Zaburi 49 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 49:1-20

Zaburi 49

Upumbavu Wa Kutegemea Mali

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora.

149:1 Isa 1:2; Za 33:8; 78:1Sikieni haya, enyi mataifa yote,

sikilizeni, ninyi wote mkaao dunia hii.

249:2 Za 62:9Wakubwa kwa wadogo,

matajiri na maskini pamoja:

349:3 Za 37:30; 119:130Kinywa changu kitasema maneno ya hekima,

usemi wa moyo wangu utatoa ufahamu.

449:4 Za 33:2; 78:2; 1Sam 16:16; Mit 1:6; Eze 12:22; 16:44; 18:2, 3; Hes 12:8; Lk 4:23Nitatega sikio langu nisikilize mithali,

nitafafanua kitendawili kwa zeze:

549:5 Za 23:4; 27:1Kwa nini niogope siku mbaya zinapokuja,

wakati wadanganyifu waovu wanaponizunguka,

649:6 Yer 48:7; Za 10:3; 73:12; Ay 22:25; 36:19wale wanaotegemea mali zao

na kujivunia utajiri wao mwingi?

749:7 Mt 16:26Hakuna mwanadamu awaye yote

awezaye kuukomboa uhai wa mwingine,

au kumpa Mungu fidia kwa ajili yake.

849:8 Hes 35:31; Mt 16:26; Ay 36:18Fidia ya uhai ni gharama kubwa,

hakuna malipo yoyote yanayotosha,

949:9 Za 22:29; 89:48; 16:10; Ebr 9:27ili kwamba aishi milele

na asione uharibifu.

1049:10 Mhu 2:16, 18, 21; Za 92:6; 94:8; Ay 27:17; Lk 12:20Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa;

wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia

na kuwaachia wengine mali zao.

1149:11 Mk 5:3; Lk 8:27; Za 106:31; Kum 3:14Makaburi yao yatabaki kuwa nyumba zao za milele,

makao yao vizazi vyote;

ingawa walikuwa na mashamba

na kuyaita kwa majina yao.

1249:12 Ay 14:2Lakini mwanadamu, licha ya utajiri wake, hadumu;

anafanana na mnyama aangamiaye.

1349:13 Lk 12:20Hii ndiyo hatima ya wale wanaojitumainia wenyewe,

pia ya wafuasi wao, waliothibitisha misemo yao.

1449:14 Yer 43:11; Isa 14:2; Hes 16:30; Eze 31:14; Mal 4:3; Ay 21:13; Ufu 2:26; 1Kor 6:2; Za 9:17; 55:15; Dan 7:18, 22; Lk 22:30; 2Tim 2:12Kama kondoo, wamewekewa kwenda kaburini,49:14 Kaburini hapa ina maana ya Sheol kwa Kiebrania, yaani Kuzimu.

nacho kifo kitawala.

Wanyofu watawatawala asubuhi,

maumbile yao yataozea kaburini,

mbali na majumba yao makubwa ya fahari.

1549:15 Za 56:13; Hos 13:14; Mwa 5:24Lakini Mungu atakomboa uhai49:15 Au: nafsi. wangu na kaburi,

hakika atanichukua kwake.

16Usitishwe mtu anapotajirika,

fahari ya nyumba yake inapoongezeka,

1749:17 1Tim 6:7; Za 17:14kwa maana hatachukua chochote atakapokufa,

fahari yake haitashuka pamoja naye.

1849:18 Za 10:6; Lk 12:19Ingawa alipokuwa akiishi alijihesabu kuwa heri,

na wanadamu wanakusifu unapofanikiwa,

1949:19 Mwa 15:15; Ay 33:30atajiunga na kizazi cha baba zake,

ambao hawataona kamwe nuru ya uzima.

2049:20 Mit 16:16; Mhu 3:19-21Mwanadamu mwenye utajiri bila ufahamu

ni kama wanyama waangamiao.

New International Version

Psalms 49:1-20

Psalm 49In Hebrew texts 49:1-20 is numbered 49:2-21.

For the director of music. Of the Sons of Korah. A psalm.

1Hear this, all you peoples;

listen, all who live in this world,

2both low and high,

rich and poor alike:

3My mouth will speak words of wisdom;

the meditation of my heart will give you understanding.

4I will turn my ear to a proverb;

with the harp I will expound my riddle:

5Why should I fear when evil days come,

when wicked deceivers surround me—

6those who trust in their wealth

and boast of their great riches?

7No one can redeem the life of another

or give to God a ransom for them—

8the ransom for a life is costly,

no payment is ever enough—

9so that they should live on forever

and not see decay.

10For all can see that the wise die,

that the foolish and the senseless also perish,

leaving their wealth to others.

11Their tombs will remain their houses49:11 Septuagint and Syriac; Hebrew In their thoughts their houses will remain forever,

their dwellings for endless generations,

though they had49:11 Or generations, / for they have named lands after themselves.

12People, despite their wealth, do not endure;

they are like the beasts that perish.

13This is the fate of those who trust in themselves,

and of their followers, who approve their sayings.49:13 The Hebrew has Selah (a word of uncertain meaning) here and at the end of verse 15.

14They are like sheep and are destined to die;

death will be their shepherd

(but the upright will prevail over them in the morning).

Their forms will decay in the grave,

far from their princely mansions.

15But God will redeem me from the realm of the dead;

he will surely take me to himself.

16Do not be overawed when others grow rich,

when the splendor of their houses increases;

17for they will take nothing with them when they die,

their splendor will not descend with them.

18Though while they live they count themselves blessed—

and people praise you when you prosper—

19they will join those who have gone before them,

who will never again see the light of life.

20People who have wealth but lack understanding

are like the beasts that perish.