Zaburi 44 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 44:1-26

Zaburi 44

Kuomba Ulinzi Wa Mungu

Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora.

144:1 2Sam 7:22; 1Nya 17:20; Yer 26:11; Amu 6:13; Kum 32:7; Ay 37:23Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu,

baba zetu wametueleza

yale uliyotenda katika siku zao,

siku za kale.

244:2 Kut 15:17; Kum 7:1; Yos 10:42; 3:10; Mdo 7:45; Isa 60:21; Amu 4:23; 2Nya 14:13; Za 80:9; Yer 32:23Kwa mkono wako uliwafukuza mataifa

na ukawapanda baba zetu,

uliangamiza mataifa

na kuwastawisha baba zetu.

344:3 Yos 24:12; Kut 15:16; Za 78:54; 77:15; 79:11; 89:10, 15; Isa 40:10; 52:10; 63:5; Kum 4:37Sio kwa upanga wao waliipata nchi,

wala si mkono wao uliwapatia ushindi;

ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume,

na nuru ya uso wako,

kwa kuwa uliwapenda.

444:4 Za 24:7; 5:2; 21:5; 74:12Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu,

unayeamuru ushindi kwa Yakobo.

544:5 Yos 23:5; Za 60:12; 108:13; Dan 8:10Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu;

kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.

644:6 Za 33:16; Hos 1:7; Mwa 48:22Siutumaini upinde wangu,

upanga wangu hauniletei ushindi;

744:7 Kum 20:4; Ay 8:2bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu,

unawaaibisha watesi wetu.

844:8 1Kor 1:3; Rum 2:17; Za 34:2; 52:1; 30:12; 2Kor 10:17Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa,

nasi tutalisifu jina lako milele.

944:9 Kum 8:3; 31:17; Za 43:2; 107:39; 108:11; Isa 5:15; Yos 7:12Lakini sasa umetukataa na kutudhili,

wala huendi tena na jeshi letu.

1044:10 Law 26:17; Amu 2:14; Kum 28:25Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui,

nao watesi wetu wametuteka nyara.

1144:11 Yer 12:3; 32:37; Law 26:33; Zek 2:6; Kum 4:27; Eze 6:8; Lk 21:24; Za 9:11; 60:1; 2Fal 17:6Umetuacha tutafunwe kama kondoo

na umetutawanya katika mataifa.

1244:12 Kum 32:30; Isa 50:1; 52:3; Yer 15:13Umewauza watu wako kwa fedha kidogo,

wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao.

1344:13 2Nya 29:8; Isa 30:3; Yer 25:9; 42:18; 44:8; Kum 28:37; Mik 2:6; Za 79:4; 80:6; 89:41; Eze 23:32Umetufanya lawama kwa jirani zetu,

dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka.

1444:14 1Fal 9:7; 2Fal 19:21Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa,

mataifa hutikisa vichwa vyao.

1544:15 Mwa 30:23; 2Nya 32:21; Za 35:26; 34:5Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa,

na uso wangu umejaa aibu tele,

1644:16 Za 42:10; 10:13; 55:3; 74:10; 1Sam 18:25; Yer 11:19; Rum 12:19kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana,

kwa sababu ya adui, ambaye anatamani kulipiza kisasi.

1744:17 Kum 6:12; 32:18; Mit 3:1; Dan 9:13; Za 119:16, 61, 153, 176Hayo yote yametutokea,

ingawa tulikuwa hatujakusahau

wala hatujaenda kinyume na agano lako.

1844:18 Za 119:51, 157Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma;

nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako.

1944:19 2Nya 14:13; Za 51:8; Isa 43:12; Ay 30:29; 3:5Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha,

na ukatufunika kwa giza nene.

2044:20 Kum 32:18; Amu 4:7; Isa 43:12; Kut 20:3; Yer 5:12Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu

au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni,

2144:21 1Sam 16:7; 1Fal 8:39; Yn 2:25; Mit 15:11; Yer 12:3; 17:10; Ay 31:14; Za 139:1; Mhu 12:14; Mdo 1:24; Ufu 2:23; Rum 2:16; Ebr 4:12je, Mungu hangaligundua hili,

kwa kuwa anazijua siri za moyo?

2244:22 Yer 11:19; 12:3; Isa 53:7; Rum 8:36Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa;

tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.

2344:23 Za 7:6; 78:65; 59:5; 74:1; 77:7Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala?

Zinduka! Usitukatae milele.

2444:24 Mao 5:20Kwa nini unauficha uso wako

na kusahau taabu na mateso yetu?

2544:25 Za 119:25Tumeshushwa hadi mavumbini,

miili yetu imegandamana na ardhi.

2644:26 Za 102:13; 26:11; 12:5; 6:4; Hes 10:25Inuka na utusaidie,

utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.

Ketab El Hayat

مزمور 44:1-26

الْمَزْمُورُ الرَّابِعُ وَالأَرْبَعُونَ

لِقَائِدِ الْمُنْشِدِينَ، مَزْمُورٌ تَعْلِيمِيٌّ لِبَنِي قُورَحَ

1يَا اللهُ، بِآذَانِنَا قَدْ سَمِعْنَا، وَآبَاؤُنَا أَخْبَرُونَا بِمَا عَمِلْتَهُ فِي أَيَّامِهِمِ الْقَدِيمَةِ. 2بِيَدِكَ اقْتَلَعْتَ الأُمَمَ، وَغَرَسْتَ آبَاءَنَا. حَطَّمْتَ الشُّعُوبَ وَأَنْمَيْتَهُمْ. 3لَمْ يَمْتَلِكُوا الأَرْضَ بِسَيْفِهِمْ وَلَا بِذِرَاعِهِمْ خَلُصُوا، وَلَكِنْ بِفَضْلِ يُمْنَاكَ وَذِرَاعِكَ وَنُورِ وَجْهِكَ، لأَنَّكَ رَضِيتَ عَنْهُمْ. 4أَنْتَ هُوَ مَلِكِي يَا اللهُ، فَمُرْ بِخَلاصِ شَعْبِكَ. 5بِعَوْنِكَ نَطْرَحُ خُصُومَنَا أَرْضاً، وَبِاسْمِكَ نَدُوسُ الْقَائِمِينَ عَلَيْنَا. 6فَإِنِّي لَنْ أَتَّكِلَ عَلَى قَوْسِي وَلَنْ يُخَلِّصَنِي سَيْفِي. 7فَأَنْتَ أَنْقَذْتَنَا مِنْ مُضَايِقِينَا وَأَلْحَقْتَ الْعَارَ بِمُبْغِضِينَا. 8بِاللهِ نَفْتَخِرُ الْيَوْمَ كُلَّهُ، وَنَحْمَدُ اسْمَكَ إِلَى الأَبَدِ.

9غَيْرَ أَنَّكَ قَدْ رَذَلْتَنَا وَأَخْجَلْتَنَا، وَلَمْ تَعُدْ تُرَافِقُ جُنُودَنَا إِلَى الْحَرْبِ. 10جَعَلْتَنَا نَتَقَهْقَرُ أَمَامَ عَدُوِّنَا. أَمَّا مُبْغِضُونَا فَيَغْنَمُونَ لأَنْفُسِهِمْ. 11أَسْلَمْتَنَا كَغَنَمٍ مُعَدَّةٍ لِلذَّبْحِ، وَبَدَّدْتَنَا بَيْنَ الأُمَمِ. 12بِعْتَ شَعْبَكَ بِلَا مَالٍ وَبِثَمَنِهِمْ لَمْ تَرْبَحْ. 13تَجْعَلُنَا عَاراً عِنْدَ جِيرَانِنَا، وَمَثَارَ هُزْءٍ وَسُخْرِيَةٍ لِمَنْ حَوْلَنَا. 14تَجْعَلُنَا مَثَلاً بَيْنَ الأُمَمِ وَأُضْحُوكَةً بَيْنَ الشُّعُوبِ. 15الْيَوْمَ كُلَّهُ خَجَلِي مَاثِلٌ أَمَامِي، وَخِزْيُ وَجْهِي قَدْ غَمَرَنِي 16مِنْ صَوْتِ الْمُعَيِّرِ وَالْمُجَدِّفِ وَمَرْأَى الْعَدُوِّ الْمُنْتَقِمِ.

17هَذَا كُلُّهُ وَقَعَ عَلَيْنَا، فَمَا نَسِينَاكَ وَلَا خُنَّا عَهْدَكَ. 18لَمْ يَرْتَدَّ قَلْبُنَا إِلَى الْوَرَاءِ، وَلَا حَادَتْ خُطْوَاتُنَا عَنْ طَرِيقِكَ. 19مَعَ أَنَّكَ سَحَقْتَنَا وَسَطَ الْوُحُوشِ، وَغَمَرْتَنَا بِظِلالِ الْمَوْتِ. 20إِنْ كُنَّا قَدْ نَسِينَا اسْمَ إِلَهِنَا، وَصَلَّيْنَا إِلَى إِلَهٍ غَرِيبٍ، 21أَلَا يَعْرِفُ اللهُ ذَلِكَ وَهُوَ عَلّامُ الغُيُوبِ؟ 22أَلَا أَنَّنَا مِنْ أَجْلِكَ نُعَانِي الْمَوْتَ طُولَ النَّهَارِ، وَقَدْ حُسِبْنَا مِثْلَ غَنَمٍ مُعَدَّةٍ لِلذَّبْحِ.

23قُمْ يَا رَبُّ. لِمَاذَا تَتَغَافَى؟ انْتَبِهْ وَلَا تَنْبِذْنَا إِلَى الأَبَدِ. 24لِمَاذَا تَحْجُبُ وَجْهَكَ وَتَنْسَى مَذَلَّتَنَا وَضِيقَنَا؟ 25إِنَّ نُفُوسَنَا قَدِ انْحَنَتْ إِلَى التُّرَابِ، وَبُطُونَنَا لَصِقَتْ بِالأَرْضِ. 26هُبَّ لِنَجْدَتِنَا وَافْدِنَا مِنْ أَجْلِ رَحْمَتِكَ.