Zaburi 53 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 53:1-6

Zaburi 53

Uovu Wa Wanadamu

(Zaburi 14)

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi.

153:1 Za 107:17; 74:22; 10:4; Mit 10:23; Rum 3:10Mpumbavu anasema moyoni mwake,

“Hakuna Mungu.”

Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa,

hakuna hata mmoja atendaye mema.

253:2 Za 33:13; 82:5; Yer 4:22; 8:8; 2Nya 15:2Mungu anawachungulia wanadamu chini

kutoka mbinguni

aone kama wako wenye akili,

wowote wanaomtafuta Mungu.

353:3 Rum 3:10-12; Mhu 7:29Kila mmoja amegeukia mbali,

wameharibika wote pamoja,

hakuna atendaye mema.

Naam, hakuna hata mmoja!

453:4 Yer 4:22Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza:

wale ambao huwala watu wangu

kama watu walavyo mkate,

hao ambao hawamwiti Mungu?

553:5 Law 26:17; Eze 6:5; 2Fal 17:20; 23:14; Za 141:7; Mao 5:22; Yer 6:30; 14:19; 8:1; Ay 8:22Hapo waliingiwa na hofu kuu,

ambapo hapakuwa cha kutetemesha.

Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia;

uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.

6Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni!

Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake,

Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!

King James Version

Psalms 53:1-6

To the chief Musician upon Mahalath, Maschil, A Psalm of David.

1The fool hath said in his heart, There is no God. Corrupt are they, and have done abominable iniquity: there is none that doeth good.53.1 Maschil: or, of instruction

2God looked down from heaven upon the children of men, to see if there were any that did understand, that did seek God.

3Every one of them is gone back: they are altogether become filthy; there is none that doeth good, no, not one.

4Have the workers of iniquity no knowledge? who eat up my people as they eat bread: they have not called upon God.

5There were they in great fear, where no fear was: for God hath scattered the bones of him that encampeth against thee: thou hast put them to shame, because God hath despised them.53.5 were…: Heb. they feared a fear

6Oh that the salvation of Israel were come out of Zion! When God bringeth back the captivity of his people, Jacob shall rejoice, and Israel shall be glad.53.6 Oh that…: Heb. Who will give salvation, etc