Zaburi 45 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 45:1-17

Zaburi 45

Wimbo Wa Arusi Ya Kifalme

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi.

1Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema

ninapomsimulia mfalme mabeti yangu;

ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.

245:2 Lk 4:22; Za 21:6Wewe ni bora kuliko watu wengine wote

na midomo yako imepakwa neema,

kwa kuwa Mungu amekubariki milele.

345:3 Kum 32:41; Ufu 1:16; Za 21:5; 149:6; 2Sam 1:19; Ay 40:10Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu,

jivike fahari na utukufu.

445:4 Ufu 6:2; Sef 2:3; Za 21:8; 65:5; 66:3; Kum 4:34Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi,

kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki,

mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.

545:5 Kum 32:23; Hes 24:8; Isa 50:10; Za 56:3, 11; 9:13; 92:9; Mao 3:24Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme,

mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.

645:6 Mwa 21:33; Mao 5:13; Za 93:2; Isa 9:6, 7; Ebr 1:8Ee Mungu, kiti chako cha enzi

kitadumu milele na milele,

fimbo ya utawala wa haki

itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.

745:7 Za 33:5; 11:5; 2:2; 23:5; Ebr 1:9; Eze 7:26; Isa 45:1; 61:1; Yn 20:17; Mt 3:15; Zek 4:14Unaipenda haki na kuchukia uovu;

kwa hiyo Mungu, Mungu wako,

amekuweka juu ya wenzako,

kwa kukupaka mafuta ya furaha.

845:8 Kum 28:8; Wim 1:3; 4:10; Mwa 37:25; Hes 24:6; Yn 19:39; Kut 30:24; 1Fal 22:39; Za 144:9; 150:4; Isa 38:20; Mt 27:9Mavazi yako yote yana harufu nzuri

ya manemane, udi na mdalasini;

kutoka kwenye majumba ya kifalme

yaliyopambwa kwa pembe za ndovu,

sauti za vinanda vya nyuzi

zinakufanya ufurahi.

945:9 Wim 6:8; Isa 62:5; Mwa 10:29; 1Fal 2:19Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa;

kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.

1045:10 Yer 5:1; Rut 1:11; 1:16; Kum 21:13Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio:

Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.

1145:11 Mao 2:15; Efe 5:33; Isa 54:5; Za 95:6; Es 1:11Mfalme ameshangazwa na uzuri wako;

mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.

1245:12 Yos 19:29; 1Fal 9:16; 2Nya 9:24Binti wa Tiro atakuletea zawadi,

watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.

1345:13 Isa 61:10; Kut 39:3; Ufu 19:7, 8Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake;

vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.

1445:14 Amu 5:30; Es 2:15; Wim 1:3Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa,

mabikira wenzake wanamfuata

na wanaletwa kwako.

1545:15 Es 8:17Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha,

na kuingia katika jumba la mfalme.

1645:16 1Sam 2:8; Za 68:27; 113:8; 1Pet 2:9; Ufu 1:6Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu,

mtawafanya wakuu katika nchi yote.

1745:17 Isa 11:10; Mal 1:11; Kut 3:15; Ufu 22:5; Za 33:11; 138:4; 119:90; 135:13Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote,

kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

诗篇 45:1-17

第 45 篇

婚礼诗歌

可拉后裔作的训诲诗,也是婚礼上唱的情歌,交给乐长,调用“百合花”。

1我心中涌出美丽的诗章,

我要把它献给王,

我的舌头是诗人手上的妙笔。

2你俊美无比,口出恩言,

因此上帝永远赐福给你。

3伟大的王啊,

佩上你的宝剑,

你是何等尊贵、威严!

4你威严无比,所向披靡,

捍卫真理和正义,

保护卑微的人。

愿你的右手彰显可畏的作为!

5你的利箭刺穿敌人的心窝,

列国臣服在你脚下。

6上帝啊,你的宝座永远长存,

你以公义的杖执掌王权。

7你喜爱公义,憎恶邪恶,

因此上帝,你的上帝,

用喜乐之油膏你,

使你超过同伴。

8你的衣袍散发出没药、沉香和肉桂的芬芳,

你陶醉在象牙宫的弦乐中。

9众公主在你的贵客中,

俄斐金饰的王后站在你右边。

10女子啊,

要侧耳倾听:不要再挂念家乡的父老,

11王喜欢你的美貌,

你要敬重他,因他是你的主。

12泰尔人必来送礼,

富人必来取悦你。

13公主身穿金线衣,无比华贵。

14她身披锦绣,

由侍女伴随前来见王,

15她们欢喜快乐地进入王宫。

16你的子孙将来要继承祖先的王位,

你要立他们在各地做王。

17我要使你的名世代受尊崇,

万民必永远称谢你。