Zaburi 45 – Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu) NEN

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 45:1-17

Zaburi 45

Wimbo Wa Arusi Ya Kifalme

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi.

1Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema

ninapomsimulia mfalme mabeti yangu;

ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.

245:2 Lk 4:22; Za 21:6Wewe ni bora kuliko watu wengine wote

na midomo yako imepakwa neema,

kwa kuwa Mungu amekubariki milele.

345:3 Kum 32:41; Ufu 1:16; Za 21:5; 149:6; 2Sam 1:19; Ay 40:10Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu,

jivike fahari na utukufu.

445:4 Ufu 6:2; Sef 2:3; Za 21:8; 65:5; 66:3; Kum 4:34Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi,

kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki,

mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.

545:5 Kum 32:23; Hes 24:8; Isa 50:10; Za 56:3, 11; 9:13; 92:9; Mao 3:24Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme,

mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.

645:6 Mwa 21:33; Mao 5:13; Za 93:2; Isa 9:6, 7; Ebr 1:8Ee Mungu, kiti chako cha enzi

kitadumu milele na milele,

fimbo ya utawala wa haki

itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.

745:7 Za 33:5; 11:5; 2:2; 23:5; Ebr 1:9; Eze 7:26; Isa 45:1; 61:1; Yn 20:17; Mt 3:15; Zek 4:14Unaipenda haki na kuchukia uovu;

kwa hiyo Mungu, Mungu wako,

amekuweka juu ya wenzako,

kwa kukupaka mafuta ya furaha.

845:8 Kum 28:8; Wim 1:3; 4:10; Mwa 37:25; Hes 24:6; Yn 19:39; Kut 30:24; 1Fal 22:39; Za 144:9; 150:4; Isa 38:20; Mt 27:9Mavazi yako yote yana harufu nzuri

ya manemane, udi na mdalasini;

kutoka kwenye majumba ya kifalme

yaliyopambwa kwa pembe za ndovu,

sauti za vinanda vya nyuzi

zinakufanya ufurahi.

945:9 Wim 6:8; Isa 62:5; Mwa 10:29; 1Fal 2:19Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa;

kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.

1045:10 Yer 5:1; Rut 1:11; 1:16; Kum 21:13Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio:

Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.

1145:11 Mao 2:15; Efe 5:33; Isa 54:5; Za 95:6; Es 1:11Mfalme ameshangazwa na uzuri wako;

mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.

1245:12 Yos 19:29; 1Fal 9:16; 2Nya 9:24Binti wa Tiro atakuletea zawadi,

watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.

1345:13 Isa 61:10; Kut 39:3; Ufu 19:7, 8Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake;

vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.

1445:14 Amu 5:30; Es 2:15; Wim 1:3Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa,

mabikira wenzake wanamfuata

na wanaletwa kwako.

1545:15 Es 8:17Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha,

na kuingia katika jumba la mfalme.

1645:16 1Sam 2:8; Za 68:27; 113:8; 1Pet 2:9; Ufu 1:6Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu,

mtawafanya wakuu katika nchi yote.

1745:17 Isa 11:10; Mal 1:11; Kut 3:15; Ufu 22:5; Za 33:11; 138:4; 119:90; 135:13Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote,

kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.