 11:9; Mdo 2:4; Za 11:5; Isa 59:6; Yer 6:7; Eze 7:11; Hab 1:3Ee Bwana, uwatahayarishe waovu
na uwachanganyishie semi zao,
maana nimeona jeuri na ugomvi mjini.
1055:10 1Pet 5:8Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake,
uovu na dhuluma vimo ndani yake.
1155:11 Za 5:9; 10:7Nguvu za uharibifu zinatenda kazi mjini,
vitisho na uongo haviondoki mitaani mwake.
12Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia,
kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu,
ningejificha asinione.
1355:13 2Sam 15:12Kumbe ni wewe, mwenzangu,
mshiriki na rafiki yangu wa karibu,
1455:14 Mdo 1:16-17; Za 42:4ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri,
tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu.
1555:15 Za 64:7; 49:14; Mit 6:5; Isa 29:5; 47:9, 11; 1The 5:3; Hes 16:30Kifo na kiwajie adui zangu ghafula,
na washuke kuzimu wangali hai,
kwa maana uovu upo ndani yao.
16Lakini ninamwita Mungu,
naye Bwana huniokoa.
1755:17 Za 141:2; 88:13; 92:2; 5:3; Mdo 3:1; 10:9; 10:3, 30; Lk 18:1; Dan 6:10Jioni, asubuhi na adhuhuri
ninalia kwa huzuni,
naye husikia sauti yangu.
1855:18 2Nya 32:7Huniokoa nikawa salama katika vita
vilivyopangwa dhidi yangu,
ingawa watu wengi hunipinga.
1955:19 Kum 33:27; Za 29:10; 78:59; 36:1; 64:4; Kut 15:18Mungu anayemiliki milele,
atawasikia na kuwaadhibu,
watu ambao hawabadilishi njia zao,
wala hawana hofu ya Mungu.
2055:20 Za 7:4; 41:9Mwenzangu hushambulia rafiki zake,
naye huvunja agano lake.
2155:21 Za 59:7; 57:4; 12:2; 64:3; Ufu 1:16; Mit 5:3; 6:24; 12:18Mazungumzo yake ni laini kama siagi,
hata hivyo vita vimo moyoni mwake.
Maneno yake ni mororo kuliko mafuta,
hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa.
2255:22 1Pet 5:7; Za 15:5; 18:35; 112:6; 21:7; 37:24; Mt 6:25-34Mtwike Bwana fadhaa zako,
naye atakutegemeza,
hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke.
2355:23 Za 5:6; 11:1; 9:15; 73:18; 94:13; 25:2; 30:3; 56:3; Isa 14:15; Eze 28:8; Lk 8:31; Ay 15:32Lakini wewe, Ee Mungu,
utawashusha waovu katika shimo la uharibifu.
Wenye kiu ya kumwaga damu na wenye hila,
hawataishi nusu ya siku zao.
Lakini mimi ninakutumaini wewe.
第 55 篇
被朋友出卖者的祷告
大卫作的训诲诗,交给乐长,用弦乐器。
1上帝啊,
求你垂听我的祷告,
不要对我的呼求置之不理。
2求你垂听、应允我的呼求。
我思绪烦乱,坐立不安。
3仇敌向我咆哮,
恶人迫害我。
他们带给我苦难,
怒气冲冲地辱骂我。
4我内心悲痛,
被死亡的恐怖笼罩。
5我浑身颤栗,惊恐不已。
6啊,但愿我能像鸽子展翅飞去,
得享安息。
7我要飞到远方,住在旷野。(细拉)
8我要赶快躲进避难所,
避过暴雨狂风。
9主啊,
我在城中看见暴力和争斗,
求你使他们言语混乱。
10他们昼夜在城墙上出没,
城内充满了邪恶和压迫,
11毁坏的势力到处肆虐,
恐吓与欺诈遍布大街小巷。
12倘若是仇敌辱骂我,
我还能忍受;
倘若是恨我的人欺凌我,
我还可以躲开。
13可是,竟然是你——我志同道合的伙伴,我的挚友!
14从前我们情谊深厚,
与众人同去上帝的殿。
15愿死亡突然抓住我的仇敌,
愿他们活活地下阴间,
因为他们的内心和家中罪恶充斥。
16但我要呼求耶和华上帝,
祂必拯救我。
17晚上、早晨和中午,
我发出痛苦的呼求,
祂必垂听。
18虽然许多人攻击我,
祂必救我平安脱离险境。
19永掌王权的上帝必鉴察并惩罚他们,
因为他们顽梗悖逆、不敬畏上帝。
20我的同伴违背盟约,攻击朋友。
21他口蜜腹剑,笑里藏刀。
22把你的重担卸给耶和华,
祂必扶持你。
祂必不让义人跌倒。
23上帝啊,
你必把恶人送进灭亡的坑里。
嗜血成性的骗子必早早夭亡。
但我要信靠你。