Zaburi 33 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 33:1-22

Zaburi 33

Ukuu Na Wema Wa Mungu

133:1 Za 64:10; 101:1; 147:1; 11:7Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki;

kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.

233:2 Mwa 4:21; 1Kor 14:7; Ufu 5:8; Za 92:3; 144:9Msifuni Bwana kwa kinubi,

mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.

333:3 Za 40:3; 35:27; 47:1; Isa 42:10; Ufu 5:9; Ay 3:7Mwimbieni wimbo mpya;

pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.

433:4 Ufu 19:9; 22:6; Za 19:8; 18:25; 119:142; 25:10Maana neno la Bwana ni haki na kweli,

ni mwaminifu kwa yote atendayo.

533:5 Za 11:7; 6:4Bwana hupenda uadilifu na haki;

dunia imejaa upendo wake usiokoma.

633:6 Ebr 11:3; Kut 8:19; Mwa 1:3, 16; 2Nya 2:12; Yn 1:1-3; Ay 26:13Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa,

jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.

733:7 Mwa 1:10; Yos 3:16Ameyakusanya maji ya bahari

kama kwenye chungu;

vilindi vya bahari

ameviweka katika ghala.

833:8 Kum 6:13; 14:23; Za 2:11; 49:1; Isa 18:3; Mik 1:2Dunia yote na imwogope Bwana,

watu wote wa dunia wamche.

933:9 Za 148:5; Mwa 1:3Kwa maana Mungu alisema, na ikawa,

aliamuru na ikasimama imara.

1033:10 Isa 44:25; Za 2:1; Ay 5:12Bwana huzuia mipango ya mataifa,

hupinga makusudi ya mataifa.

1133:11 Hes 23:19; Yer 51:12, 29; Ay 23:13; Mit 19:21; Eze 38:10; Mdo 4:27, 28Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele,

makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.

1233:12 Za 144:15; 65:4; 4:3; 84:4; Kum 7:6; Kut 8:22; 34:9Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao,

watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.

1333:13 Za 53:2; 102:19; 11:4; 14:2; Ebr 4:13; 2Nya 16:9; Ay 28:24Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini

na kuwaona wanadamu wote;

1433:14 Law 15:31; 1Fal 8:39kutoka maskani mwake huwaangalia

wote wakaao duniani:

1533:15 Ay 10:8; 11:11; 10:4; Yer 32:19; Isa 64:8; Hes 7:2; Za 44:21; 119:73; Mit 24:12yeye ambaye huumba mioyo yao wote,

ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.

1633:16 1Sam 14:6Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake;

hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.

1733:17 Za 20:7Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu,

licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.

1833:18 Kut 3:16; Ay 36:7; Za 11:4; 6:4; 34:15; 1Pet 3:12Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao,

kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,

1933:19 Za 56:13; Ay 5:20; Mdo 12:11ili awaokoe na mauti,

na kuwahifadhi wakati wa njaa.

2033:20 Za 27:14Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini,

yeye ni msaada wetu na ngao yetu.

2133:21 1Sam 2:1; Yoe 2:23; Za 30:4; 99:3Mioyo yetu humshangilia,

kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.

2233:22 Za 6:4Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana,

tunapoliweka tumaini letu kwako.

New International Version

Psalms 33:1-22

Psalm 33

1Sing joyfully to the Lord, you righteous;

it is fitting for the upright to praise him.

2Praise the Lord with the harp;

make music to him on the ten-stringed lyre.

3Sing to him a new song;

play skillfully, and shout for joy.

4For the word of the Lord is right and true;

he is faithful in all he does.

5The Lord loves righteousness and justice;

the earth is full of his unfailing love.

6By the word of the Lord the heavens were made,

their starry host by the breath of his mouth.

7He gathers the waters of the sea into jars33:7 Or sea as into a heap;

he puts the deep into storehouses.

8Let all the earth fear the Lord;

let all the people of the world revere him.

9For he spoke, and it came to be;

he commanded, and it stood firm.

10The Lord foils the plans of the nations;

he thwarts the purposes of the peoples.

11But the plans of the Lord stand firm forever,

the purposes of his heart through all generations.

12Blessed is the nation whose God is the Lord,

the people he chose for his inheritance.

13From heaven the Lord looks down

and sees all mankind;

14from his dwelling place he watches

all who live on earth—

15he who forms the hearts of all,

who considers everything they do.

16No king is saved by the size of his army;

no warrior escapes by his great strength.

17A horse is a vain hope for deliverance;

despite all its great strength it cannot save.

18But the eyes of the Lord are on those who fear him,

on those whose hope is in his unfailing love,

19to deliver them from death

and keep them alive in famine.

20We wait in hope for the Lord;

he is our help and our shield.

21In him our hearts rejoice,

for we trust in his holy name.

22May your unfailing love be with us, Lord,

even as we put our hope in you.